EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, March 25, 2014

Msanii JB na Timu ya EATV Nirvana wauvamia mji wa LUSHOTO

Katika kuelekea siku ya wanawake duniani,iliyoadhimishwa Duniani kote mnamo Machi 5, kampeni ya Grow ikiongozana na mmoja wa mabalozi wake muigizaji Jacob Stephen ‘JB’ iliungana na kipindi cha EATV Nirvana na kuutembelea mji wa Lushoto,Jijini Tanga.

Kampeni ya GROW, inayoendeshwa na Oxfam, inahamasisha mabadiliko kwenye mifumo iliyopo ili iwafanufaishe wakulima na wafugaji/wavuvi wadogo wadogo hususani wanawake wawe na maisha endelevu! Inawasherekea kwa mchango wao mkubwa wa kulisha nchi huku wakipambana na changamoto nyingi ikiwemo ukosefu wa masoko, pembejeo na miundo mbinu. Katika harakati hizi, mnamo mwaka 2011, shindano la "Mama Shujaa wa Chakula " lilizinduliwa rasmi hapa nchini. Lengo la tuzo hii ni kutambua mchango wa wanawake hasa waishio vijijini.

Huko Lushoto hali ilikuwa kama picha zinavyoonyesha...
Alfajiri ya Machi 6, timu ya Nirvana, Grow, pamoja na JB walielekea soko kuu la Lushoto ambapo walikutana na wakulima ili kusikia hadithi zao za mafanikio pamoja na changamoto. Nirvana na Kampeni ya GROW wanahamasisha lifestyle njema! Lakini tunavyokula vyakula bora, vyenye virutubisho tunajua vinatoka wapi!
Akizungumza kutoka katika sehemu yake ya biashara, Zinira Ally (kushoto aliyekaa) alishuhudia jinsi ambavyo anasomesha watoto na kulisha familia yake kwa pesa inayotokana na biashara yake ya uuzaji wa mbogamboga na matunda.
"Nzenze"... Salaam na wapenzi wa filamu zikiendelea.
JB, Lotus na Deo wakitizama mazao mbalimbali katika soko kuu la Lushoto.
Veronica Joseph ambaye ni muuzaji wa mboga mboga sokoni Lushoto anasema angependa kuona mabadiliko katika miundombinu ya soko ili kulinda ubora wa mazao, “soko halina ubora, watu wananunua vyakula hivi hivi kwa bei ghali kwenye supermarket kwa sababu ya ubora, sie tunauza tu bora tunauza, tunaogopa vyakula kuoza, tungekuwa na mafriji ya kuhifadhia mboga mboga na sisi tungeweza kuuza bei sawa na supermarket.”Akiendelea kutaja changamoto, Veronica ambaye ni mama wa watoto wawili, alionyesha kusikitishwa kwake na maisha duni wanayoishi wakulima, “mkulima analima chakula ambacho wengine wanakula hadi kutupa lakini yeye hawezi hata kula mlo kamili kwa sababu kipato anachopata ni kidogo” Veronica anaamini kama, “masoko yangeboreshwa, tungeuza bidhaa kwa bei nzuri ili na sisi tusomeshe watoto wetu na kujikimu kimaisha.”
Uvuvi unalipa..??
Ugeni umefika katika meza ya Asha Paulo (Kushoto) na Shakira Rashid (kulia), hawa ni wauzaji wa samaki katika soko kuu la Lushoto. Asha na Shakira wanaelezea jinsi ambavyo mikopo kwa wakulima na wafugaji isivyokuwa rafiki. Asha anasema, “mikopo ina masharti makali sana, sidhani kama inamlenga mtu wa hali ya chini kwani makato ni makubwa sana.”
Watangazaji wa kipindi cha Nirvana, Lotus na Deo walishangaa kuona apple zinazolimwa Tanzania. Kisado kimoja ambacho kwa wastani kina ma-apple ishirini (20) kinauzwa kwa Tshs. 2000 wakati kwa wastani apple moja jijini Dar es salaam linauzwa hadi Tshs. 1000. Baada ya kuonja, Deo anashangaa kuona ladha haipishani sana na ile ya matunda hayo yanayoagizwa kutoka nje. Ukweli ni kwamba miundo mbinu, technolojia, sera na mifumo iliyopo imewaangusha wakulima hapa Tanzania! Fikiria kwamba ni rahisi na kuna faida zaidi kusafirisha apple kutoka nje ya nchi kuliko hapa hapa Lushoto Tanzania!
Paulina Isaya (mwenye nguo nyeusi), muuzaji wa matunda apple katika soko kuu la Lushoto anasema, “kama wakulima wangepewa mafunzo sahihi, mbegu bora na kuhakikishiwa masoko, hakika matunda hayo yangekuwa na kiwango kama hayo yanayoagizwa kutoka nje”.
Taswira ya soko kuu la Lushoto kwa nje.
JB akiangalia kabichi zilizowekwa pembezoni mwa barabara. (Haikujulikana mara moja kama zilikuwa zinasubiri kusafirishwa ama la)

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate