EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, March 18, 2014

TUMEJIFUNZA NINI HELIKOPTA YA CHADEMA KULINDA KURA?

 
WAKATI ninaandika makala haya, upigaji kura katika Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kalenga mkoani Iringa ulikuwa unaendelea kufanyika na kwa maana hiyo sikuwa na matokeo kuweza kujua nani ataibuka kidedea.

Lakini ninafahamu kwamba kulikuwa na ushindani mkali kati ya wagombea wa CCM (Godfrey Mgimwa) na Chadema (Grace Tendega). Ingawa wapo washiriki wengine, lakini kama ambavyo imejitokeza katika miaka ya hivi karibuni, vyama hivi ndivyo vimeonekana kuwa na ushindani mkali katika siasa za Tanzania Bara.

Vyama vyote vilifanya kampeni kubwa kuhakikisha mgombea wake anakuwa ndiye mwakilishi wa jimbo hilo ambalo limekuwa wazi kufuatia kufariki kwa mbunge wake, aliyekuwa Waziri wa Fedha, marehemu William Mgimwa mapema mwaka huu.

Kama kawaida ya siku zote, Chadema wamekuwa hawawaamini CCM, wakiamini wanacheza rafu zinazosababisha wao kushindwa katika chaguzi kadhaa. Kutokana na sababu hiyo, mara nyingi wamekuwa wakilalamikia suala hilo na kuelezea mikakati yao kuhakikisha jambo hilo halijitokezi.

Safari hii, wameibuka na kauli mpya kwamba ili kulinda kura zao, watatumia helikopta, ambayo mwanzo waliitumia katika kampeni zao, ili kuzuia upotevu wowote wa kura. Kwamba wakiwa angani, wataweza kufuatilia mwenendo wa magari yatakayokuwa yamebeba masanduku ya kura.

Ninapata shida kidogo kuwaelewa Chadema kuhusu jambo hili. Ingawa sihusiki na malumbano baina ya polisi waliozuia matumizi ya chombo hicho cha usafiri na chama hiki kikuu cha upinzani, najaribu kuangalia jinsi gani wanasiasa wanavyoweza kucheza vizuri na akili za watu ili kujizolea mashabiki.

Watu wenye akili wanajaribu kujiuliza ni kwa namna gani helikopta ile inavyoweza kulinda kura wakati zoezi la kuzihesabu hufanyika ardhini, tena ndani ya vyumba maalum? Hii, kama nilivyosema ni namna ya kujitafutia mashabiki kwa kucheza na akili zao kwa bei rahisi.

Kila chama kinao mawakala wake katika vituo vyote vya kupigia kura. Hawa ndiyo wasimamizi wakubwa wa kura, kwani kwa muda wote wako macho kuhakikisha haufanyiki udanganyifu wala hila za aina yoyote. Na kwamba baada ya zoezi la kupiga kura, wote wanapaswa kufuata taratibu zote kama zilivyoainishwa na msimamizi wa uchaguzi.
Kwa maana nyingine, helikopta ni kama inayotumika kuharibu fikra za watu juu ya kumpata mwakilishi wamtakaye, badala yake akili yao wanaiweka katika kuitazama inapopaa angani.
Hata hivyo, naamini kuwa uchaguzi huo umepita kwa amani na vyama hivyo vitakuwa na la kujifunza.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate