EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, March 17, 2014

WEMA, DIAMOND WACHAPANA


Stori: WAANDISHI WETU
Tayari kimenuka! Habari ya mjini wikiendi iliyopita ni madai ya njiwa wapendanao Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuchapana makofi laivu, Ijumaa Wikienda lina kisa na mkasa.
Diamond.
TIMBWILI STUDIO
Kwa mujibu wa shuhuda wetu aliyekuwa eneo la tukio, timbwili hilo la haja lilijiri usiku mnene kwenye studio ya kurekodia nyimbo za Bongo Fleva za Tanzania House of Talent (THT) ambapo Diamond alikuwa akirekodi wimbo wa kolabo na msanii wa Kenya, Victoria Kimani ‘Vicky’ na Omary Faraji ‘Ommy Dimpoz.
Stori ni kwamba wakati wasanii hao watatu wakifanya yao studio, Ommy alichukua kipande cha video kilichowaonesha wakiwa pamoja huku Diamond akiwa ‘veri klozi’ na Vicky kisha akakitumbukiza kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram.
Wema.
MUVI YAANZA
Hapo ndipo muvi lilipoanzia kwani ilisemekana kuwa Wema ‘Mama la Mama’ alikiona kipande hicho cha video ndipo akaunganisha na ule uvumi wa Diamond ‘kuminya kimalavu’ na Vicky walipokuwa nchini Afrika Kusini ‘Sauz’.
Ilidaiwa kuwa Wema alimtafuta shostito wake kwa sasa, Aunt Ezekiel ambaye alimuomba ‘amdraivu’ hadi katika studio hizo lakini yeye (Aunt) hakushuka kwenye gari aina ya Toyota Lexus Harrier la rangi ya pinki.

Mastaa hao wawili ambao wameurudisha uhusiano wao hivi karibuni baada ya awali kuvunjika, walijikuta kwenye ugomvi mkubwa mara tu Wema alipozama studio na kukutana na wasanii hao.
Diamond na Victoria.
UHUSIANO GANI?
Ilidaiwa kuwa Wema alipofika alimhoji Diamond ana uhusiano gani na Vicky huku akimkumbusha kuwa siku chache zilizopita kulikuwa na tuhuma za wao kuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi.
Ilisemekana kuwa mzozo huo ulianza taratibu lakini baadaye ulikuwa mkubwa hadi kufikia hatua ya kuchapana makofi huku Ommy na prodyuza Tuddy Thomas wakifanya kazi kubwa ya kuwaamulia bila mafanikio.
UGOMVI SAA MBILI
Kwa mujibu wa ‘kronometa’ yetu, ugomvi huo ulidumu kwa zaidi ya saa mbili huku Diamond akidaiwa kuichukua simu ya Wema na kuipasua chini.
Ilidaiwa kwamba wakati wawili hao wakipeana ‘nakozi’, kila mmoja alikuwa akimtupia mwenzake lugha ‘mbofumbofu’ kama ‘wewe umetembea na fulani’ huku mwingine akimwambia ‘na wewe mbona umetembea na fulani na fulani na fulani na fulani na fulani na…’.
Ilielezwa kwamba kauli hizo zilimfanya Diamond aishie kumwambia Wema kuwa yeye ndiye anamuweka mjini kwa sasa hivyo afunge mdomo wake.
Ilidaiwa kuwa Wema alipoendelea na maneno ndipo Diamond akapandwa na hasira hadi akamchania mwanadada huyo dela sehemu ya mgongoni.
“Asikwambie mtu, palichimbika kweli,” kilisema chanzo hicho.
WAACHANISHWA
Baada ya Ommy na Tuddy kufanikiwa kuwaachanisha, Wema alitoka kwa hasira kisha akatimua. Uzuri ni kwamba hakumgusa Vicky.
Baada ya kuzinyaka habari hizo, gazeti hili lilimsaka Ommy ambaye alikiri kutokea kwa ishu hiyo huku akidai ni masuala ya kawaida katika mapenzi.
Kwa upande wake Diamond simu yake iliita bila kupokelewa na hata alipotumiwa ujumbe mfupi (SMS) hakujibu.
WEMA ATOA LA MOYONI
Alipotafutwa Wema, alieleza ya moyoni juu ya sakata hilo ambapo alisema hayo ni mapenzi na ndiyo raha ya mapenzi.
“Kwenye uhusiano kugombana ndiyo raha yenyewe, mapenzi huwa hayaingiliwi nampenda na nitampenda maisha yote.
“Kama ni mjinga, taahira ndiyo tayari amekwishakuwa wangu, kumbuka kuna usemi kuwa chukua jembe ukalime,” alisema staa huyo anayeaminika kuwa maarufu zaidi kwa sasa Bongo.
DIAMOND NA VICKY
Uvumi wa kuwepo kwa uhusiano wa kimapenzi kati ya Diamond na Vicky ulivuma baada ya wawili hao kuonekana kwenye picha ya pamoja wakiwa katika One Project Campaign nchini Afrika Kusini.
Hata hivyo, wote walikana kwa nyakati tofauti.
SI MARA YA KWANZA
Kuhusu Wema na Diamond kupigana siyo mara ya kwanza kwani jamaa huyo anayeuza zaidi muziki wa Bongo Fleva aliwahi kumtoa nundu mrembo huyo enzi za uhusiano wao wa awali.
Imeandaliwa na Imelda Mtema, Musa Mateja na Shakoor Jongo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate