Katibu Mkuu wa CCM Ndugu
Abdulrahman Kinana akizungumza na Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM
Wilaya ya Kigoma Vijijini na kuwataka kufanya kazi kwa umoja na
mshikamano .
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya Kigoma Vijijini wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu
Abdulrahman Kinana akiwasalimia wakazi wa wilaya ya Kigoma Vijijini
waliokuwa nje ya ofisi za CCM Wilaya kabala ya kuelekea kwenye kijiji
cha Mahembe ambapo mkutano mkubwa wa hadhara ulifanyika.
Katibu wa NEC Itikadi na
Uenezi Nape Nnauye akizungumza na wananchi wa wilaya ya Kigoma Vijijini
akiwa pamoja na kiongozi wa Umoja wa Madereva na Makondakta wa Wilaya
hiyo Ndugu Mgaya Mustafa ambaye alitoa taarifa ya kuwepo kwa kero ya
kukamatwa Daladala kwa sababu ya kukosa sare za dereva na kondakta
ambazo kwa maelezo ya madereva hao tatizo lipo kwa aliyepewa tenda
kuchelewesha kushona.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu
Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mkungwe kata
ya Mahembe wilaya ya Kigoma Vijijini na kuwaambia Chama Cha Mapinduzi
kiahidi kinachoweza kutekelezeka hivyo ahadi ya kuwapatia maji
wanakijiji hao ipo na mkandarasi alishajenga mradi kwa asilimia 70 hivyo
watapata maji mapema iwezekanavyo.
Katibu Mkuu wa CCM
Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia mradi wa maji katika kijiji cha
Mkungwe kata ya Mahembe wilaya ya Kigoma Vijijini
Kijiji cha Mkungwe wilaya ya Kigoma Vijijini kupata maji safi na salama hivi karibuni.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu
Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kijiji cha Mahembe ambapo alitoa
sifa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.Jakaya Mrisho
Kikwete kwa kujenga madaraja makubwa matatu,Maragarasi ,Kilombero na
Kivukoni na kujenga Shule za Kata nchi nzima.
Ampongeza kwa ujenzi wa madaraja matatu
makubwa, Daraja la Malagarasi,Kilombero na Daraja la Kigamboni, Ujenzi
wa Sekondari za Kata. Nape awaambia wakazi wa kijiji cha Mahembe
wachague viongozi watakaotatua matatizo yao ya msingi kwanza na si
vinginevyo kwani takwimu zinaonyesha viongozi wengi wa upinzani
wameshindwa kutatua matatizo ya wananchi wa majimbo wanayoyaongoza.
No comments:
Post a Comment