EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, May 27, 2014

BINTI ALIYEZIKWA AIBUKIA KWAO

Stori: Joseph Ngilisho, ARUMERU
HOFU ya ushirikina imetikisa Mkoa wa Arusha kufuatia tukio la hivi karibuni ambapo mwanafunzi wa Chuo cha Kompyuta jiji hapa, Witness Obed (21) aliyefariki dunia Aprili 12, mwaka huu na kuzikwa kwenye makaburi ya nyumbani kwao Kijiji cha Nanja, Kata ya Moshono wilayani Arumeru, Arusha kuibuka akiwa hai.
Witness Obed (21) aliyefariki dunia Aprili 12 mwaka huu na kuzikwa kwenye makaburi ya nyumbani kwao Kijiji cha Nanja, mkoani Arusha na kuibuka akiwa hai tena.
Binti huyo aliibuka kwao hivi karibuni akiwa mpole na kuwafanya baadhi ya watu, wakiwemo wazazi wake kutimua mbio kwa hofu.

Watu kutoka maeneo
mbalimbali jijini hapa  wamekuwa wakimiminika nyumbani kwa wazazi wa binti huyo kwa lengo la kumshuhudia kwa vile ndugu walishaamini kuwa, mpendwa wao huyo alishakufa na alizikwa.
Umati wa watu ukiwa katika hali ya mshangao kutokana na tukio hilo.
UWAZI LATIA TIMU NYUMBANI
Baada ya kusikia taarifa hizo, Uwazi lilifunga safari mpaka eneo la tukio na kumshuhudia binti huyo kisha likaenda kwenye kaburi alilozikwa.
Kwenye kaburi hilo, msalaba wenye kuonesha siku yake ya kuzaliwa (1992) na kufa (12, Aprili, 2014) ulikuwa bado umesimama imara huku kaburi lenyewe likionesha dalili ya kutitia kidogo.
BABA MZAZI ASIMULIA
Akisimulia mkasa huo kwa mshangao mkubwa, baba mzazi wa binti huyo, Obed Leiyo alisema:
“Ilikuwa Aprili mwanzoni, binti yangu alitoweka nyumbani  baada ya kurudi kutoka chuoni majira ya saa 2 usiku akiwa amechelewa.
Hili ni kaburi alipozikwa Witness Obeid Leiyo.
Mimi kama mzazi nilimfokea kwa kuchelewa kwake kurudi nyumbani.
“Yeye kwa hasira zake alizunguka nyumba akaondoka muda huohuo na hakurudi kabisa hapa nyumbani.
“Siku iliyofuata tulianza kumtafuta maeneo mbalimbali bila mafanikio, tukatoa matangazo kwenye vyombo vya habari lakini binti yangu hakuonekana.”
TAARIFA ZAFIKA, KAFA
Mzazi huyo aliendelea kusema: “Siku moja tulipata taarifa kwamba kuna mwili wa msichana umeonekana  katika Kijiji cha Bwawani hapahapa Arumeru.
“Mimi pamoja na ndugu wengine tuliamua kwenda katika kile kijiji. Tulipofika tuliambiwa ni kweli mwili wa msichana uliokotwa lakini wananchi wakauzika.”
WAFUKUA KABURI
Baba huyo anaendelea: “Niliamua kwenda Kituo cha Polisi cha Usa River ambako niliomba kibali kwa ajili ya kufukua kaburi na kuutoa mwili ili kuutambua kama ni binti yangu au la!
“Nilipewa kibali, tukafukua kaburi na kutoa mwili. Nilimtambua kuwa ni binti yangu kutokana na alama mbalimbali alizokuwa nazo, ikiwemo rangi kwenye kucha na sehemu ya kushoto ya uso ilikuwa nyeusi kwa sababu aliwahi kupooza.
Witness akiwa na baba yake mzazi, Bw. Obeid Leiyo Mara baada ya kurudi nyumbani akiwa hai.
MWILI WASAFIRISHWA, WAZIKWA
Baba huyo wa Witness alizidi kueleza kuwa waliusafirisha mwili huo hadi nyumbani kwake Moshono na kuandaa taratibu za mazishi ambapo Aprili 23, mwaka huu mwili ulizikwa.
AIBUKA GHAFLA
Hata hivyo, Obed anasema alishangaa siku ya tukio kumwona binti yake huyo akiibuka nyumbani hapo akiwa hai jambo ambalo lilimshangaza na kumfanya akimbie kwanza na baadaye kufanya mawasiliano naye.
BINTI ASIMULIA
Akizungumza na Uwazi, binti huyo alikiri kutoweka nyumbani kwao Aprili 15, mwaka huu na kwenda kusikojulikana.
Alisema hakujua kilichoendelea baada ya kuondoka nyumbani lakini baadaye alibaini kuwa alikuwa katika Kijiji cha Olkokola wilayani Arumeru na alikwenda kwenye nyumba ya mwanamke mmoja asiyefahamiana naye akamuomba maji ya kunywa.
“Nilifika kwenye nyumba moja nikamkuta mama mmoja, nikamwomba maji ya kunywa akaenda kuniletea. Nilikunywa huku amenisimamia, lakini maji yalikuwa machungu sana, nikamrudishia, akanilazimisha ninywe kwa kunisukumia kikombe kinywani. Nilipomaliza nilipoteza fahamu.
“Baadaye nilizinduka, nikaendelea kuishi palepale nyumbani kwa yule mama  lakini sifahamu nilikuwa nafanya nini.
“Juzi ndiyo nikashangaa
kujikuta nimerudi nyumbani, mimi sijui nini kilikuwa kikiendelea,” alisema binti huyo.
MAJIRANI NAO
Majirani kadhaa waliokuwepo nyumbani kwa Obed walilielezea tukio hilo kwamba ni la ushirikina huku wakisema ni jambo la kuogofya ambalo halikuwahi kutokea kijijini hapo kabla.
Wengine walisema kuwa binti huyo alifufuka na wengine walisema alichukuliwa msukule.
“Hili si suala la kawaida lazima kuna ushirikina kwani huyu binti tulishamzika na wazazi wake walimtambua kabisa kuwa ni yeye baada ya
kuambiwa alikutwa amekufa, sasa hebu fikiria tangu tumezika mbona hakuna mtu aliyekuja na kusema na yeye alipotelewa na binti yake halafu cha ajabu hilo kaburi mbona limebonyea? Atakuwa amefufuka,’ alisema mkazi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Amina Liwa.
Mkuu wa Polisi wa Kituo cha Usa River, Benedict Mpujila amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema uchunguzi unafanyika.
KUMBUKUMBU
Mapema mwaka jana tukio la kishirikina liliibuka katika wilayani Arumeru eneo la Kwa Mrefu ambapo mtu mmoja alidaiwa kudondoka na ungo, muda mfupi baadaye alitoweka na kwenye ungo kubaki mayai na kuku mweupe.CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate