EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, June 2, 2014

DAU LA MAXIMO LAIHENYESHA YANGA, MANJI ASEMA ‘ATAKUFA NAYE’


Na Renatus Mahima, DAR ES SALAAM KOCHA Mbrazil Marcio Maximo, aliyekuwa kocha wa timu ya taifa (Taifa Stars), muda wowote atatua nchini na kusaini mkataba wa kukinoa kikosi cha Yanga katika msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika, imefahamika. Uongozi wa Yanga katika mkutano mkuu wa dharura wa wanachama iiliofanyika kwenye Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay jijini hapa jana, umesema umekuwa na mazungumzo ya muda mrefu na kocha huyo ili achukue kandarasi ya kuinoa timu yao.
Atakuja? Kocha wa zamani wa Taifa Stars, Marcio Maximo anatakiwa na Yanga SC
"Tunapenda kuwaataarifu wanachama wa Yanga kwamba tuna mpango wa kumleta Maximo kuifundisha timu yetu msimu ujao. Tumekuwa  na mazungumzo naye kwa miezi miwili sasa tukimwomba apungumze kidogo mshahara," amesema Yusuph Manji, Mwenyekiti wa Yanga. "Zoezi la usajili linakwenda vizuri. Hatusajili wachezaji wengi kwa sababu kikosi chetu cha msimu uliopita ni kizuri ndiyo tukaifunga hadi Al Ahly ya Misri. Tunachokifanya kwa sasa ni kurekebisha maeneo ambayo tumebaini kuwa na upungufu. "Wachezaji wote wanasajiliwa makao makuu ya klabu ili kuepuka matatizo ambayo yamejitokeza huko nyuma," amesema zaidi kiongozi huyo. Maximo, raia wa Brazil aliiongoza Taifa Starsb kwa mafanikio makubwa akisifika kama 'mhamasishaji' kutokana na Watanzania wengi kuingia viwanjani kuiona timu yao ya taifa ikicheza dhidi ya timu mbalimbali. Hamasa ya Watanzania kuishangilia ilianza kupungua baada ya kuondoka kwa kocha huyo na mikoba yake kuchukuliwa na Jan Poulsen ambaye baadaye arithiwa na Mdenmark mwenzake Kim Poulsen aliyetimuliwa mwanzoni mwa mwaka huu. Taifa Stars kwa sasa iko chini ya Mholanzi Mart Nooij na Yanga haina kocha mkuu baada ya kuondoka kwa Mholanzi Hans van der Pluijm Aprili mwaka huu. Aidha, katika mkutano huo wanachama wamepitisha kuingizwa kwa kipengele katika Katiba ya Yanga kinachotaka klabu hiyo iwe na Kamati ya Maadili kama ilivyoagizwa na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka (TFF) Desemba mwaka jana. Kipengele kilichopitishwa kinasema: "Kutakuwa na Kamati nya Maadili itakayokuwa na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na wajumbe watatu watakaoteuliwa na Kamati ya Utendaji na muda wao hautazidi mwaka mmoja. Mwenyekiti lazima na taaluma ya sheria." "Kazi za chombo hiki zitasimamiwa na Katiba ya Yanga na Kanuni za Maadili za Yanga na endapo hazitajitosheleza, Kanuni za Maadili za TFF zitatumika ipasavyo. "Rufaa zote kutoka Kamati ya Maadili zitasikilizwa na Kamati ya Rufaa ya Maadili ya TFF." Aidha, wakati Mwenyekiti wa Yanga akitengua kauli yake ya kutowania tena uongozi, uchaguzi mkuu wa klabu hiyo sasa umepangwa kufanyika Juni 15 mwakani. Wanachama wa Yanga katika mkutano mkuu wa dharura wa marekebisho ya Katiba kwenhye Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay jijini hapa leo, wamekubaliana uchaguzi mkuu wa klabu hiyo ambao awali ulikuwa umepangwa kufanyika Juni 15 mwaka huu ufanyike mwakani ili kupishya shughuli mbalimbali za maendeleo ya klabu hiyo ikiwamo marekebisho ya Katiba na michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL). Novemba mwaka jana, Manji alitangaza kutowania tena uongozi ndani ya klabu hiyo ili kupisha watu wengine waiongoze klabu hiyo kongwe nchini katika kile alichokieleza kuwa kutimiza matakwa ya demokrasia. Lakini, baada ya ajenda kuu ya mkutano mkuu wa jana kuingiza kipengele cha kuunda Kamati ya Maadili ya Yanga kama ilivyoagizwa na Shirikisho la Soka nchini (TFF) Desemba mwaka jana, wanachama wa Yanga katika kujadili mengineyo waliamua kuwaondoa mkutanoni kwa muda wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo ili kujadili kauli yao ya kutowania tena uongozi. Baada ya hoja hizo kujadiliwa huku wanachama mbalimbali akiwamo 'mzungu' Javet Peytov mwenye kadi ya uanachama Na. 009472, wakisimama na kuchagia, wajumbe hao walilazimika kufuta kauli hiyo na kurudhia kuwania tena uongozi katika uchaguzi mkuu ujao.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate