EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, July 9, 2014

Adui 5 wa Maximo watajwa


Kocha wa Yanga, Marcio Maximo kutoka Brazil.
CHANZO: CHAMPIONI JUMATANO
ADUI watano ambao watampa shida kubwa Kocha wa Yanga, Marcio Maximo kutoka Brazil, wametajwa na wengine wamo ndani ya Yanga na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Wachambuzi watatu maarufu wa soka nchini, Edibily Lunyamila, Bakari Malima na Saleh Ally, wameeleza kuwa, adui hao kwa Maximo ni viwanja vibovu, waamuzi wabovu, hujuma, uzalendo mikoani na presha ya Simba.

Wakijibu maswali kuhusiana na ujio wa Maximo katika klabu, wote walieleza kuhusiana na masuala ambayo yatampa wakati mgumu Mbrazili huyo na anapaswa kupambana vilivyo kuwashinda adui hai.
“Viwanja ni changamoto kubwa, haitakuwa rahisi kwake kama ilivyokuwa kwa Taifa Stars ambayo ilikuwa ikifanya mazoezini na kucheza mechi zake kwenye Uwanja wa Taifa.
“Waamuzi watakuwa adui mwingine wa Maximo, unajua viwango vyao vilivyo na hili liko ndani ya TFF na chama cha waamuzi hao. Walifanyie kazi kwa kuwa halitamkuta Maximo tu, hata makocha
wengine na wamekuwa wakilalamika.

“Nafikiri kuna vitu vingine ana taarifa navyo, lakini ni lazima uongozi wa Yanga ukae na kumueleza kuhusiana na hali halisi, hasa kama atakwenda mikoani,” alisema Lunyamila, ambaye pia ni winga hatari wa zamani wa Yanga, Simba, Mtibwa Sugar na Taifa Stars.
Kuhusiana na hilo, Malima, beki wa zamani wa Pan African, Yanga, Simba na Taifa Stars, alisema:
“Kweli kuna watu wapo tayari kuihujumu Yanga bila kujali wao ni Yanga, hii itakuwa ni moja ya vitu ambavyo vinaweza kumtokea, ingawa uongozi unatakiwa kukaa karibu na kudhibiti hili, si wote wanaupenda uongozi wa klabu.
“Pili mikoani, kuna suala la uzalendo. Wakati sisi tunacheza tumekutana nalo hili na mtu anaweza kuwapiga chenga mabeki na kipa, akafunga halafu mwamuzi akasema ameotea. Haya mambo yanatokea.

“Kingine uongozi uwe makini kumuweka vizuri kisaikolojia kwamba mashabiki sasa watakuwa wakimzomea vibaya na si kumuunga mkono kama ilivyokuwa timu ya taifa. Vizuri akajua mapema kusudi siku moja asije akamvaa shabiki au mwamuzi.”
Kwa upande wa Saleh Ally, ambaye ni mmoja wa wachambuzi wakongwe zaidi wa soka nchini, alisisitiza kuwa, presha kubwa kutoka Simba ni kati ya hao maadui watano.
“Kweli pia waamuzi, viwanja kitu ambacho Maximo ameshaanza kukiona na hujuma ni mambo ambayo yanaziandama klabu na wakati mwingine wanahujumiana wao kwa wao. Mwisho muathirika anakuwa kocha,” alisema Saleh Ally (soma uchambuzi wake uk 9).
Tayari Maximo ameanza kuinoa Yanga kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Bara. Msimu uliopita, Yanga ilimaliza ikiwa katika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Azam FC ambao walichukua kombe hilo kwa mara ya kwanza.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate