EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, July 17, 2014

LULU AWEHUKA UKUMBINI

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
Mchecheto! Staa wa sinema za Bongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’, hivi karibuni alijikuta akiendelea kuwehukia penzi la mwanamuziki Mkanada anayefanya shughuli zake nchini Marekani, Justin Drew Bieber (20), Amani  lina cha kushika mkononi.
Staa wa sinema za Bongo, Elizabeth Michael Kimemeta ‘Lulu’,
Ishu hiyo ilitokea Julai 14, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa BoT uliopo maeneo ya Posta jijini Dar es Salaam ambapo wasanii wa Marekani waliotinga Bongo kwa mwiliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete ‘JK’ walikuwa wakitoa semina kwa wasanii wa Bongo.

Lulu ambaye kwa miaka mingi amekuwa akiweka wazi mapenzi yake kwa Bieber alifika ndani ya ukumbi huo na kumwambia staa mwenzake wa sinema, Zuweza Mohamed ‘Shilole’ kwamba lengo la kufika kwake ni kuwaomba wasanii hao namba za simu za Bieber.
ILIKUWAJE?
Semina hiyo ilikuwa na lengo la kutoa mbinu za namna ya kukuza na kupanua soko la muziki na sanaa zote Tanzania.
Semina ilianza saa 3:00 asubuhi na wasanii wa Bongo waliitikia wito kwa kufika mapema, lakini Lulu alizama ukumbini hapo saa 8:12 mchana.
Justin Bieber
AINGIA KWA MBWEMBWE
Lulu alishuhudiwa akiwasili ndani ya ukumbi huo kwa  mbwembwe nyingi huku akimwambia Shilole kwamba ametia timu kwa lengo la kuchukua namba za simu za mpenzi wake wa moyoni, Bieber kwa  vile alijua miongoni mwa Wamarekani hao lazima mmoja atakuwa na mawasiliano ya msanii huyo.
HATUA KWA HATUA NA AMANI
Mwanahabari wetu, baada ya kuyanasa mazungumzo ya Lulu kwa Shilole, alianza kumfuatilia staa huyo hatua kwa hatua kama kweli atamvaa mmoja wa wasanii hao na kumuomba namba za simu za Bieber!
Lulu alikwenda kukaa kwenye kiti mbele kidogo huku wasanii wengine wa Bongo wakiwa kwa nyuma yake na akaanza kufuatilia semina hiyo ilivyokuwa ikiendeshwa kwa usahihi.
Muigizaji na Mtangazaji wa kituo cha televisheni cha E! cha nchini Marekani, Terrence J akiongea mbele ya wasanii wa Bongo leo.
JINA LA BIEBER LATAJWA, LULU ASHTUKA
Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mtoa semina mmoja alilitaja jina la Bieber katika mfano wa maelezo ya kuzingatia, ndipo Lulu akashtuka na kujishika sehemu ya kushoto kifuani kisha akamwelekea meneja wa Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ’Diamond’, Babu Tale ambaye alikuwa karibu yake na kumwambia maneno haya: “Naona sasa hawa Wamarekani wanaanza kugusa ninapopataka mimi.”
BAADA YA SEMINA
Baada ya semina kumalizika, baadhi ya wasanii wa Bongo walipiga picha za pozi na Wamarekani hao huku Lulu akienda chemba kuzungumza na Diamond, jambo lililotafsirika kuwa huenda alitaka msanii huyo amfanyie wepesi wa kukutana na Wamarekani hao kwa vile yeye alikuwa huko hivi karibuni akiwania Tuzo za BET.
Terrence J na Shaka Zulu (kulia).
LULU AONDOKA KIMYAKIMYA
Mpaka mwisho, Lulu aliondoka kimyakimya tofauti na alivyowasili huku paparazi wetu akiendelea kumfuatilia.
AMANI LAMVUTIA WAYA
Baadaye mwandishi wetu alimpigia simu ya mkononi staa huyo na kumuulizia kama alikipata alichokuwa amekikamia ndani ya ukumbi huo.Paparazi: “Lulu nilikusikia pale ukumbini ukimwambia Shilole kuwa lengo lako kubwa la kwenda ni kuipata namba ya simu ya Justin  Bieber, vipi uliipata?”
Lulu: “Of course ni kweli nimekuwa nikimpenda Bieber tangu alipoibuka na Wabongo wanajua hilo, maana nimekuwa nikimsifia na kumzungumzia, ila pale ukumbini nilipongia Shilole ndiye alianza kwa kuniambia nimekwenda kuchukua namba ya Bieber.
Prodyuza David Banner akizungumza jambo na wasanii kwenye semina iliyofanyika leo.
“Hata mimi nilimkubalia kuwa ninavizia watakapomaliza kutoa semina niipate namba ya Bieber lakini sikumaanisha sana jamani!”
Paparazi: “Je, ulipokwenda kuongea na Diamond nini ilikuwa hoja yako kwake, akuunganishe nao?”
Lulu: “Mambo mengine bwana. Kuna wakati Shaka Zulu (mmoja wa wagane hao) naye alimzungumzia Justin Bieber na baada ya kutaja jina tu nilishtuka sana, nilitaka nione akina Diamond watasemaje?”
KUMBUKUMBU ZA LULU
Mwaka 2011 baadhi ya magazeti pendwa ya Bongo sanjari na mitandao ya kijamii yaliripoti jinsi Lulu alivyopagawa na mwanamuziki huyo kiasi cha kushindwa kuvumilia na kujianika kwenye ukurasa wake wa Twitter.
Lulu alikwenda mbele zaidi kwa kudai kuwa, kwa jinsi anavyompenda staa huyo alikuwa tayari kumpa chochote kile (hakufafanua). Alikuwa ‘akitwiti’ kwa Kiswahili wakati mwingine akitumia ‘yai’ (Kingereza).
Katika maelezo yake Lulu alikaririwa akisema kuwa endapo staa huyo atatua Bongo, atatembea utupu kutoka nyumbani hadi sehemu ambayo Bieber atakuwa anapafomu.
Bieber mwenyewe anadaiwa kuwa na mashabiki zaidi ya 47,180,630 wanaomfuatilia kwenye Twitter hivyo huenda ilikuwa vigumu kumsoma Lulu.
KAMA VILE HAITOSHI
Hivi karibuni ambapo hata mwezi mmoja haujapita wakati Diamond akiwa nchini Marekani kwenye Tuzo za BET, Lulu alimtupia kwenye Instagram maneno haya: “Hongera kwa levo uliyofikia. Huko ulinionea Justin Bieber wangu?”
NADRA SANA, KWA LULU VIPI?
Ni nadra katika jamii ya Kiafrika mwanamke kuanika hisia za mapenzi yake kwa mwanaume asiyekuwa na habari naye huku jamii ikijua au kutambua hilo lakini Lulu amethubutu. Je, inakuwaje hapo?
Wewe msomaji tuma maoni yako uelezee unachokielewa kwa Lulu kuhusu kujianika huko kwenda namba;  0655 207520.

JIUNGE NA GLOBAL BREAKING NEWS!



No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate