EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 29, 2014

YATIMA AOTA NYAMA YA AJABU ANA UMRI WA MIAKA 16 KILA ANAYEMLEA HUFARIKI DUNIA


CHANZO NI GLOBAL PUBLISHERS
Kwa kweli duniani kuna mateso, lakini ya mtoto huyu yatima ni makali na maisha yake yapo hatarini kama hatawahi kupata matibabu. Fuatilia mkasa wake hapa chini ambao naamini utakuhuzunisha.
Kijana Twaha Sultan akiwa na maumivu makali.
Kijana Twaha Sultan (16) ambaye ni yatima mkazi wa Kipawa Karakata, Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam akisimulia mkasa wake alikuwa na haya ya kusema:
“Ndugu zangu, kufuatia maradhi ya ajabu yanayonisumbua sina raha ya maisha, niheri ningewafuata wazazi wangu waliotangulia mbele ya haki nikapumzike.“Nimekuwa mtu wa maumivu wakati wote, kulala na kula kwangu ni shida tupu mbaya zaidi ndugu ninaoishi nao hawana uwezo.

“Naamini kama wangekuwa na uwezo huenda ningekuwa nimepona maradhi haya yaliyoanza kama utani baada ya kunipeleka katika hospitali kubwa na kupatiwa tiba ya uhakika, kwa kweli nateseka jamani!
“Naumia zaidi ninapowaona vijana wa umri wangu wakiwa wanasoma na wenye furaha, wakati mimi nateswa na haya maradhi ambapo nisipopata tiba hatima yangu itakuwa kifo.
“Kabla ya kuanza kuugua, nilikuwa naishi na wazazi wangu huko Majengo, mkoani Tanga, bahati mbaya mwaka 2000 walitengana.
Akionyesha nyama ya ajabu iliyomuota kijana.
“Kufuatia kutengana kwao, mama alinichukuwa tukaja hapa jijini Dar kwa mama mkubwa tukaanza maisha mapya bila baba.“Tukiwa tunaendelea na maisha, Desemba mwaka huo, mama mkubwa aliugua na kufariki dunia, kifo chake kilikuwa pigo kubwa kwetu kwani tulikuwa tukimtegemea kwa kila kitu.
“Kufuatia tuliyekuwa tukimtegemea kufariki, mimi na mama tulianza kuishi maisha ya kubangaiza, ilipofika Mei 21, 2002 mama naye akafariki dunia baada ya kuuguwa kwa muda mfupi.
“Nilibaki peke yangu, babu alinichukuwa tukaenda kuishi Banana, Ukonga lakini haukupita muda mrefu aliugua na kufariki dunia na kuniacha nikiwa darasa la tano katika Shule ya Msingi Kitunda.
“Baada ya babu kufariki, nilikosa pa kuishi ilibidi nichukuliwe na babu mwingine aliyekuwa akiishi Korogwe, Tanga. Hata hivyo, babu huyo hakuwa na uwezo kwani alikuwa mzee sana, alifariki akiwa na umri wa miaka 78.
“Wakati babu anakufa ndipo nilianza kupata uvimbe kiunoni kwa nyuma.
“Awali nilidhani ungeisha lakini kadiri siku zilivyosonga mbele uliongezeka.
“Nikawa napata maumivu makali na kushindwa kujisaidia haja ndogo, kwani mkojo ulikuwa hautoki. Siku moja nilikwenda  kwa mwenyekiti wa kijiji chetu cha Mgombezi ili anisaidie matibabu. Aliniandikia barua ya kuomba fedha kwa watu lakini sikufanikiwa.

.....akizidi kuonyesha kwa ukaribu.
“Nilipoona hali si nzuri na sina fedha, niliamua kwenda Hospitali ya Wilaya Korogwe (Magunga), nikalazwa kwa wiki mbili. Walitoboa tumbo na kuniwekea mpira wa kutolea haja ndogo, cha kushangaza maumivu yakazidi kuwa makali zaidi.
“Ndipo mtoto wa marehemu mama mkubwa, Salha Magamba alisikia kilio changu akanitumia nauli na kuja tena hapa kwake Dar.“Nilimkuta anaishi maisha duni kwa kutembeza biashara ya mkononi huku akiishi katika chumba kimoja na mwanaye. Mei 14, mwaka huu alinipeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili kutibiwa ambapo madaktari waliangalia jinsi ya kuweka mpira vizuri. Wakati huo uvimbe nao ulikuwa mkubwa karibia kilo mbili na nusu.
“Nililazwa Jengo la Kibasila Wadi ya 14, nilifanyiwa kipimo cha CT Scan lakini vipimo vingine niliambiwa vibovu. Dada alinipeleka Hospitali ya Tumaini (Dar) ambapo kipimo kilikuwa shilingi 200,000 kwa hiyo sikufanyiwa kwa kukosa fedha hizo.
“Kuanzia hapo nimekuwa nikibadilishiwa mpira kila baada ya wiki mbili kwa shilingi 30,000. Kwa upande wa uvimbe mgongoni ambao unaniuma kupita kiasi bado matibabu yake kwani nasubiri majibu, sijui itakuwa shilingi ngapi!”
Ndugu msomaji, bila shaka umesikia kilio cha kijana Twaha. Kwa kifupi anahitaji sana msaada ili kuokoa maisha yake. Kama umeguswa msaidie fedha kupitia namba 0713-970 491 au 0789-288 743.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate