EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, July 26, 2014

YEMI, SHILOLE KUFANYA MAAJABU TAIFA


WAKATI hamu ya mashabiki kila kona kwa sasa ni Agosti 8, mwaka huu katika tamasha kubwa la kihistoria la Usiku wa Matumaini litakalofanyia Uwanja wa Taifa jijini Dar, mashabiki wengi wanatamani kuwaona wakali kibao wakipanda jukwaani na kupiga nyimbo zao kali.
Diva wa muziki kutoka Nigeria anayetamba na wimbo wa Johnny, Yemi Alade
Good newz ni kwamba Zuwena Mohamed ‘Shilole’ atapanda jukwaa moja na diva wa muziki kutoka Nigeria anayetamba na wimbo wa Johnny, Yemi Alade kudondosha shoo ya kihistoria.
Uzuri wa wasanii hao wawili ndiyo unashawishi watu wengi kufika katika tamasha hilo lenye lengo ya kuchangia mfuko wa elimu nchini.

Unataka kujua sifa za wasanii hao? Hizi hapa:
Shilole ambaye wengi wamezoea kumwita  Shishi Baby, amekuwa habahatishi jukwaani kwa jinsi anavyojua kuwapagawisha, hivyo mashabiki wategemee sapraizi kibao kutoka kwa bidada huyo kwenye sekta maalum ya kukata mauno na kuacha watu midomo wazi.
Kwa upande wake, Yemi Alade anatisha balaa. Staili ya Johnny ndiyo atakayoinesha siku hiyo huku akichungulia kwa kumtafuta Johnny uwanjani mpaka atakapofanikiwa kumuona na kurudi naye Nigeria kama alivyoahidi.
NGOMA ZAO
Pata picha kwa Shilole atapopanda na kupiga nyimbo zake kali kama Chuna Buzi, Lawama, Nakomaa na Jiji, Paka la Baa na Namchukua inayotamba kwa sasa, hakika patakuwa hapatoshi kwani Shilole amesema hatabakisha kitu siku hiyo.

Zuwena Mohamed ‘Shilole’
Bidada Yemi Alade atashuka na ngoma inayotamba Afrika, Johnny kisha atazidondosha kali nyingine ambazo zimetokea kuiteka Afrika kama GhenGhenLove, Bamboo, Show Me na Tangerine.
MADANSA
Shilole ameahidi kudondoka na madansa wake ambapo watakuwa naye sambamba jukwaani katika kukamua siku hiyo.

“Mashabiki wategemee kuona mpangilio na staili tofauti kutoka kwa masteji shoo hao ambazo zitakuwa funika bovu,” alisema Shilole.
Yemi naye hatakuwa nyuma katika eneo hilo, ameahidi kucheza sambamba na madansa wake siku hiyo. Kama ilivyo kwenye makamuzi yake kupitia video ya Johnny na Tangerine ambapo madensa wake wanaonekana wakikamua mwanzo mwisho.
WENGINE
Mratibu wa tamasha hilo, Luqman Maloto amefunguka kuwa mbali na shoo hiyo kali, utamu zaidi utakolezwa zaidi na mastaa wakali wa Bongo Fleva wakiongozwa na mfalme, Saleh Ally ‘Ali Kiba’, Meninah, Madee, R.O.M.A Mkatoliki, Scorpion Girls, Juma Nature na kundi zima la TMK Wanaume Halisi.
“Kila msanii atakayepanda jukwaani atahakikisha anapiga nyimbo zake zote ndipo ampishe mwenzake, itakuwa ni jiwe baada ya jiwe,” alisema Maloto.

Aidha, tamasha hilo litapambwa na mechi za mpira wa miguu kati ya wabunge mashabiki wa Simba na wenzao wa Yanga, Bongo Fleva na Bongo Movie pamoja na mapambano kibao ya ndondi, burudani zote hizo mashabiki watazipata kwa kiingilio cha shilingi elfu tano.
Tamasha hilo limedhaminiwa na E.FM, Clouds FM, Times FM, Vodacom, Pepsi, Azam TV na SYSCORP.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate