EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, August 12, 2014

Bunge Maalumu mtegoni tena kuanzia leo

 
Dodoma.
Mjadala kuhusu masuala ya Muungano unatarajiwa kurejea upya katika kamati za Bunge Maalumu leo, wakati zitakapoanza kujadili sura za saba, nane, kumi na moja, 18 na 15 za Rasimu ya Katiba.
Kamati zimepewa siku sita kujadili sura hizo tano ambazo zina jumla ya ibara 79, huku miongoni mwake zikigusa masuala mengi ambayo msingi wake umejengwa juu ya mfumo wa serikali tatu.
Miongoni mwa masuala hayo ni pamoja na baraza la mawaziri, tume ya kusimamia na kuratibu uhusiano baina ya Serikali ya Muungano na Serikali za Nchi Washirika (Tanganyika na Zanzibar), Sekretarieti ya Tume ya Uhusiano na Uratibu, Masuala yanayohusu Benki Kuu na Fedha pamoja na uteuzi wa watumishi katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Suala la aina ya muungano lilianza kujadiliwa katika sura ya kwanza na ya sita katika awamu ya kwanza ya Bunge iliyomalizika mwishoni mwa Aprili mwaka huu na kuzua mvutano mkali ambao hatimaye ulisababisha baadhi ya wajumbe wa Bunge Maalumu kususia mchakato huo.
Wajumbe hao ni wale wanaotokana na vyama vya siasa vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambao wanataka mapendekezo yaliyomo kwenye Rasimu ya Katiba ya kuwapo kwa muundo wa serikali tatu yabaki kama yalivyo na upande mwingine unaowajumuisha wabunge wengi wa CCM ukitaka muundo wa sasa wa Serikali mbili uendelee.
Kutokana na mvutano huo, Bunge Maalumu liliahirisha upigaji kura kuamua aina ya muundo unaofaa, lakini hata liliporejea Agosti 5, mwaka huu halikuweza kupiga kura, badala yake lilibadilisha kanuni ili kuwezesha upigaji kura kufanyika baada ya kumaliza mjadala wa sura zote ndani ya kamati. 
Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad alisema hakuna maelekezo yoyote yaliyotolewa kwa wajumbe kuhusu jinsi ya kujadili masuala yanayohusu muungano na kwamba wajumbe watazingatia mapendekezo waliyoyatoa katika rasimu ya kwanza na ya sita.

“Sidhani kama ni wajibu wetu kutoa maelekezo yoyote, kinachoweza kutokea ni wajumbe kuzingatia kila walichokijadili na kukubaliana katika sura zile za awali, kama walikubali serikali ya shirikisho watazingatia hilo, kama walikubaliana serikali mbili watazingatia hilo pia,” alisema Hamad.

Itakumbukwa kwamba idadi kubwa ya kamati baada ya kujadili sura ya kwanza na ya sita zinazohusu aina ya muungano, zilipendekeza kuachana na muundo wa shirikisho na kuwasilisha maoni yanayotaka kuendelea kwa mfumo wa Serikali mbili. Kamati nyingi zilipata idadi ya kura za kutosha kuunga mkono mapendekezo hayo na chache zilikosa theluthi mbili kutoka kwa wajumbe wa Tanzania Bara na Zanzibar.

Ikiwa kamati hizo zitazingatia uamuzi wake wa awali, basi masuala yote yanayogusa serikali tatu yatafutwa, hivyo zitakuwa na kazi kubwa ya kuandika upya ibara nyingi zinazozingatia utekelezaji wa mfumo serikali mbili.
Maudhui ya Ibara
Ibara ya 98 ya Rasimu pamoja na mambo mengine, inazungumzia idadi ya mawaziri ambao idadi yao hawapaswi kuzidi 15, huku uteuzi wao ukipendekezwa uthibitishwe na Bunge.

Ibara ya 99 inazungumzia uwepo wa Waziri Mwandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano atakayeteuliwa na Rais na kuthibitishwa na Bunge, wakati Ibara ya 100 (1) inasomeka kuwa: “Waziri Mwandamizi atakuwa na madaraka ya udhibiti na usimamizi wa utekelezaji wa shughuli za serikali za siku hadi siku.” Katika sura ya nane inayozungumzia uhusiano na uratibu wa serikali, Rasimu inapendekeza kuanzishwa kwa tume ya kusimamia na kuratibu uhusiano baina ya Serikali ya Muungano na Serikali za Nchi washirika.
Tume hiyo iliyopewa jina la “Tume ya Uhusiano na Uratibu wa Serikali”, wajumbe wake ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ambaye atakuwa Mwenyekiti, Rais wa Tanganyika, Rais wa Zanzibar, Mawaziri Wakazi wanaoziwakilisha nchi washirika katika Serikali ya Muungano na waziri mwenye dhamana ya mambo ya nje wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano.
Ibara ya 110 inabainisha kazi za tume hiyo, utaratibu bora na endelevu wa kushauriana na kushirikiana baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali za Nchi Washirika pamoja na kukuza na kuwezesha uratibu na ushirikiano miongoni mwa nchi washirika kuhusu mambo yasiyo ya Muungano. Ibara ya 229 inazungumzia masuala ya fedha na jinsi nchi washirika wa muungano zinavyoweza kukopa fedha kutoka ndani na nje ya nchi wakati Ibara ya 234 inapendekeza Serikali za Nchi Washirika kuwa na Benki zitakazokuwa na jukumu la kutunza akaunti ya fedha za serikali ya nchi mshirika husika na kusimamia sera za kifedha.
Ibara ya 237 iliyopo katika Sura ya 15 inazungumzia uwapo wa Baraza la Ulinzi na Usalama la Taifa litakalokuwa na wajumbe kadhaa wakiwamo Makamu wa Rais, Rais wa Tanganyika, Rais wa Zanzibar na Waziri mwenye dhamana ya ulinzi.
Akizungumzia sura hiyo mtaalamu wa sayansi ya siasa na utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Alexander Makulilo alisema Watanzania wasitarajie miujiza katika mijadala inayogusia muundo wa Serikali.
“Wakati wakijadili sura ya kwanza na ya sita zilizokuwa zikigusia masuala ya muungano wajumbe walikubaliana juu ya muundo wa serikali mbili, licha ya kuwa hawakupiga kura ya pamoja kuamua jambo hilo,” alisema na kuongeza:
“Kwa hiyo katika sura hii ya nane, mtizamo wao utakuwa uleule kama ilivyokuwa sura mbili zilizopita. Hakutakuwa na mvutano mkubwa kwa sababu awali walishakubaliana kuhusu muundo wa serikali mbili. Watanzania wategemee hivyo.”
Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata) ambalo limeweka kambi Dodoma kushinikiza Bunge hilo kusitishwa, Deus Kibamba alisema Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilishatoa mwelekeo wa kuijadili rasimu hiyo lakini haufuatwi.
“Tume ilisema sura ya sita, nane, 10 na 12 zinazungumzia muundo wa Serikali na zijadiliwe kwa pamoja ili upatikane mwafaka, ushauri ambao haukufuatwa. Kesho (leo) mvutano utakuwa mkubwa kutokana na hali halisi iliyopo juu ya muundo wa serikali,” alisema.
*Maelezo ya nyongeza na Fidelis Butahe
CHANZO NI GAZETI LA MWANANCHI

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate