EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, August 25, 2014

MAKANISA SINGIDA YAONYA MATUSI NA UBAGUZI BUNGENI‏

DSC00479Askofu wa kanisa la Evanglist Assembels of God Tanzania (E.A.G.T) Singida mjini, John Mafwimbo akizungumza kwenye mkutano wa Injili uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ukombozi mjini Singida.Pamoja na mambo mengi, askofu Mafwimbo amewasihi wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, kufanya mambo waliyotumwa na Watanzania na si vinginevyo.

Mchungaji wa kanisa la Free Pentekoste Tanzania Singida mjini, Boniface Ntandu, akiwahubiria waumini wa madhehebu ya dini mbalimbali waliohudhuria mkutano wa injili uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ukombozi.

DSC00471
Na Nathaniel Limu, Singida
Makanisa ya Kipentekoste mkoani Singida, yameungana na Watanzania wengine kuwaomba wajumbe wa Bunge Maalum la kuandaa Katiba mpya,kujiepusha na mambo/vitendo ambavyo hawakutumwa na wananchi na badala yake washikamane na wavumiliane ili waweze kufanikisha kupatikana kwa katiba itakayoendeleza amani na utulivu uliopo nchini.
Makanisa hayo ambayo ni pamoja na Free Pentekoste Tanzania na Evangelist Assembles of God Tanzania (E.A.G.T.),yamedai kwamba matusi, dharau, ugomvi na kejeli za aina mbalimbali hazitachangia kupatikana kwa Katiba inayotarajiwa na Watanzania.
Wamedai vitendo hivyo, vitachangia pamoja na mambo mengine kubomoa umoja na undugu uliojengeka kwa miongo mingi na vitakaribisha vitendo viouvu kama vinavyofanywa na vikundi vya Boko haramu na Alshabab.
Akizungumza kwenye mkutano mkubwa wa injili uliofanyika kwenye viwanja vya shule ya msingi Ukombozi mjini Singida, Askofu wa E.A.G.T, John Mafwimbo alisema ni wakati sasa kwa waumini wa madhehebu mbalimbali ya dini kufunga kwa ajili ya kufanya maombi kuliombea Bunge Maalum la Katiba,liweze kutekeleza yale yote waliyotumwa na Watanzania.
"Tuwaombee bila kuchoka wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba,waweze kututengenezea/kutuboreshea vizuri Katiba na wala wasituchanganye,ili sisi huku waumini wa madhehebu ya dini na Watanzania wengine wasiokuwa na dini tuje tufanye uamuzi sahihi wakati wa kuipigia kura Katiba hiyo",alifafanua.
Akifafanua zaidi, Mafwimbo, alisema kazi ya wajumbe nikuwajengea Watanzania mazingira mazuri ili waje kupigia kura Katiba itakayokidhi mahitaji yao ya zaidi ya miaka 50 ijayo.
Kwa hali hiyo, Askofu Mafwimbo amewashawishi wajumbe hao kuimarisha utamaduni wa kuvumiliana, kupendana na kumaliza tofauti zao wao kwa wao.
"Niwakumbushe tu wajumbe wetu, kwamba Watanzania ni waumini wazuri wa amani na utulivu. Kitendo hicho kimeendelea kuchangia nchi yetu kupaa kimaendeleo na wakati huo huo, sisi waumini tunaendelea kuabudu kwa uhuru mpana bila usumbufu wa aina yo yote",alisema na kuongeza kwa kusema; "Endapo hatutapata katiba stahiki,tutakuwa tunakaribisha vurugu kama zile zinazofanywa na makundi ya boko haramu".

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate