EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, August 11, 2014

MWIGULU, RIDHIWANI KIKWETE MZUKA 100%


Stori: Gladness Mallya
KWELI raha jipe mwenyewe! Usemi huo ulidhihirika wikiendi iliyopita ndani ya Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwenye Tamasha la Usiku wa Matumaini (Night of Hope) ambapo wabunge mashabiki wa Yanga walikipiga na wabunge mashabiki wa Simba na kutia fora kwa kushangiliwa wakati wa mtanange huo.
Katika mchuano huo, wabunge wa Yanga waliwagaragaza wa Simba kwa mabao 3-2 hali iliyosababisha uwanja ulipuke kwa kelele za kushangilia kutoka kwa mashabiki na wapenzi halisi wa Yanga waliokuwepo  uwanjani hapo.
Mbunge za Chalinze kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Ridhiwani Kikwete (kulia) akiwa uwanjani.
Kama vile hiyo haitoshi, baada ya kipyenga cha mwisho, wabunge wa Yanga walipanda mzuka na kuanza kuuzunguka uwanja wakisherehekea ushindi wao.
Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba akiwa na mshabiki wao mkubwa kwa upande wa Yanga.
Wabunge waliotia fora zaidi kwa kushangilia huku wakionesha hisia kali ni Mbunge za Chalinze kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Ridhiwani Kikwete ambaye baada ya ushindi huo alikimbilia kwa mashabiki wa timu hiyo na kuvua jezi yake ya juu na kuwatupia, hali hiyo iliyomfanya kubaki tumbo wazi.

Ridhiwani Kikwete akirusha T-shirt yake kwa mashabiki wa timu yake.
Naye Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba alikuwa sanjari na Ridhiwani ambapo yeye aliwarushia mashabiki wake ‘skafu’ aliyokuwa amejifunga shingoni, hali ambayo ilimfanya shabiki mmoja kuchomoka alikokuwa na kumfuata mheshimiwa huyo uwanjani na kuungana naye kushangilia.
Wakati huo, shabiki huyo alikuwa amevua shati na kuonekana kutoamini macho yake kwani kila wakati alikuwa akipiga magoti na kumshika miguu mheshimiwa huyo.
Baadhi ya wabunge wa Simba waliochezea kichapo kutoka kwa wabunge wa Yanga.
Matukio ya wabunge hao yaliwafurahisha mashabiki waliokuwa uwanjani hapo na shangwe kuwa kubwa kupindukia.
“Jamani sijui niseme nini, najiona kama naota hivi kwa sababu nampenda sana Mwigulu na leo nimemuona na nimemshika na kushangilia naye.
Nina raha sana na sijutii kuja kwenye tamasha hili,” alisikika akisema shabiki huyo.
Mwanadada kutoka Nigeria, Yemi Alade alikonga nyoyo za mashabiki wake.
Hata hivyo, hali ilikuwa tofauti kwa wabunge wa Simba ambao baada ya kipigo hicho, walianza kulalamika kuwa wamehujumiwa na refarii wa mchezo huo, Othman Kazi.
  Kwa upande wa muziki, mwanadada kutoka Nigeria, Yemi Alade aliwakonga nyoyo mashabiki na baadaye akakiri kwamba alifikiri itakuwa ni shoo ndogo, kumbe ni kubwa kiasi hicho, akaeleza jinsi alivyofurahi na kutamani kualikwa tena Tanzania.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate