BAHATI
mbaya sana, simjui huyu bwana mdogo, anayekwenda kwa jina la Nuhu
Mziwanda, aliyekuwa rafiki wa kiume wa msanii anayekimbiza katika muziki
wa mduara, Zuwena Mohamed maarufu kama Shilole.
Naambiwa naye ni msanii wa muziki wa kizazi kipya, ingawa sijawahi
kuisikia kazi yake yoyote. Lakini nikiri kuwa nimeiona picha yake mara
nyingi, akiwa na mpenziwe na hata na watu wengine. Ni kijana mtanashati
anayeweza kuwavutia wasichana wanaopenda mabrazamen!
Kwa muda mrefu, Nuhu na Shilole walikuwa wakiishi pamoja kama mtu na
mpenzi wake. Mara kadhaa, yamewahi kuibuka madai kuwa kijana huyo
alikuwa ni mdogo kiumri kwa msichana, lakini mara zote, mkali huyo wa
kibao cha Paka la Baa amekuwa akikataa.
Binafsi aliwahi kuniambia wanaosema umri mdogo wa mpenzi wake, ni
wambeya, wanamuonea wivu, kwa sababu yeye ana umri sawa na mwenzake.
Haina ubishi kwamba walipendana na ili kuwathibitishia watu hivyo, Nuhu
alijichora tatoo kwenye paja la mkono wake, akiwa ameandika maandishi
yanayosomeka Shishi Baby, jina lingine la kisanii la Shilole!
Lakini katika hali isiyotarajiwa, penzi la Shilole na Nuhu
likaparanganyika ghafla. Ni hapa ndipo ninapotaka kujikita leo
ninapozungumza na huyu bwana mdogo. Najua, umri wake bado mdogo, hivyo
kuna mambo mengi kwake ni mageni na asiyo na uzoefu nayo.
Kwa mujibu wa mashuhuda, tatoo aliyojichora Nuhu, ni ile ambayo
haiwezi kufutika, kwa maana hiyo pamoja na kupigwa kibuti, Shishi Baby
itaendelea kung’ara mkononi mwake na kila siku ataiona.
Moja kati ya
vitu ambavyo mtu anapaswa kuviogopa na kuwa na tahadhari kubwa kabisa
ni mapenzi, hasa haya ya kizazi cha sasa chenye kupenda kuiga, anasa,
utanashati na kulelewa (Shugamami na shugadadi).
Mapenzi yamesababisha wengi kuharibu maisha yao na kama mnavyojua,
watu wanauana kila siku, mke au mume anamuua mwenzake, tena wakati
mwingine, kikatili kabisa. Mapenzi ya siku hizi yanahitaji ‘timing’.
Uaminifu, siyo tu ule wa kutotoka nje ya ndoa, bali kupendana kwa dhati
ya moyo, haupo.
Watu wanapendana kulingana na upepo unavyokwenda, leo wanashibana sana, kesho chui na paka.
Hatukatai kuonyeshana mapenzi, tunawaona watu ufukweni kila siku
wameshikana viuno, wanakulana denda hadharani na wakati mwingine hata
zaidi ya hapo. Ni wakati wao, unaruhusu kwa sababu ni nyakati za furaha.
Kesho wakigombana, kukumbatiana kwao jana ufukweni hakuonekani.
Kwanza, utamaduni wa kujichora tatoo binafsi huwa siupendi kwa vile
naamini siyo wetu, ni wa kuiga. Lakini kama ni kuongeza mapambo mwilini
kwa kuwa wao ni wasanii, zipo tatoo za kujichora kwa rangi, badala ya
hizi za kutoboa mwili. Siku ikikuchosha, unaitoa.
Halafu, nadhani kama ni kujichora kuonyesha mapenzi kwa mtu, watu
pekee wenye hadhi hiyo ni watoto wako, mama au baba yako. Hawa, vyovyote
itakavyokuwa, hata mgombane vipi, bado watabaki kuwa ni damu yako.
Nasisitiza tena, kila mtu ana haki ya kupenda atakavyo, lakini jambo
moja muhimu ambalo nina uzoefu nalo, mapenzi ya enzi hizi za dotcom ni
ya upepo. Kuna machungu mengi ambayo yanawafanya watu kujutia uamuzi wao
wa kuoa au kuolewa na walionao sasa. Wakati mababu zetu walizeekea
kwenye ndoa, asilimia chache sana ya vijana wa sasa wanaoweza, angalau
kukaa miaka kumi katika ndoa.
Sidhani kama kweli Nuhu alimpenda kihivyo Shilole na kama ndivyo,
nimpe pole na kumtahadharisha asije chora tena tatoo nyingine ya
mwanamke mwilini mwake, wanaume wenzake watamcheka!
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
HABARI MBALIMBALI
‘Dk. Cheni’
‘Sharo Milionea
‘Thea’
African Women
AGNESS MASOGANGE
AK CLASSIC COSMETICS
ALI KIBA
Amanda Poshy
Ant
ANT LULU
Ashley Toto
Aunt Ezekiel
Aunty Ezekiel
AUNTY LULU
Azam Fc
Baby Madaha
BAHATI BUKUKU
Barnaba
BATULI
BBA
Beauty of the day
Belle 9
BI KIDUDE
BIBI BOMBA
Big Brother
Big Brother Africa
Bill Gates
BINTI KIZIWI
BOB JUNIOR
Bodi ya Filamu
Bongo Movie
Bongo Movies
CCM
CHADEMA
Chombezo
Christina Shusho
Chuchu hans.
Clouds Media Group
Club Bilicanas
DAR LIVE
DAVINA
Dayna Nyange
Diamond
Dida
Diva Loveness Love
Dj Ommy Crazy wa Maisha Club
DOGO JANJA
DOKI
DR.CHENI
DSTV
Dude
Dully Sykes
EBSS 2013
Elizabeth Michael
Epiq Bongo Star Search (EBSS)
ESHA BUHETI
Ester Bulaya
Feza Kessy
FIESTA 2014
Flaviana Matata
FLORA MBASHA
FLORA MVUNGI
Francis Cheka
GARDNER
GLOAL PUBLISHERS
GLOBAL TV ONLINE
H. BABA
Halima Mdee
HAMISA
Happy birthday
Hemedi
Hemedy Suleiman
HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE
Hoyce Temu
Huddah Monroe
HUSINA
IRENE PAUL
Irene Uyoya
ISABELLA
J film 4 life
Jack Chuz
JACK PATRICK
Jacob Steven ‘JB’
Jacqueline Dustan
JACQUELINE WOLPER
Jaji Khamis 'Kashi'
Jay Dee
JENNIFER KYAKA (ODAMA)
JIDE
JINI KABULA
JK
JO
Johari
Jokate Mwigelo ‘Kidot’.
JOTI
Joyce Kiria
Joyce Kiwia
JUX
K-LYNN
KADINDA
kaja
Kajala Masanja
Kapotive Star Singers
KATUNI
Kemmy
Kero Zetu
KHADIJA OMAR KOPA
KIKWETUKWETU
KILI MUSIC AWARDS
KOLETA
Lady Jay Dee
Lady Jaydee
Lake Oil
LAVEDA
Linah Sanga
Linex
Lisa Jensen
Loveness Diva
Lucy Francis Komba
Lulu
M2 The P
MABILIONEA
Madam Rita
MADELA
Magazeti
Mahusiano
Maimartha Jesse
MAINDA
MAISHA
Makala
Malkia Elizabeth
MAMTEI
MANDELA
MARIAM ISMAIL
Masanja Mkandamizaji
Mashindano ya Miss Tanzania
Matangazo
Matonya
MaxMalipo
MAYA
MELLIS EDWARD
MENINAH
MGOSI MKOLONI
Mh Halima Mdee
mic
Michezo
MILLEN HAPPINESS MAGESE
MISS CHANG'OMBE
MISS DAR CITY CENTER
Miss East Africa
MISS REDD'S IRINGA 2013
MISS TANGA 2013.
MISS TANZANIA 2014
Miss Tanzania mwaka 2011
MISS TEMEKE 2014
MISS USTAWI
MISS UTALII TANZANIA 2012/13
Miss vyuo vikuu 2013
MKALA
MREMBO HUDDAH
Mrisho Mpoto
Mrisho Ngassa
MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES.
MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013
Mtitu
muziki
Mwana FA
MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Mzee Majuto
Nancy Sumari
Nani Mtani Jembe?
NAPE
Nassoro ‘Nora’
Natasha
Nay wa Mitego
Necta
Nelly Kamwelu
NEY WA MITEGO
Nisha
NSSF;Zantel
Nyamwela
NYimbo
Nyota yako
OBAMA TANZANIA
OMMY DIMPOZ
P FUNK
PAM D
Peniel Mgilwa ‘Penny’
PETIT MAN
Profesa Jay
Q - CHILA
Q Boy
Q Chilla
QUEEN DARLEEN
RACHEL NDAUKA
RAIS KIKWETE
Rais Kikwete.
Rasimu Ya Katiba TZ
Ray
Ray C
Redd’s Miss IFM
REDD'S MISS KAGERA 2013
REDD'S MISS TZ
REDDS MISS TANZANIA 2014
Redds Miss wa Mikoa
REHEMA FABIAN
RICHIE RICHIE
Rihanna
ROSE MUHANDO
Rose Ndauka
Ruge Mutahaba.
SABASABA 2013
Saida Karoli
Saikolojia
Sajeti
SAJUKI
Sandra
SHAA
Shamsa Ford
Sheikh Ponda
Shilole
Sintah
Siwema
Skin Tricks
Snura Mushi
Spika Makinda
staa
Staa Wetu
Stella Mwangi
STYLE ZA NYWELE
Taifa Stars
Tamasha la matumaini
TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013
Tangazo
TANZANIA
TEGO
TENGENEZA WEBSITE NA BLOG
TID
Tundaman
Tupo wangapi?
TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14
Twanga Pepeta
USA PAGEANT 2014
VAI
Wastara
WEMA
WEMA SEPETU
Yanga
Yanga Bingwa 2013
YOUNG D
Yvonne Cherry ‘Monalisa’
Z Anton.
Zari
Zito kabwe
No comments:
Post a Comment