EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, August 23, 2014

TUNAITUMIA DIJITALI VIZURI?

Madenti mambo vipi?
Naona maisha yanaendelea na kwa sisi mashabiki wa soka la Ulaya, msimu wetu ndiyo umeshawadia. Hili soka la Bongo tunamuachia Malinzi na wapambe wake wazidi kuliporomosha, sisi macho yetu kule Premiership, La Liga, Bundesliga, Serie A, Ligue 1 na kadhalika.

Leo nina mada ambayo kwa kweli siwezi kuizungumzia kwamba eti enzi zetu. Labda tu niseme kwamba wakati ule sisi tukisoma, teknolojia hii ya sasa, ilikuwa ndiyo inaingia na kwa maana hiyo ilitupita.

Nazungumzia simu, kompyuta na zaidi mtandao wa Internet. Simu tulitumia zile za mezani, yaani hadi urudi nyumbani au uende posta ndipo unaweza kuwasiliana na mwenzako, lakini nao kwao wawe nayo.
Sasa nyinyi maanko mko kizazi cha Digitali, mnamiliki simu zenu za mkononi, tena basi teknolojia ikiwa imewawekea kila kitu, yaani simu lakini pia unaweza kupata internet inayokuingiza kwenye mitandao ya kijamii ambayo inapendwa sana na vijana kama Instagram, Twitter, Facebook, Viber, Tango, WhatsApp, YouTube na kadhalika.
Kwa kuwa sisi enzi zetu mambo haya hayakuwepo, siwezi kuweka ulinganisho na ilivyo leo, lakini uzoefu nilionao katika mitandao hii, unanifanya nijiulize kama tunaitumia kwa faida ya maisha yetu ya baadaye au tunafanya ili kujifurahisha tu.
Internet ina faida nyingi sana kwenu, kwa sababu unaweza kujifunza vitu vingi kama utapata mwongozo wa mwalimu kuhusu kitu chochote duniani. Sisi tulio ofisini inatusaidia sana kupata taarifa za sasa hivi zinazotokea popote. Hatupishani tena na habari kama ilivyokuwa zamani tulipolazimika kusubiri magazeti ya siku hiyo ndiyo tujue kilichotokea juzi.
Kule kwenye hiyo mitandao ya kijamii, vijana ni wengi na bila shaka wanafunzi pia mpo wa kutosha. Ninaona baadhi yao wanatupia picha wakionekana wapo bize kimasomo, ingawa inasikitisha kuona pia wengine ni kama wanajiuza flan, kwa kuanika picha zao walizopiga wakiwa nje kabisa ya mstari wa maadili.
Acha hiyo ya kujianika, lakini pia lingine linalokera ni jinsi wanavyopigana vikumbo kutafuta marafiki wenye majina makubwa. Kila mtu anataka kuwa friends na Diamond, Dimpoz, Wema, Kajala, Masanja Mkandamizaji, Kidoti, Ray na mastaa wengine kemkem.
Sikatai, ni jambo zuri kuchat na marafiki, hasa kama hawa mastaa wetu, lakini najiuliza kama hili ndilo jambo pekee tunalolifanya kupitia mitandao hii. Maana kutwa utakuta madenti wanasimuliana jinsi Chris Brown alivyomnanga Rihanna katika akaunti yake ya Twitter!
Siku hizi kuna hadi kutumiana picha kupitia simu zetu za mikononi, wenyewe mnaita WhatsApp. Utawasikia, simu yako ina wazap? Nataka nikutumie bonge la picha nipo beach jana nakula bata!
Nijaribu tu kuwashauri madenti ambao kwa vyovyote nyinyi ni baba na mama watarajiwa, kwamba huu ni wakati mzuri sana wa kujaribu kutengeneza maisha yetu ya kesho kupitia mitandao, hasa kwa mambo yanayohusu masomo.
Zamani sisi tulikuwa tunasoma kitabu kimoja kiliitwa Jiandae, chenye maswali mengi ya kila masomo tunayosoma. Sijui kama kipo siku hizi. Kitabu hiki kilikuwa kinakusanya mitihani mingi ya taifa ya darasa la saba iliyofanywa miaka ya nyuma yake, ili kumwandaa mwanafunzi kwa mtihani wake wa kumaliza elimu ya msingi.
Lakini ninavyojua mimi, hivi sasa unaweza kujifunza au kupata mitihani ya kidato cha nne ya mwaka jana kupitia internet. Ukajifua na kujifua kuusubiri mtihani wako wa kidato cha nne au sita.
Ni bahati mbaya tu kwamba muda ukipita huwa haurudi, lakini nataka niwaapie kuwa kama ndiyo ningekuwa denti sasa hivi kwa akili hizi na teknolojia hii, mngenikamatia pale kwenye kile kibao cha HAKUNA SHULE MBELE!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate