EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, October 13, 2014

MISS TANZANIA 2014 ACHA KABISA

Acha kabisa! Fainali ya lile shindano kubwa la mrembo wa Miss Tanzania 2014 limechukua nafasi usiku wa kuamkia jana, Jumapili ambapo Ijumaa Wikienda lilikuwepo ndani ya eneo la tukio kukukusanyia matukio yote yaliyojiri mbele na nyuma ya pazia hivyo lina full story.
Warembo 30 walioshiriki kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania, wakionesha shoo ya kufa mtu.
WAREMBO 30
Baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania na Mkurugenzi wa Lino International, Hashim Lundenga ‘Anko’ kukaribisha wageni waalikwa, warembo 30 walioshiriki kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania, walionesha shoo ya kufa mtu kupitia kwa msanii wa nyimbo za asili, Wanne Star.

Vanessa Mdee akifanya makamuzi jukwaani
VANESSA AFUNIKA
Kabla ya mambo mengine kuendelea, Vanessa Mdee alifunika kwa bonge la shoo alilokamua , akisindikizwa na wacheza shoo wake wawili ambao walikamua ile mbaya.
MVUTO KWENYE PICHA
Aliyeibuka kidedea kwenye kipengele hicho ni Evelyn Bassah huku Kipengele cha Top Model, mrembo Jihan Dimach akijitwalia taji.
Warembo walifanikiwa kuingia Top Five.
KIPAJI
Katika Kipengele cha Miss Talent (kipaji), taji lilikwenda kwa Nicole Sarakikya, Elizabeth Tarimo akaibuka kidedea kwenye Kipengele cha mwanamichezo mwanamke (Sports woman) huku Miss Personality ikitwaliwa na Salama Saleh.
KIFUTA JASHO
Baada ya kuenguliwa warembo 15, wale top 15 waliosalia walilamba Sh. laki saba kila mmoja kama kifuta jasho.
TOP 5
Washiriki waliofanikiwa kuingia kwenye Tano Bora ni Jihan Dimach, Siti Mtemvu, Dorice Mollel, Nasreen Abdul na Lilian Kamazima.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia shoo.
WAVALISHWA KAMA NDEGE TAUSI
Bila shaka unawajua ndege tausi hasa wale wanaoonekana pale Ikulu ya Magogoni. Warembo hao walioingia Top 5 walikuwa wamevalishwa kama ndege huyo isipokuwa rangi kwa namna walivyoonekana jukwaani.
MREMBO AMWAGA KIFARANSA
Wakati wa kipindi cha maswali na majibu, mrembo Siti Mtemvu aliwaacha watu midomo wazi aliposema atajibu kwa Kiingereza lakini baada ya kumaliza kumwaga ung’eng’e, akamalizia kwa kutema Kifaransa.
Meza ya majaji ikijipanga kutoa uamuzi wa mwisho katika kinyang'anyiro hicho.
MWINGINE ACHEMKA
Naye mrembo mwingine, Nasreen Abdul alijikuta akichemka kujibu maswali hivyo kuzomewa hasa pale alipochanganya kati ya maneno tourism (utalii) aliloulizwa na terrorism (ugaidi).
JIHAN ALA SHANGWE
Kwenye ‘segmenti’ ya maswali na majibu, mrembo Jihan alijikuta akipokea shangwe la kufa mtu kwa kujibu vizuri kwa ung’eng’e.
Siti Mtemvu (Miss Tanzania 2014 ) akiwa na anyedaiwa ni baba yake, Mbunge wa Temeke (CCM), Abbas Mtemvu.
VITUKO VYATAWALA
Vituko vilivyojiri vilikuwa vingi kwa mfano katika shoo ya msanii Vanessa Mdee aliyetumbuiza katika shindano hilo, alijikuta akiachia  ‘nido’ moja nje wakati akicheza na kuchafua hali ya utulivu, akaibua zomeazomea ya ‘weweeeee’.
nyuma ya pazia
Kituko kingine ni cha mtangazaji maarufu Bongo, Gardner G. Habash kutinga ukumbini akiwa ameongozana na kale kabinti ambako katika siku za hivi karibuni, amekuwa akionekana akiwa beneti nako bila Lady Jaydee kujua.
Ommy Dimpoz akipiga shoo katika fainali hizo
Baada ya shoo kali ya Ommy Dimpoz, washiriki walioingia fainali, walipanda tena jukwaani ambapo Mkurugenzi wa Lino International, Hashim Lundenga naye  alipanda jukwaani na kuanza kuwatangaza washindi, kuanzia namba tano mpaka namba moja.
Nasreem Abdul alishika nafasi ya tano, nafasi ya nne ikaenda kwa  Dorice Mollel.
TOP THREE
Jihan Dimach alitangazwa kuwa mshindi wa tatu (second runner up) wakati Lilian Kamazima, alishika nafasi ya pili (first runner up).
Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania na Mkurugenzi wa Lino International, Hashim Lundenga ‘Anko' (kushoto) akisimamia shoo.
Nafasi ya kwanza, ilishikwa na Siti Mtemvu, mrembo kutoka Temeke ambaye alitawazwa kuwa Miss Tanzania 2014 na kuvalishwa taji na Miss Tanzania 2013, Happiness Watimanya.
Pia Siti alijishindia shilingi milioni 18 za Kitanzania kama zawadi kwa ajili ya mshindi wa kwanza huku Lilian na akiondoka na shilingi milioni 6 za Kitanzania na Jihan akiambulia milioni 4.2.
MSHINDI ALIJULIKANA MAPEMA?
Swali kubwa ambalo wadau wengi wa mashindano ya umiss Tanzania walijiuliza usiku huo ni kwamba, je, mshindi alijulikana mapema?
Mashabiki wakipigia debe na kutoa sapoti kwa Mrembo Siti Mtemvu katika kinyang'anyiro hicho.
Viashiria vya mapema vilionesha kwamba, Siti ambaye inadaiwa ni mtoto wa Mbunge wa Temeke (CCM), Abbas Mtemvu angeibuka mshindi kutokana na jinsi alivyokuwa akishangiliwa kwa nguvu huku wapambe wake wakiinua vipeperushi vyenye picha ya mshiriki huyo, hali ambayo haikuwepo kwa wenzake.
Waandishi: Issa Mnally, Gabriel Ng’osha na Musa Mateja

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate