EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, October 13, 2014

MNIGERIA AOZA PENZI LA JOKATE

Kutoka moyoni! ‘Ubuyu’ mpya mjini ni madai ya staa wa muziki wa Nigeria, Panshak Zamani ‘Ice Prince’ kuoza akilitamani penzi la staa wa Kibongo, Jokate Mwegelo ‘Jojo’.
Staa wa muziki wa Nigeria, Panshak Zamani ‘Ice Prince’ kuoza akiwa na staa wa Kibongo, Jokate Mwegelo ‘Jojo’.
MNIGERIA ABEMBELEZA
Habari kutoka kwa vyanzo makini zilidai kwamba, Mnigeria huyo amekuwa akiwasiliana na kumbembeleza Jokate usiku na mchana akiomba wawe pamoja kwa jinsi moyo unavyomtuma.
Ilidaiwa kwamba hivi karibuni, Ice Prince anayekimbiza na ngoma yake ya I Swear amekuwa akitumbukiza vipande vya video kwenye ukurasa wake wa kijamii wa Instagram akimsifia Jokate ambaye anapendelea zaidi kumwita Kidoti.

ICE PRINCE: I MISS YOU KIDOTI!
Ilisemekana kwamba katika moja ya video hizo jamaa huyo anayefanya kazi na Jokate kwenye Runinga ya Chanel O nchini Afrika Kusuni ‘Sauz’ alisikika akimwambia mwadada huyo; ‘I miss you Kidoti’.
CHANZO CHATIRIRIKA
“Jamaa amemzimika Jokate ile mbaya. Unaambia anapiga simu na kumwita Jokate Sauz kila siku.
“Jamaa kafa kaoza. Kama unasikia mahaba niue ndiyo hayo sasa. Ishu ipo kwa Jokate tu kumkubali maana Ice Prince amekuwa akimuahidi kumpa maisha ayatakayo mtoto wa kike. Kazi anayo bidada, aamue kusuka au kunyoa,” alisema mmoja wa watu wa karibu wa Jokate.
Staa wa muziki wa Nigeria, Panshak Zamani ‘Ice Prince’
JOKATE ABANWA
Baada ya kunyetishiwa ‘mchele huo ulionyooka’ Ijumaa Wikienda, gazeti namba moja la mastaa Bongo lilimsaka Jokate ambapo aliulizwa juu ya uhusiano wake na mwanamuziki Ice Prince na iwapo anajua kuwa ana mapenzi na yeye na kama akimtamkia ndoa, je, atakubali?
Huku akionekana kushtushwa na habari hiyo, Jokate alisema kwamba iwapo Ice Prince atamwambia jambo hilo, atamchunguza tabia zake na kama zitamridhisha basi hana shaka atamkubalia.
MWANAMKE SHURTI APENDWE
Jokate alisema kwamba mwanamke kupendwa ni habari nzuri, ingawa hadi sasa bado hajaona wa kumuoa.
BOFYA HAPA KUMSIKIA KIDOTI
“Sijaona bado wa kunioa lakini kama Ice Prince ana nia, nitamchunguza kama anafaa ishallah,” alisema Jokate huku akicheka.
ATAKA MTOTO
Kwa upande mwingine staa huyo wa sinema na Bongo Fleva alisema kwa sasa matamanio yake yote anahitaji mtoto kutokana na umri wake (miaka 27) kuzidi kuyoyoma.
Staa wa Kibongo, Jokate Mwegelo ‘Jojo’.
BABA BORA MPO?
Jokate alisema kuwa kama kweli akijitokeza baba bora (husband material) atazaa haraka.
Mwanadashoti alisema kwamba, yeye kama msichana, anatamani siku moja aitwe mama na kila akikaa anapata mawazo ya kuzaa lakini anashindwa kwa sababu Mungu bado hajamjalia mume ambaye atazaa naye.
“Natamani mtoto kiukweli basi tu ni Mungu anapanga ndoa lakini akinijalia tu mimi nitazaa mapema, sitasubiri ndoa yangu ikae sana kama wanavyofanya wanandoa wengine,” alisema Jokate.
KUKUTANA CHANEL O
Jokate mwenye mipango lukuki na bidhaa za Kidoti na Ice Prince wanatarajia kukutana kwenye kipindi kipya cha Runinga ya Channel O kinachokwenda kwa jina la Top Ten Most na huko ndiko kitaeleweka.
KWENYE ‘PROFAILI’ YA JOKATE
Huko nyuma Jojo aliwahi kuhusishwa kutoka kimapenzi na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Mbongo ambaye ni staa wa Mpira wa Kikapu (NBA) nchini Marekani, Hasheem Thabeet Manka.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate