EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, November 4, 2014

WAREMBO DAR WALIVYONYONGWA


Stori: Haruni Sanchawa  na Makongoro Oging
DUNIA hii basi tena! Ni tukio la kusisimua ukilisoma mwanzo hadi mwisho lakini ni la kikatili sana! Ni lile la ndugu wawili warembo, dada na mdogo wake kukutwa wamekufa kwa kunyongwa ndani ya nyumba aliyokuwa amepanga mmoja wao huku muuaji akidaiwa alivaa taulo lenye weupe wa kufifia akitokomea zake.
Nuru Tumwaga enzi za uhai wake.
ENEO LA TUKIO
Tukio hilo la kusikitisha lilitokea hivi karibuni kwenye Mtaa wa Mji Mpya, Kata ya Azimio wilayani Temeke jijini Dar es Salaam ambapo warembo hao, Mariam Buruhani (39) na dada yake Nuru Tumwaga (42) (pichani) walikutwa wamekufa katika nyumba hiyo aliyopanga Mariam.

UWAZI LAFUATILIA
Uwazi kama lilivyo kawaida yake, baada ya kuipata taarifa za kuwepo kwa vifo hivyo vya usiku mmoja, lilianza kufuatilia hatua kwa hatua.Kwa mujibu wa ndugu mmoja, mchana wa kuelekea siku ya tukio ambayo ni Jumamosi usiku, marehemu wote walionekana wakiwa wazima wa afya ambapo Mariam alikuwa kwenye saluni yake ya kike na Nuru akiendelea na shughuli zake  za kuwaremba wanawake wenzake.
Ikadaiwa kuwa, nje ya saluni ya Mariam kulikuwa na gari dogo jeusi ambalo huwa linapaki maeneo hayo kila wakati ikisemekana mmiliki wake ni bwana wa Mariam ambaye jina halikufahamika mara moja.
Mariam Buruhani enzi za uhai wake.
GARI LAONDOKA
Ndugu huyo aliongeza: “Baadaye lile gari liliondoka na kwenda kusikojulikana, Mariam alibaki saluni.
MARIAM AFUNGA SALUNI
“Ilipofika saa moja usiku, Mariam alifunga ofisi na kwenda nyumbani kwake akiwa ameongozana na Nuru ambaye alikuja jijini Dar kwa Mariam akitokea Mtwara. Mariam ni mtoto wa mama mkubwa wa Nuru.“Baada ya kufika nyumbani, Mariam alitoka kwenda dukani kwa ajili ya kununua mahitaji ambapo alinunua juisi chupa tatu, mafuta ya taa na mahitaji mengine.”
INAVYODAIWA
Habari zaidi kutoka kwa ndugu huyo zilidai kuwa, wiki moja nyuma marehemu Mariam aliomba hati ya nyumba yake iliyoko Tandika kwa lengo la kuiuza kwa vile alipata mteja.
“Siku ya tukio, ilikuwa mteja wake afike kwa ajili ya ununuzi wa nyumba hiyo lakini kwa bahati mbaya hakufika, alikuwa na matatizo.
Wanafamilia wakiwa na nyuso za simanzi.
“Kesho yake, Jumapili saa sita mchana yule mteja alifika nyumbani kwa kaka wa marehemu aitwaye Abdallah ambapo ni jirani na alipopanga Mariam, kaka akamtuma mtoto wake kwenda kumwita shangazi yake (Mariam).“Lakini cha kushangaza, mtoto huyo alichelewa kurudi ndipo kaka mtu na watu wale waliamua kufuatilia,” alisema ndugu huyo.
MSIKIE KAKA MTU
“Tulipoona mtoto harudi tukafuata, kufika tulishtuka sana kumkuta Mariam amelala sebuleni amekufa, kuingia chumbani tukamkuta Nuru naye amelala kitandani amekufa,” alisema kaka mtu.
MAUZO YA NYUMBA YANATAJWA
Kaka wa Mariam aliendelea kusema: “Tunaamini muuaji alijua marehemu ameuza  nyumba  na pesa anazo ndani.”
VYANZO ENEO LA TUKIO.
Naye jirani na Mariam (aliomba jina lake lihifadhiwe) akizungumza na Uwazi kuhusu mazingira ya kunyongwa kwa warembo hao alisema:
Waombolezaji wakiwa msibani.
“Usiku wa tukio mimi nilichungulia dirishani baada ya kusikia mtu akitembea, nikamuona mwanaume amevaa taulo lenye weupe wa kufifia. Nilipomwangalia vizuri nikagundua ni bwana’ake da’ Mariam maana namfahamu.
“Baada ya muda nikasikia mngurumo wa gari, nikachungulia tena nje nikaliona gari ambalo ni la bwana’ke da’ Mariam likiondoka eneo hilo.“Sikujali, niliamini tuko salama. Nilipoamka asubuhi  nikawa namuona  mtu amelala sebuleni kwa Mariam, nikajua kwa vile ni Jumapili, huenda  amepumzika, sikujua ni marehemu Mariam mpaka kaka yake alipofika na watu wenegine na kubainisha kuwa, kumbe wote waliolala ndani humo walikuwa wameuawa, inauma sana.”
SERIKALI YA MTAA
Kwa upande wake Mwenyekiti wa  Serikali ya Mtaa wa Azimio, Wadudi Mlangwa akizungumza na waandishi wetu ofisini kwake alisema yeye ni kati ya viongozi wa mwanzo kufika eneo la tukio baada ya kupigiwa simu na kaka wa marehemu.
Mwili wa Nuru ukiswaliwa kwa ajili ya mazishi.
“Tulipofika tulikuta mwili wa Mariam uko sebuleni na mwili wa Nuru uko chumbani, wote wakiwa  wameaga dunia. Hapo ilikuwa saa saba na nusu mchana wa Jumapili Oktoba 26, mwaka huu,” alisema.Mwenyekiti huyo aliongeza kuwa, baada ya kuthibitisha hali hiyo aliagiza miili hiyo isiguswe  hadi  polisi  wafike kwa  hatua zaidi.
UCHUNGUZI WA  AWALI WA KIDAKTARI
Uchunguzi wa awali uliofanywa  na madaktari wa Hospitali ya Temeke jijini Dar ulibaini kuwa, marahemu hao walinyongwa kwani shingo zao zilikutwa zimepindia upande.
NINI KILIFANYIKA BAADA YA MAUAJI?
Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kuwa  baada ya mauaji hayo, chumba cha marehemu Mariam kilionekana kupekuliwa kila sehemu.  Baada ya upekuzi huo, mpekuaji alichukua redio, tivii na vitu  vingine ambavyo vinaendelea kufuatiliwa na polisi.
Mwili wa Mariam Buruhani ukiswaliwa kwa ajili ya mazishi.
MAZISHI YAO
Mariam alizikwa Jumatatu ya Oktoba 27, mwaka huu kwenye Makaburi ya Wailesi Temeke, Nuru alisafirishwa  siku hiyohiyo na kwenda kuzikwa kwao, Mtwara Jumanne ya Oktoba 28, 2014.
KAMANDA WA POLISI
Kamanda wa  Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, SACP  Kihenya wa Kihenya alithibitisha kutokea kwa  tukio hilo, “Tunamtafuta mtu aliyehusika na mauaji hayo ambaye anatajwa alivaa taulo,” alisema.
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate