Habari kutoka chanzo cha kuaminika zinasema, picha hizo ziliibwa katika simu ya msanii huyo na mtu asiyefahamika, ambaye kwa lengo lisiloeleweka, alianza kuzitawanya kwa watu mbalimbali.
Inadaiwa kuwa Amanda amekuwa akionekana
sehemu tofautitofauti jijini Dar akiwa na mzungu huyo ambaye anasemekana
kuwa na makazi yake maeneo ya Masaki.Amanda alionekana kushtushwa baada
ya kuulizwa kuhusu kuwepo kwa picha hizo na kukiri kuwa ni kweli mtu
huyo anafahamiana naye.
“Duh! hizo picha zimefikaje kwenu? Jamani haya ni maisha yangu
binafsi naombeni mniache na huyo jamaa ni rafiki yangu sana, kwanza siyo
mtanzania ni raia wa Uturuki,” alisema muigizaji huyo.
No comments:
Post a Comment