EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, December 5, 2014

MADAI MAZITO: AUNT ANASA MIMBA NJE YA NDOA

Madai mazito! Pamoja na kutumia nguvu kubwa kukanusha kwa miezi kadhaa, bado staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel Grayson, anaendelea kugandwa na madai kwamba, amenasa mimba nje ya ndoa, Ijumaa lina mkanda kamili.
Staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel akiwa viwanja na shosti yake, Wema Sepetu.
Habari hizo zilishika kasi mithili ya moto wa kifuu baada ya Aunt kunaswa Klabu ya New Maisha iliyopo Masaki jijini Dar, Jumapili iliyopita akiwa ameshiba yaani kitumbo ndi huku akishindwa kukificha baada ya kila kitu kuonekana waziwazi kwa macho yasiyohitaki miwani.

KIGAUNI CHAANIKA KILA KITU
Aunt, akiwa ukumbini humo na mastaa wenzake waliohudhuria kwenye shoo ya msanii wa Bongo Fleva aitwaye Mirrow anayesimamiwa na kampuni ya muigizaji, Wema Isaac Sepetu na Meneja Petit Man, alitinga akiwa amevaa kigauni cha drafti nyeupe na nyeusi ambacho kilionesha vilivyo tumbo lake.
WEMA ADAIWA KUMSINDIKIZA KLINIKI
Kwa mujibu wa mpenda ubuyu wetu ambaye naye alikuwemo ukumbini humo, kwa kumtazama Aunt anaonekana kuwa na ujauzito wa si chini ya miezi minne sasa na kwamba Wema ambaye ni shosti wake anadaiwa kuwa huwa anamsindikiza kliniki lakini staa huyo ameendelea kusisitiza kuwa hana.
UJAUZITO MIEZI MINNE
“Mimi najua muda mrefu na jinsi anavyoonekana kwa sasa hakuna ubishi kwani ujauzito wake una kama miezi minne hivi,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
Aunt Ezekiel akiwa na dansa wa 'Diamond', Mose Iyobo.
“Mwanamke mjamzito anajulikana kabisa. Hebu mcheki usoni alivyobadilika. Yaani kawa mweupe wakati Aunt huwa ana rangi ya chokuleti. Ukweli ni kwamba ana dalili zote za kubeba mimba.”
MAKE-UP YAMKATAA
Chanzo hicho kilizidi kuweka wazi kwamba, siku hiyo, Aunt hakuwa amechangamka kama alivyozoeleka siku zote na uso wake ulionekana kama mtu aliyechoka na hata ‘make-up’ aliyoweka haikuwa ikionekana vizuri.
NDUGU WAANZA MANENOMANENO
Habari zaidi zilidai kwamba, baadhi ya ndugu na mawifi wa staa huyo wameanza kucharuka wakidai kwamba Aunt atakuwa amepata ujauzito huo nje ya ndoa kwa kuwa muda mrefu hajaonana na mumewe, Sunday Demonte anayedaiwa kuwa gerezani huko Dubai.“Tangu mumewe apate matatizo Dubai hawajaonana hivyo Aunt hawezi kusema ni ya mumewe,” kiliendelea kudai chanzo chetu.
VITABU VYA DINI
Baadhi ya ndugu hao wametaka vitabu vya Dini ya Kiislam viweke wazi kama ni sahihi kwa Aunt kubeba ujauzito nje ya ndoa kwani kwa upande wao wanapinga kitendo hicho na kwamba ni udhalilishaji kwa ndugu yao ambaye alifuata taratibu zote za kumuoa staa huyo.
Aunt Ezekiel wakati wa kufunga ndoa.
MNENGUAJI WA DIAMOND AHUSISHWA
Sosi huyo alidai kwamba ujauzito wa Aunt unahusishwa na mnenguaji wa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Moze Iyobo ambaye kwa sasa wamegandana kama kumbikumbi wakisemekana kuwa kwenye mahaba niue.
SHEHE ANASEMAJE?
Ili kuondoa utata huku likijiridhisha kuwa Aunt anakaribia miaka miwili bila kukutana na mumewe, gazeti hili lilizungumza na Shehe Kaima wa jijini Dar ambaye analijua vizuri sakata la staa huyo ambapo alikuwa na haya ya kusema:
“Kwa kawaida mwanamke ambaye hajakutana na mumewe kwa miezi 6 au zaidi baada ya ndoa, hupaswa kwenda mara moja Baraza Kuu la Waislam Tanzania (Bakwata) kulalamika na hatimaye kudai talaka.
“Ikiwa mwanamke ameridhika na hali hiyo, naye akaamua kukaa kimya huku akifanya mambo yake na kuanzisha uhusiano na wanaume wengine maana yake amejitoa mwenyewe kwenye mamlaka ya mumewe, hivyo hapo kunakuwa hakuna ndoa tena.”
AUNT ANASEMA?
Kama alivyojitetea siku ya bethidei yake oktoba, mwaka huu baada ya kuvaa kigauni cha pinki kilichoonesha kitumbo kikianza kuchomoza, katika tukio hilo la Jumapili iliyopita, Aunt ameendelea kusisitiza kuwa ni aina ya magauni anayovaa ndiyo yanayomuonesha na kitumbo lakini hana mimba.
“Sina huo ujauzito, labda ni kwa sababu ya aina ya magauni ninayovaa,” alisema Aunt kwa kifupi.
MIAKA MIWILI ILIYOPITA
Oktoba 18, 2012, Aunt alifunga ndoa na Sunday ambapo mwigizaji huyo alibaki huku mumewe akitimkia Dubai kabla ya baadaye kupata matatizo na kutupwa jela.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate