EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, December 2, 2014

MALI ZA VIGOGO ESCROW USIPIME

HUKU moto wa upotevu wa fedha za umma katika akaunti ya Tegeta Escrow ukiwa bado unawaka kufuatia mawaziri wawili, mwanasheria mkuu wa serikali, katibu mkuu mmoja na Bodi ya Tanesco kutakiwa kuwajibishwa, mali zinazomilikiwa na vigogo waliochotewa fedha hizo usipime.
 
Moja ya ghorofa la kifahari katika maghorofa yanayomilikiwa na vigogo wa Escrow.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili kwa wanaotajwa kunufaika na fedha hizo, unaonyesha kuwa, pamoja na mambo mengine, wanamiliki majumba makubwa ya kifahari, yakiwemo maghorofa katika maeneo mbalimbali ya mikoa, ikiwemo Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya na Morogoro.
Mmoja wa wanaotajwa (jina linahifadhiwa kwa sasa) ana jumba kubwa la ghorofa mbili sehemu za Mbezi Beach, Dar, ambalo licha ya kuwa ya thamani kubwa, pia ukubwa wa eneo analomiliki, umemfanya pia kujenga bwawa kubwa la kuogelea.

“Aina ya maisha anayoishi huwezi kusema kama ni Mtanzania, kwa sababu haonyeshi kama anajua uwepo wa shida, kwa sababu watoto wake wote wanasoma nje ya nchi na zipo likizo ambazo hawarudi kwa vile wanasafiri nchi tofauti na wanazosoma kwa ajili ya matembezi tu.
“Acha hii nyumba, ana ghorofa pale Kariakoo lote limepangishwa na magari anayoendesha huyu bwana ni hatari. Nafikiri gari la thamani ndogo kabisa ni BMW analoendesha mkewe. Kuna watu wana fedha hadi wanaudhi aiseee,” alisema mkazi mmoja wa Mbezi Beach, anayedai kuishi jirani na mfanyabiashara huyo aliyenufaika na fedha za Escrow.
 
Muonekano wa juu wa ghorofa hiyo.
Kigogo mwingine mwenye asili ya Mwanza, anadaiwa kununua jengo lenye ghorofa nne lililopo katikati ya Jiji la Mwanza na limeshaanza kufanyiwa marekebisho, kwani ana lengo la kuifanya hoteli.
Wakati ikiwa bado haijafahamika kama watu hao walionufaika na fedha hizo mali zao watafilisiwa au la, habari zinasema baadhi ya waliochotewa, wamekuwa na maisha ya kufuru, kutokana na matumizi ya kutisha ya fedha wanayofanya, huku wakinunua vitu mbalimbali vya thamani.
Hata hivyo, wakati watu hao wachache wakiwa wamegawana kiasi cha shilingi bilioni 306, idadi kubwa ya Watanzania wanaishi maisha ya umaskini mkubwa, kiasi cha kula mlo mmoja kwa siku, huku wakikosa huduma muhimu kama maji safi na salama ya kunywa, huduma bora za afya na elimu.
Mamia ya vituo vya afya vinavyomilikiwa na serikali huko vijijini havina dawa, hasa kipindi hiki ambacho serikali inadaiwa kiasi cha shilingi bilioni 90 na Bohari Kuu ya Madawa (MSD). Kutokana na kukosekana kwa dawa, Watanzania wengi hufariki dunia kwani zahanati nyingi zina dawa ndogondogo kama panado za kutuliza maumivu tu.
 
Muonekano wa ndani wa ghorofa hiyo.
“Wakati wengine wanakufa kwa kukosa dawa, shule zikiwa hazina vifaa vya kufundishia na uhakika wa kula ukiwa mdogo, Watanzania wengine wanaishi kifalme, wanapata kila kitu wanachotaka, wanakwenda popote wanapotaka, wanatibiwa hospitali wanazotaka. Bora maisha wanayoishi yangekuwa kwa sababu ya fedha halali, lakini hizi za wizi ni hatari sana,” alisema mwanaharakati mmoja, aliyejitaja kwa jina moja la Nando.
Wiki iliyopita, Bunge lilitoa maazimio nane yanayotakiwa kutekelezwa na serikali, ikiwa ni pamoja na kupendekeza mamlaka ya uteuzi kuwavua nyadhifa zao Mawaziri Sospeter Muhongo na Anna Tibaijuka, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Frederick Werema, Katibu Mkuu wa Nishati na Madini, Eliakim Maswi pamoja na kuvunjwa kwa Bodi ya Shirika la Ugavi wa Umeme (Tanesco).
Bunge hilo pia, lilimjadili Singasinga Harbinder Sigh Seth (pichani) ambaye inadaiwa ndiye kinara wa dili hilo.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate