EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, December 2, 2014

AMUUA MKE KWA WIVU WA MAPENZI

Shangwe Thani, Shinyanga UKATILI! Mwanamke mmoja, Regina Salago (24) (pichani) ameuawa kinyama kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na kuvunjwavunjwa shingo na mikono na mume wake, Kishimba Keya, kutokana na wivu wa kimapenzi.

Regina Salago enzi za uhai wake.
Tukio hilo la kinyama, limetokea hivi karibuni katika Kijiji cha Maganzo, Kata ya Songwa wilayani Kishapu, Shinyanga.Akizungumza na gazeti hili kuhusu tukio hilo, mama mzazi wa Regina aliyejitambulisha kwa jina la Catherine Kondo (45) alisema siku mbili kabla ya kifo, binti yake huyo alikuwa amerudi nyumbani kutoka kwa mumewe kwa nia ya kuachana naye.

‘’Siku aliyorudi mwanangu aliniambia amechoshwa na vitendo vya wivu wa kupita kiasi anavyofanyiwa na mume wake, ameona bora arudi nyumbani aanze upya maisha akiwa huru hata kama ni ya shida,’’ alisema mama huyo.
Aliongeza kuwa Regina alishinda siku mbili tu nyumbani hapo ndipo mume wake alimfuata na kumbembeleza kuwa waondoe tofauti zao na kwamba alikuwa amejirekebisha.
“Regina alikataa katakata kurudi kwa mwanaume huyo kutokana na vitendo vya kikatili na unyanyasaji alivyokuwa akifanyiwa kiasi cha kukosekana kwa amani kwa kusingiziwa alikuwa akitembea nje ya ndoa yao,” alisema Catherine.
Kufuatia hali hiyo mwanaume aliamua kubadili msimamo na kumpa shilingi 40,000 Regina kama kumuomba msamaha akashawika kuondoka naye kurudi kwao.Habari zinadai walipofika kwao alimshambulia kwa kumpiga na springi ya gari na kuivunja mikono na shingo kwa kutumia chuma hicho kizito.
Baada ya kumuua, Kishimba alimpigia simu mama mkwe wake mara kadhaa akimhimiza aende nyumbani haraka kwa kuwa mtoto wake Monica (mdogo wa Regina) alikuwa mgonjwa mahututi.Aliporudi nyumbani alianza kumtafuta Regina na alipokwenda kwa mumewe alimkuta akiwa amelala kifudifudi na damu ikiwa imetapakaa mwili mzima, akiwa amekata roho.
Mama huyo aliongeza kuwa, kufuatia tukio hilo alipiga mayowe ya kuomba msaada kwa majirani na baadaye polisi waliitwa eneo la tukio.Mama huyo alisema kuwa muuaji alifanikiwa kutoroka na kuwaacha watoto wake wawili, Frank (5) na Minza (3) aliozaa na marehemu.
Kamanda wa Polisi mkoani Shinyanga, SACP Justus Kumugisha amethibitisha kutokea kwa tukio hilo. “Sasa hivi tunamtafuta muuaji ili aweze kufikishwa mahakamani,” alisema Kamanda Kamugisha.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate