EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, December 20, 2014

MPAMBE WA MGOMBEA URAIS AVISHWA SHANGA


Stori: Richard Bukos na Issa Mnally JAMAA anayedaiwa kwamba ni mpambe mkubwa wa mmoja wa wagombea urais mwakani ambaye ni fundi wa kufunga madishi, mkazi wa Magomeni-Makanya jijini Dar es Salaam, almaarufu Mgosingwa, amejikuta akivishwa shanga baada ya kunaswa na mke wa mtu chumbani kwake.
Mgosingwa akivishwa shanga baada ya kufumaniwa na mke wa mtu.
FUMANIZI
Tukio hilo la aina yake la kufungia mwaka 2014 lilijiri kwenye fumanizi la jamaa huyo lililochukua nafasi nyumbani kwake maeneo ya Magomeni-Makanya, Dar, Jumanne iliyopita ambapo alifumwa na mke wa jamaa aliyejitambulisha kwa jina moja la Faki aitwaye Mwanahamisi akidaiwa kumrubuni kwa nguo za Sikukuu ya Krismasi.


Kwa mujibu wa mwenye mke, baada ya Mgosingwa ambaye mkewe alikuwa safarini, kunaswa laivu alitaka kuchoropoka kupitia dirishani lakini jamaa alimkamata miguu na kumrudisha ndani.
OFM
Kama kawa, makamanda wa Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publisher wanaotumia bodaboda ziendazo kasi, walitonywa na kufanikiwa kufika eneo la tukio ndani ya dakika sifuri.

...Akiwasihi wamuachie baada ya kufumaniwa.
OFM walipofika walikuta mtiti umeshika kasi ambapo kabla ya kufikia hatua ya kudhuriana, polisi waliokuwa doria mtaani waliitwa na wasamaria wema na kwenda kuokoa jahazi.
AVISHWA SHANGA
Polisi walipofika walimkuta mwenye mke akiwa na shanga mkononi akimvalisha Mgosingwa ambaye tayari hakuwa na ujanja.Hata hivyo, polisi hao walifanya kazi ya ziada kumdhibiti mwenye mke ambaye alikuwa akipambana nao akitaka aachiwe apambane na mgoni baada ya kumvisha shanga.

MAYOWE
“Niacheni jamani lazima na mimi leo nim….(tusi), haiwekani kabisa mtu atake kumdhalilisha mke wangu.
“Mke wangu nitajua cha kumfanya tukifika nyumbani, yaani ukweli nampenda sana mke wangu,” alisikika mwenye mke akipiga mayowe.

Dk. Wilbrod Slaa,
WAAMRISHWA WAVAE NGUO
Tukio hilo lilisababisha mjumbe wa nyumba kumi wa eneo hilo aliyejitambulisha kwa jina la Mama Vicky na Afisa Mtendaji wa Mtaa wa Makanya (hakutaja jina) wafike eneo hilo na kuwaamrisha waliofumaniwa wavae nguo kwanza.

SERIKALI YA MTAA
Baada ya kuvaa, wahusika wote walipelekwa kwenye ofisi ya mtendaji wa mtaa huo ili wazungumze na ikiwezekana wayamalize kwani wahusika hao walikuwa ‘hawajaduu’ bado.

January Makamba.
MSAMAHA
Baada ya kufika ofisi ya mtendaji, Mgosingwa alimpigia magoti mwenye mke na kumuomba msamaha huku akikiri kuwa alikuwa akitaka kula tunda la mkewe lakini alikuwa bado hajathubutu kufanya hivyo hata siku moja.

“Chondechonde kaka, mimi ni mwanaume mwenzako na wote, mimi, wewe na mkeo tunatoka pamoja pale Makorora (Tanga) na familia zetu zinajuana fika.“Naomba unisamehe ndugu yangu niko tayari kukulipa fidia ya kunishika ugoni,” aliomba Mgosingwa.
Mgosingwa aliendelea kuomba radhi ambapo mjumbe wa nyumba kumi na afisa mtendaji walimshauri mwenye mke kupunguza jazba kisha akubali kuzungumza na mgoni wake, wasifike mbali na kuyamaliza ili kuepusha usumbufu.
Benard Membe.
FAINI MIL. 1.5
Baada ya kushauriwa kwa muda mrefu, mwenye mke aliiheshimu mamlaka hiyo ya serikali na kukubali kulipwa faini shilingi milioni moja na nusu za Kitanzania ili kumsamehe mgoni na kumpa onyo kali endapo wataendeleza kamchezo hako.Baada ya hapo, Mgosingwa aliendelea kuwapigia simu ndugu zake wamtumie fedha kwenye simu ili amalize tatizo hilo.

NI MPAMBE WA MGOMBEA GANI?
Kwa mujibu wa majirani wa Mgosingwa ni mpambe wa mmoja wa wanasiasa maarufu anayedaiwa kuwa kwenye ‘resi’ za kugombea urais mwakani, kufumaniwa kwake kumetajwa pia kama ni njia mojawapo ya kumchafua mgombea huyo.Mgosingwa alipoulizwa kama ni mpambe wa mgombea gani hakuwa tayari kutaja.

Waziri mkuu Mizengo Pinda.
WANAOTAJWA URAIS 2015
Baadhi ya vigogo wanaotajwa kutaka kugombea urais kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 ambao wana wapambe kila kona Bongo ni pamoja na Mizengo Pinda, Benard Membe, January Makamba, Frederick Sumaye, Dk. Khamis Kigwangala, Dk. Wilbrod Slaa, Wiliam Ngeleja, Steven Wasira, Dk. Mohamed Shein, Dk. Emmanuel Nchimbi, Dk. Asha-Rose Migiro na Edward Lowassa.

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate