EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, December 30, 2014

WAIMBA INJILI WANA NINI?


 
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
MENGI yameibuka kufuatia waimba Injili Bongo kukumbwa na kashfa mbalimbali zikiwemo ndoa zao kuvunjika, madai ya kuchepuka, kupata ujauzito nje ya ndoa na matumizi ya madawa ya kulevya, Uwazi limechimba na kuchimbua.
Janet Mreme akiwa na mume wake Jonas Mrema.
BADO JINAMIZI LA KUVUNJA NDOA LAWAANDAMA
Mpaka sasa, waimba Injili wanawake wameshakumbwa na mikasa mbalimbali lakini mpya kabisa ni madai ya hivi karibuni kwamba, ndoa ya mwimbaji mwingine, Kabula George imesambaratika.
Kabula George mwaka 2012 alitamba na Albamu ya Nitang’ara Tu! Inadaiwa hayuko kwa mumewe baada ya ndoa yao kudumu kwa miaka nane!

JANET MREMA ANAUMWA
Huyu aliwahi kuripotiwa na Gazeti la Amani miezi miwili iliyopita kwamba, ndoa yake na mumewe, Jonas Mrema imesambaratika madai makubwa ni mume kutomwamini mkewe huyo na kudai alitoroshwa nyumbani na mchungaji mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) aliyejulikana kwa jina moja la Emmanuel.
Bahati Bukuku.
Habari mpya ni kwamba kwa sasa hali yake ni tete, anaumwa lakini wengi wanaamini ugonjwa wake unatokana na mawazo ya kuchanika kwa ndoa yake.Tayari mwanaume huyo ameshafungua kesi Mahakama ya Kinondoni, Dar akimlalamikia Mchungaji Emmanuel kumtoroshea mkewe. Anataka fidia ya pesa ambazo mahakama itaamua kama itaona ni sahihi.
BAHATI BUKUKU
Huyu ni mwimba Injili mkongwe Bongo. Ndoa yake na Daniel Basila ilivunjika mwaka 2005, mume alimtuhumu Bahati kutoroshwa nyumbani na mzungu mmoja ambaye hakumtaja jina.
Baadaye Bahati alikanusha, akasema aliamua kuondoka nyumbani kwa Daniel kutokana na manyanyaso mengi. Alishindwa kuvumilia. Mpaka sasa, Bahati hayuko kwenye ndoa.
Rose Mhando.
NEEMA MWAIPOPO
Alipovuma sana na wimbo wa Sipati Picha alikuwa akijulikana kwa jina la Neema Mushi. Mumewe ndiye Mushi. Baadaye, ndoa yake ilivunjika, akarudia jina la ukoo wake, Mwaipopo. Akatoa albamu inaitwa Raha Jipe Mwenyewe.


ROSE MHANDO
Rose Mhando ndiyo anavyojulikana na wengi. Jina la baba yake ni Athuman. Familia yake yote ni ya Kiislam.

Majanga yake makubwa ni kuzaa watoto watatu pasipokuwa na ndoa. Lakini kwa sasa ana mimba tena, ina maana ni ya mtoto wa nne! Ilishawahi kuandikwa kuwa, kila mtoto ana baba yake!
Lakini pia, Rose aliwahi kudaiwa kubwia ‘unga’ hali inayosemekana kumpotezea utendaji wa huduma.

Flora Mbasha.
FLORA MBASHA
Huduma yake kwa sasa ni kama imesimama baada ya ndoa yake na mumewe, Emmanuel Mbasha kuparaganyika!Kwa sasa, Flora yuko mahakamani akimdai talaka mumewe huyo kwa madai kwamba, kwa kipindi chote cha ndoa yao, alikuwa mtu wa kupigwa mara kwa mara!

CHRISTINA SHUSHO!
Na yeye ni mwimba Injili maarufu. Kwa miaka ya hivi karibuni ni kama amezimika! Ilidaiwa naye ndoa yake ina misukosuko ya mara kwa mara. Uwazi liliwahi kumfuata nyumbani kwake, Tabata-Chang’ombe, Dar ili kuujua ukweli wa ndoa yake kukumbwa na upepo wa kisulisuli, msichana wa kazi aliyefungua geti alisema:
“Dada yupo kwenye kikao cha usuluhishi, kuna mchungaji kaja.”

Christina Shusho.
Sarah Mvungi
Ni muimba Injili aliyetokea kwenye fani ya maigizo. ana watoto wawili, kila mmoja ana baba yake. Hana ndoa lakini anatoa huduma ya Neno la Mungu kwa njia ya uimbaji.

JENNIFER MGENDI
Huyu kidogo Uwazi limepekua maisha yake na kubaini kwamba, yemejaa uadilifu. Ndoa yake haikuwahi kudaiwa kukumbwa na kimbunga cha kusambaratika wala kutengana.Jennifer Mgendi.
MCHUNGAJI ATOA NENO
Mchungaji mmoja wa Kanisa la Evangelical Asemblies of God Tanzania (EAGT) ambaye hakupenda jina lake litajwe gazetini alisema:“Nawaomba hao waimbaji wa kike, hasa wanaodai talaka au walioshindwa kuvumilia maisha ya kwenye ndoa wasome maandiko, mbona yako wazi sana.

“Mimi natabiri kwamba, muziki wa Injili unaporomoka na utazidi kuporomoka kwani shetani amefanikiwa kuwashika waimbaji kwa kusambaratisha ndoa zao kwanza ili washindwe kutoa huduma ya kiroho, maana utahubirije Neno la Mungu wakati wewe linakushinda kulitekeleza?”
KUNA NINI KWENYE INJILI?
Ni swali la kujiuliza sana, ni kwa nini maisha ya waimba Injili, hususan wanawake yako hivi? Mtu anayetoa huduma ya kiroho anapofikia hatua ya kusema ‘ameshindwa kuvumilia’ inakuaje kwa asiyejua maandiko?

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate