EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, January 23, 2015

RUSHWA YA NGONO YAMNASA KANJIBAI

Hii ni tuhuma nzito! Katika hali inayoonesha maadili Bongo yanagaragazwa kwa kiwango cha kutisha, mapema wiki hii jamaa mmoja mfanyabiashara mwenye asili ya Kihindi almaarufu Kanjibai au Ponjoro, alinaswa kitandani akiwa mtupu na mwanamke aitwaye Hidaya ambaye ni mke wa mtu, akidaiwa kudai rushwa ya ngono ili ampe ajira.
Kanjibai akiwa mpole baada ya kufumaniwa.
OFM YATONYWA
Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers, ikiwa kwenye ‘mingo’ zake ilipewa ‘ubuyu’ na vyanzo vyake kwamba ifike katika nyumba moja iliyopo Tandale jijini Dar es Salaam kwani kulikuwa na zoezi la ufichuaji wa maovu.
MAOMBI YA KAZI
Kabla ya tukio hilo, ilidaiwa kwamba hivi karibuni Kanjibai na Hidaya walikutana maeneo ya Kariakoo jijini Dar ambapo mwanamke huyo alikwenda kutafuta kazi.

Ilidaiwa kuwa baada ya kusalimiana mazungumzo mengine yaliendelea huku jamaa huyo akitaka mambo matamu-matamu ya chumbani kwa ahadi ya ajira:
“Kazi kwishapata lakini lete ile kachori (rushwa ya ngono), mimi patia kazi wewe, sawasawa?”

...Akiomba kuachiwa baada ya fumaniza hilo.
KANJIBAI ATUMA VIMESEJI VITAMU
Ilidaiwa kwamba baada ya wawili hao kuagana, Kanjibai alianza kumchombeza Hidaya kwa ‘vijimeseji’ vitamu-vitamu kupitia mitandao ya simu za mkononi hasa hizi za kisasa za kuteleza ‘smart phones’.
Iliendelea kudaiwa kwamba siku ya siku, wakiwa nyumbani kwao maeneo hayo ya Tandale, Dar, mume wa Hidaya aligundua mchezo huo mchafu baada ya kunasa mawasiliano haramu kati ya Kanjibai na mkewe ambapo alianza kumbana ‘maiwaifu’ wake ampe ushirikiano wamshike ugoni.
UTETEZI
Ilidaiwa kwamba, katika utetezi wake, mwanamke huyo alimwambia mumewe kuwa jamaa huyo alikuwa akitaka mapenzi ili ampatie ajira kwenye kampuni moja iliyopo Kariakoo, Dar.
MTEGO WAANDALIWA
Baada ya kukubaliana, mume na mke waliandaa mtego ambapo Hidaya alimwelekeza Kanjibai anakoishi Tandale.Ilielezwa kwamba, Kanjibai, bila kujua kinachoendelea huku akiomba maelekezo katika kila hatua, alifanikiwa kufika kwa wanandoa hao na kuzama ndani.Ikasemekana kwamba, jamaa huyo alipotimba ndani alikaribishwa chumbani ambapo hakuchukua muda, akasaula nguo zote na kubaki mtupu akiwa tayari kutekeleza uzinzi.

BONGE LA FUMANIZI
Baada ya Hidaya kutoa ishara kwa mumewe kuwa mambo ‘yameiva’, OFM wakatonywa ambapo bila kuchelewa, kama kawaida yake, mkuu wa zamu aliwaagiza vijana wake ambao walitoka mkuku kwa kutumia pikipiki ziendazo kasi kuelekea eneo la tukio.
OFM ilipofika eneo la tukio ilikuta bonge la sekeseke la fumanizi likiendelea huku Kanjibai akiwa mtupu kitandani, chumbani kwa wanandoa hao akiomba msamaha kwa kutumia Kiswahili cha ‘makabachori’ huku akiahidi kutorudia mchezo huo mchafu.
KISWAHILI MBOVUMBOVU
“Iko samehe mimi bana, pana jua hii kama mke ya mtu, iko najua ishi peke yake, hapana ambiya mimi kama olewa, samehe mimi ngoja ita kaka yangu jua vizuri Kiswahili ongea na wewe lakini hapana peleka mimi polisi, iko ogopa sana pelekwa Segerea,” alisikika Kanjibai akijitetea huku akimuomba mume wa mwanamke huyo pamoja na ndugu zake wamsamehe na wasimpeleke polisi kwani anaogopa kupelekwa Gereza la Segerea jijini Dar.
MKONO WA SHERIA
Hadi OFM inaanua virago eneo la tukio, mume, mke na wapambe walikuwa katika taratibu za kufuata hatua zinazostahili ili kumfikisha Kanjibai kwenye mkono wa sheria.
ONYO
Ijumaa linatoa onyo kwa vitendo viovu vya ngono na kushauri wote wanaohitaji wenza kufuata taratibu zinazostahili ili kupunguza kasi ya mafumanizi, maradhi na migogoro mbalimbali katika jamii la sivyo OFM ipo kazini kila sehemu, kila saa kuwaumbua. - Mhariri.
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate