EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, February 25, 2015

STRESS HAZIPUNGUZWI KWA KUCHEPUKA!

LABDA haijawahi kukukuta, lakini maisha tunayoishi katika wakati wa sasa yanasababisha watu wengi wanapatwa na msongo wa mawazo, maarufu kama stress. Hali ni mbaya kwa wafanyakazi wenye mabosi wakorofi na hata wafanyabiashara wanaoyumba kiuchumi.
Lakini inakuwa mbaya zaidi mambo yanapoharibika ndani ya familia, kwa maana ya wanandoa au walio katika uhusiano wa kimapenzi. Ingawa sina takwimu kamili, lakini uzoefu unaonyesha tafrani katika ndoa zinasababisha watu wengi sana kuchanganyikiwa na hata kusababisha kukosa amani ndani ya mioyo yao.
Na siyo kukosa amani na kuchanganyikiwa tu, wengi pia wamepoteza maisha baada ya kushindwa kuhimili mikanganyiko iliyotokea. Mtu anaona mwenzake anakwenda ndivyo sivyo katika uhusiano wake anaamua kujimaliza mwenyewe, achilia mbali wanaoamua kujimaliza wote ili kila mmoja akose.

Ukiachana na hawa wanaokosa uvumilivu, kuna wale ambao badala ya kufanya vitu kama hivyo, wao huamua ‘kuchepuka’ ili kupunguza stress zinazotokana na mikwaruzo katika familia. Yaani ili mama aondoe ‘hasira’ za baba kumzingua jana yake, anachofanya ni kumkumbuka mtu wake wa zamani, mume wa mpangaji mwenzake aliyemkonyeza jana, jirani yao nyumba ya pili au hata kiserengeti boy chake na kwenda kuburudika nacho.
Anafanya hivi kwa akili zake akiamini kuwa anajisahaulisha machungu au kama wengi wanavyochukulia kuwa wanawakomoa wenza wao. Wachepukaji wenzao wakiwauliza vipi kuhusu waume zao, ni rahisi kuwabeza na kuwadharau!
Hali kadhalika akina baba nao baada ya kushindwa kuelewana na wake zao, kinachofuata ni kuangalia katika orodha ya walio katika simu na kumkumbuka Mwajuma Ndala Moja, jirani anayejigonga kila siku, mfanyakazi mwenzake ofisini au hata dada wa dukani anayemchekeaga akienda kupata mahitaji.
Akienda huko, hata anaochepuka nao wanapojaribu kujifanya kumuogopa mkewe au rafiki yake, ni rahisi kukutana na majibu kama haya; “achana naye mjinga huyo, wewe tulia kula maisha” au “Anajifanya anajua wakati anaungua na jua, achana naye.”
Lakini unapojaribu kuangalia suala hili, unajikuta unagundua kwamba hakuna yeyote kati yao ambaye kwa kweli anaondoa stress zaidi ya kuongeza matatizo. Utakwenda nje, sawa, lakini kumbuka huendi kule baada ya kumbusu na kumdanganya mwenzio, bali unakwenda ukiwa umenuna na hutaki hata kuaga unakoenda.
Matokeo ya uchepukaji wa namna hii ni kukosa uangalifu na umakini katika ufanyaji wa tendo, kitu ambacho kinaweza kuleta athari, siyo tu kwa mhusika, bali hata kwa mtu wake aliyemuacha nyumbani.
Ukiachana na athari za kiafya kwa mfano, lakini hata lugha ya dharau kwa mwenza wako unayoitoa, nayo inaweza kuleta madhara kwa upande wa pili kwa sababu tayari watu wa nje wanatambua udhaifu uliopo ndani mwenu. Yule jirani uliyechepuka naye atatangaza kwa marafiki zake juu ya ugomvi wenu na jinsi ulivyomdharau mume au mke wako.
Hiyo itasaidia kuzidi kumdharaulisha mume au mke wako mtaani kwenu kwa sababu watu watamuona mwenzako kama mtu rahisi na asiye na maana. Kitu cha msingi unachopaswa kufanya kila inapotokea kutoelewana ndani ya nyumba au uhusiano wenu, unatakiwa kuwa mtulivu kiakili kuliko wakati mwingine wowote.
Kumbuka, huu ni wakati unaoweza kufanya kosa linaloonekana dogo, lakini likakupa madhara makubwa. Unapohitaji kupata muda wa kujiuliza, basi usiweke mambo ya ngono akilini mwako. Tafuta mtu unayemuamini na kumwelewa, mshirikishe tatizo lako. Faida ya kumshirikisha mwingine katika tatizo lako ni zuri kwa kuwa mawazo mawili matatu tofauti kutoka vichwa tofauti yatakupa mwanga wa kujua nini cha kufanya ili kukabiliana na kilicho mbele yako.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate