EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, March 3, 2015

KIGOGO BANDARI AOZESHWA MAITI

Na Haruni Sanchawa/Uwazi
Kigogo mmoja wa Mamlaka ya Bandari Tanzania, kitengo cha kupakua makontena (TICS) jijini Dar, James Wambura, hivi karibuni alipata wakati mgumu kufuatia mwanamke aliyejulikana kwa jina la Margaret, aliyeishi naye kwa miaka mingi bila kufunga naye ndoa, kufariki dunia na ndugu kumgomea kuzika wakisema si mkewe mpaka alipe mahari, Uwazi limeipata nzima.


Marehemu Magreth enzi za uhai wake.
Margaret (pichani) alifariki dunia Februari 21, mwaka huu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar na kuzikwa Februari 26, 2015 kwenye Makaburi ya Kitunda Machimbo, Ilala jijini Dar huku kifo chake kikidaiwa kilitokana na kunywa sumu!
MKASA KAMILI
Ilidaiwa kuwa, Wambura na marehemu waliishi kwa miaka mingi na kujaliwa kupata watoto wawili ambao ni wakubwa lakini hakuwa amefunga ndoa na mwanamke huyo, hivyo kumwondolea sifa ya maamuzi ya wapi akamzike marehemu huyo.
“Ilikuwa siku ya mazishi pale Kitunda nyumbani kwa Wambura, ndugu wa marehemu wakasema wapi akazikwe ndugu yao ni uamuzi wao, kwa vile mwanaume huyo hakuwa ametoa mahari kwa familia ya marehemu, hivyo hakuwa mkewe.”
Mwili wa marehemu ukiombewa kwa ajili ya mazishi.
SHARTI NI MOJA TU
Ikazidi kudaiwa kuwa, mwanaume huyo aliambiwa kuwa, endapo atalipa mahari ataruhusiwa kumzika mama watoto wake huyo kwani atakuwa ameshaozeshwa kihalali.“Kuna ndugu mmoja alisema hata kwenye vitabu vya dini, imeandikwa mwanaume akishalipa mahari anakuwa ameshaoa mke, haya mambo ya sherehe ni siku hizi tu, lakini zamani haikuwa hivyo, mahari ilihesabika ni ndoa kamili,” kilisema chanzo chetu.
Kikaongeza kuwa, ilibidi Wambura akubali kulipa mahari na faini ambapo alitajiwa shilingi milioni tano (5,000,000), lakini baada ya ‘kulia hali’ aliambiwa atoe shilingi milioni mbili (2,000,000), akafanya hivyo.
Watoto wa marehemu wakiwa na simanzi kubwa.
KUNYWA SUMU HADI KIFO CHAKE
Marehemu Margaret alidaiwa kunywa sumu, Februari 15, mwaka huu katika kile kinachodaiwa kuwa ni kuchoshwa na hali ambayo haikuwekwa wazi. Alikimbizwa Zahanati ya Mission iliyopo Kitunda, Dar es Salaam ambako alipatiwa matibabu.
Hali yake ilipozidi kuwa mbaya, alihamishiwa Hospitali ya Dar Group, Dar  ambako pia haikutengemaa na kupelekwa Muhimbili ambako jioni ya Februari 21, mwaka huu, alifariki dunia.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate