EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, March 3, 2015

MUME ALIVYOMCHOMA KISU HAWARA


Richard Bukos na Makongoro Oging’/Uwazi
Habari zilizolitikisa Jiji la Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita ni pamoja na ile ya mkazi wa Chamazi, Hussein Mfaume, kumchoma visu hawara yake,  Ester Thomas Ungele (30), naye kujichoma mpaka kujitoa utumbo, Uwazi limeichimba kwa kina.
Hawara akipelekwa hospitali baada ya kuchomwa kisi.
Habari zilidai kuwa, kisa hasa cha mwanaume huyo kujichukulia uamuzi huo wa kikatili ni madai ya  mwanamke huyo  kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanaume mwingine anayedaiwa kuwa ni dereva wa teksi.

MANENO YA SHUHUDA MKUU
Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio  hilo ambaye ni mtoto wa Ester, Sarah siku hiyo, yeye na mama yake  walikuwa kwenye eneo lao la biashara ya Mama Lishe, nje ya  Ukumbi wa Vijana, Amana uliopo Ilala, Dar.
“Ghafla nilimwona Hussein akija huku usoni akionekana mtu mwenye hasira. Alimfuata mama alipokuwa na kumuuliza ni kwa nini anamfanyia dharau?”
Mume akiwa taabani baada ya kujichoma kisu.
MALUMBANO YAANZA, WAKIMBIZANA
Sarah anaendelea: “Niliona kama malumbano ya kawaida nikawa nawaangalia lakini nikashangaa kumuona Hussein akimsogelea mama na kutoa kisu.“Mama alianza kukimbia naye Hussein akamkimbiza huku bado ameshika kisu mkononi. Niliogopa sana, nikatetemeka. Nilipiga mayowe kumuombea msaada mama.
“Mama alikimbia uelekeo wa kuingia kwenye Ukumbi wa Vijana lakini kabla hajafika, Hussein alimchota mtama mama akaanguka. Ndipo Hussein alipoanza kumchoma visu mama sehemu mbalimbali za mwili na kisha kumkita nacho kichwani.”
KISU MWILINI MWAKE
Sarah tena: “Baada ya kumchoma mama visu hivyo, nilishangaa kumuona Hussein na yeye akijichoma visu sehemu mbalimbali za mwili wake lakini mwisho alijikita nacho tumboni na kuanza kukitikisa kama vile alikuwa anauchanachana utumbo wake, akaishiwa nguvu na kuanguka. Ndipo wasamaria wema wakaanza kuwasogelea.”
Sarah alisema hata yeye alisogea eneo hilo na kuwakuta wote wamepoteza fahamu huku utumbo wa mwanume ukiwa nje na damu chapachapa ikiwa imetapakaa mwilini. Wakachukuliwa na kukimbizwa Hospitali ya Mkoa wa Ilala, Amana, Dar ambapo ni mita chache tu kutoka eneo la tukio.
MKE WA HUSSEIN SASA
Naye mke wa mtuhumiwa huyo aliyejitambulisha kwa jina la Zubeda Abeid alipopata nafasi ya kuzungumza na Uwazi alikuwa na ya kusema:“Ukweli taarifa hizi nimezipata kwa mshtuko mkubwa sana hali iliyonifanya nipoteze fahamu. Hussein ni mume wangu wa ndoa, alinioa mwaka 1997 kijijini kwetu, Likombora mkoani Lindi. Tuna watoto wanne.
Hawara aliyechomwa kisu.
”Mwaka 2003 tulihamia hapa Dar kutafuta maisha zaidi ya Lindi, mwenzangu kazi yake ikiwa ni kuuza kahawa pale karibu na huyo hawara yake aliyemchoma visu. Mimi ni mama wa nyumbani tu.
“Sijui walihitilafiana kitu gani na huyo hawara yake maana leo ndiyo nimejua kumbe mume wangu alikuwa na hawara. Lakini hebu soma meseji hii kwenye simu yangu, alinitumia mume wangu mwanzoni mwa mwezi huu (Februari) bila kuhofia kuwa mimi ni mke wake.”
ILIVYOSOMEKA MESEJI
 “MAMA NEEMA NAKUOMBA MESEJI HIYO ISOME PEKE YAKO NA USIMWAMBIE MTU YEYOTE. MIMI NAJIUA KWA SABABU ESTER HANITAKI. WEWE BAKI NA WATOTO,  NIMEVUMILIA KUKUFICHA NIMESHINDWA. KWA HIYO MIMI NAJINYONGA, WEWE BAKI NA WATOTO.”
Baada ya Uwazi kuzungumza na mwanamke huyo, lilibahatika kuzungumza na dalali mmoja wa magari anayefanyia shughuli zake eneo hilo lakini aliomba jina lake lisiandikwe gazetini.
“Hussein alikuwa akimtuhumu dereva taksi mmoja kwamba anaingilia penzi lake na mwanamke huyo aliyemjeruhi na amekuwa akiahidi kulipa kisasi.
Mke wa ndoa.
“Yaani leo kama jamaa angekuwepo hapa basi ndiye angekuwa wa kwanza kuchomwa visu, pengine huyu mwanamke angefuatia,” alisema dalali huyo aliyeshuhudia tukio hilo.
MGANGA MKUU
Akizungumzia tukio hilo, Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Amana, Dk. Shaany Mwaruka alikiri kuwapokea majeruhi hao na kusema: “Kwa sasa hali za majeruhi zinaendelea vizuri ingawa awali hali ilikuwa mbaya na kusababisha wakimbizwe chumba cha upasuaji kutokana na kisu kilichotumika kuingia sana ndani ya miili.”

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate