EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, April 24, 2015

RAY, BASTOLA UKIIFANYA SHOO, ITAKUTOA SHOO!



Muigizaji Vincent Kigosi ‘Ray’.
INGAWA bado anaonekana kijana mdogo kiumri, tofauti na unavyoweza kumchukulia mtu kama Amri Athuman ‘King Majuto’, lakini katika uigizaji wa filamu, Vicent Kigosi maarufu kama Ray, ni mmoja wa wacheza filamu wakongwe hapa nchini.
Hii ni kwa sababu wao ndiyo vijana wa mwanzo mwanzo kujiingiza katika sinema za kizazi kipya, pale filamu ya Girl Friend ilipofungua pazia mwanzoni mwa miaka ya 2000, kwani kabla ya hapo, tulizoea michezo ya maigizo katika runinga na redio, heshima kwao King Majuto, Mzee Small, Bi Chau, Mzee Jangala na wenzao.
Ninamfahamu kidogo Ray, tangu wakati ule akiwa na Kaole na wenzake wakifanya tamthiliya zilizorushwa na Kituo cha ITV. Hii siyo mara yangu ya kwanza kumzungumzia hapa, kwa maana hiyo, sina maneno mengi yanayoongelea kuhusu yeye ana umahiri gani hasa kwa sababu mashabiki wa tasnia ya filamu watakuwa wanamfahamu vyema.
Ni vigumu kumkuta shabiki wa filamu za Kibongo akiwa hana CD ya Ray, ingawa pia wanaweza kuwa wapo ambao hawathamini mchango wake katika game. Kwa sisi tunaofahamu kidogo, ni jambo lisilowezekana kuizungumzia tasnia hii bila kuliweka mbele jina la Vicent Kigosi.

Ingawa ana jina kubwa katika uigizaji, linalomfanya kuwa miongoni mwa mastaa wanaotazamwa zaidi Bongo, bado nje ya fani yeye ni kijana wa kawaida kabisa, akitoa ushirikiano mzuri anapohitajika na ni mwepesi kuchangia mada katika mazungumzo yoyote yanayomshirikisha. Ingawa wapo wanaodai mshkaji ana nyodo, kwangu mimi sitaki dhambi, sijawahi ona nyodo zake!
Juzikati, Ray alikuwa mmoja wa mashabiki waliojitokeza kwa wingi katika shoo ya Christian Bella pale Escape One, jijini Dar ambako watu wa muziki wa kizazi kipya walipata burudani nzuri kutoka kwa wasanii mbalimbali kama Ali Kiba, Kassim Mganga na mwanadada Alicios Theluji.
Ray alikuwa katika meza moja na washkaji zake, wakiwemo waigizaji wenzake, wakipata kinywaji taratibu huku stori zikiendelea. Lakini katika jambo lisilotarajiwa, wakati mmoja staa huyo alipoinuka, kutokana na ufupi wa shati lake, silaha aina ya bastola ilionekana ikiwa imechomekwa kiunoni mwake upande wa mgongo.
Sifahamu kuhusu mamlaka ya Escape One inasema nini juu ya watu kuingia na silaha ukumbini, lakini shida yangu hasa ipo kwa Ray, kwa sababu nina uhakika wa 100%, silaha ile ilikuwa ni kwa ajili ya ulinzi wake binafsi.
Ulinzi binafsi una maana pana. Maana ya msingi kabisa ni kutambua na kuelewa maeneo na mazingira hatari kwa mmiliki wa silaha, hasa anayetumia kiburudisho, kama ilivyo kwa rafiki yangu Ray.
Nadhani busara inamzuia mwenye silaha ya kujilinda kukaa sehemu yenye uwezekano mkubwa wa kutokea kwa matukio ya kulazimisha matumizi ya silaha.
Katika starehe kama ile kwa mfano, kijana mmoja aliyejilewea zake, anaweza tu kuamua kumvaa staa yeyote kwa kuamini kuwa anajidai au kujisikia. Akamfanyia fujo. Tunajua, mara nyingi baada ya kiburudisho kuanza kufika levo zake, watu huwa hawajali na tena hutamani sana kuwasemea ovyo mastaa.
Ikitokea hivyo, kwa jinsi mastaa wetu walivyo, nao huwa hawakubali, ni wepesi wa kushambulia. Je, ukiwa na ‘mkwaju’ kiunoni, si ni rahisi kupiga, hasa kama mtu atakwambia bastola hiyo toi haina lolote huku anakufuata?
Kuna mengi ya kufikiri, huenda ni kweli ni silaha kwa ulinzi wake au pengine, alifanya hivyo ili kuwaonyesha watu kuwa anamiliki bastola. Kama hili la pili ndilo linalohusika, nimtahadharishe kuwa makini, maana anaweza kujutia uamuzi wake wa kwenda kwenye starehe akiwa na ‘cha moto.’
Na mwisho, nimshauri kubeba silaha katika eneo lile tu analoamini chochote kinaweza kutokea. Kuna maeneo unaweza kwenda na kumudu kujilinda kwa kuchunga kauli tu!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate