EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, April 13, 2015

Yanga haizuiliki


Wachezaji wa Yanga wakishangilia goli.
Na Ibrahim Mussa, Dar es Salaam
HAKUNA kauli nyingine ambayo unaweza kuitumia kwa sasa badala ya kusema kuwa Yanga haizuiliki kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara, baada ya jana kuichapa Mbeya City kwa mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Yanga iliingia uwanjani ikiwa na rekodi ya pekee baada ya wiki moja nyuma kushinda kwa mabao 8-0 dhidi ya Coastal Union kwenye uwanja huo.Matokeo hayo yanaifanya Yanga ishinde mechi tano mfululizo za ligi, ikiwa na maana kwamba tangu ifungwe na Simba Machi 8, mwaka huu imegeuka mbogo na kuanza kutoa vipigo.
Waliokumbwa na vipigo vya Yanga baada ya Machi 8 ni Kagera, Mgambo, JKT Ruvu, Coastal Union na Mbeya City. Lakini Yanga pia imeweka rekodi ya kufunga mabao 18 ndani ya mechi tano zilizopita huku Simon Msuva akitupia matano na Amissi Tambwe akifunga sita katika mechi hizo.
Hii inamaana kuwa hivi sasa Yanga haizuiliki na kila atakayekatiza mbele yake inamtembezea kipigo tu.

“Ukweli tulikuja uwanjani tukihitaji ushindi, lakini hatuna jinsi tulizidiwa na Yanga wakatumia nafasi hiyo kupata ushindi, hakika sasa tunakwenda kujiandaa na mchezo wetu ujao dhidi ya Simba,” alisema kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi.
Katika mchezo wa jana, Yanga walionyesha kiwango cha hali ya juu kuanzia mwanzoni mwa mchezo huo hadi mwisho, hali iliyowafanya mashabiki wao kushangilia kwa muda wote.Ushindi huu unamaanisha kuwa tangu Mbeya City wapande daraja hawajawahi kuibuka na ushindi hata mara moja kila wanapokutana na Yanga wakiwa wamefungwa mara tatu na kutoka sare mara moja.Katika mchezo wa mzunguko wa kwanza, Yanga walifanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 kwenye Uwanja wa Sokoine, Mbeya.
Yanga walianza kuongoza katika dakika ya 18 tu, baada ya mshambuliaji wake raia wa Liberia Kpah Sherman kuifungia timu hiyo bao safi baada ya kumzidi ujanja beki wa City, Juma Nyosso.Hili ni bao la pili kwa mchezaji huyo msimu huu akiwa amefunga bao la kwanza kwenye mchezo dhidi ya Coastal Union wiki iliyopita na sasa anaonekana kuanza kazi.
Bao la pili liliwekwa kimiani na kiungo mstaarabu Salum Telela, katika dakika ya 37, akipiga shuti kali ambalo lilimpoteza kipa wa City. Alipata pasi safi kutoka kwa Mnyarwanda, Haruna Niyonzima.Hili ni bao la pili kwa Telela msimu huu, ukiwa ndiyo msimu alioonyesha kiwango cha juu sana tangu ameanza kucheza soka.
Dakika mbili baadaye, Mbeya City walijipatia bao moja, shukrani kwa bao safi lilofungwa na Themi Felix ambaye aliwazidi ujanja mabeki wa Yanga.Kipindi cha pili hakikuwa kizuri kwa vijana wa Mbeya ambao msimu uliopita walimaliza wakiwa nafasi ya tatu baada ya dakika nne tu Nadir Haroub ‘Cannavaro’ kuifungia timu yake bao la tatu kwa kichwa, likiwa ni la pili kwake kwenye Ligi Kuu msimu huu.
Hii ina maana kwamba wachezaji wote waliofunga mabao ya Yanga jana walikuwa na bao moja moja na hayo ni mabao yao ya pili.Dakika ya 53 Mbeya City walipata pigo lingine baada ya Felix kupewa kadi nyekundu kutokana na kumchezea rafu Telela.
Hata hivyo, rafu hiyo ilikuwa mbaya kwa mchezaji huyo tegemeo kwa Yanga msimu huu baada ya kushindwa kurejea uwanja na nafasi yake kuchukuliwa na Hassan Dilunga.Yanga pia walimtoa Sherman na kumuingiza Mrisho Ngassa.
“Tumepata ushindi kwa kuwa tulitumia vyema nafasi tulizopata mwanzoni, mabao ya haraka yalitusaidia kulinda ushindi wetu, najua kuwa tuna mchezo mgumu wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Etoile, hakika tunajiandaa vyema kukabiliana nao,” alisema Kocha wa Yanga, Hans van Der Pluijm.Katika mchezo mwingine, Stand wameichapa Polisi Morogoro kwa bao 1-0.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate