EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, May 8, 2015

MAMISS ‘VICHWA’ WALIOGOMA KUPOTEA!

Millen Magese.
Na Hamida Hassan
LICHA ya fani ya u-miss hapa nchini kughubikwa na changamoto mbalimbali ikiwemo tabia mbaya mbele ya jamii hususan kipindi cha hivi karibuni, lakini baadhi ya washindi na washiriki wa shindano hilo ambao ni vichwa wamejitahidi kusimama thabiti katika mbio za kukimbizana na mafanikio.
Wapo wachache walioajiriwa na serikali pamoja na makampuni na mashirika binafsi kutokana na ujuzi wa taaluma zao huku wengine wakijikita kwenye ujasiriamali.Hapa chini ni orodha ya baadhi ya mamiss ambao wamegoma kupotea na wanatumia elimu, ujuzi na utundu wao kufanya mambo ya kuwakwamua kimaisha pia kuisaidia jamii. Hawa ni tofauti na wale waliojikita kwenye uigizaji.
Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.
Jokate Mwegelo ‘Kidoti’
Alishiriki shindano hilo mwaka 2006 na kuambulia nafasi ya pili. Nje ya ‘taito’ ya u-miss, mrembo huyu amekuwa ‘akifurukuta’ katika nyanja za ujasiriamali huku akiitumia alama yake ya usoni (kidoti) kama fursa kwani amekuwa akianzisha na kutengeneza ‘projekti’ mbalimbali kupitia nembo hiyo.
Amekuwa akifanya ujasiriamali akihusisha shughuli za urembo pamoja na kubuni mitindo ya mavazi chini ya nembo ya Kidoti. Anamiliki Kampuni ya Kidoti inayojumuisha maduka ya urembo ikiwemo nywele za Kidoti, mavazi, viatu, nguo na  malapa.

Hoyce Temu.
Hoyce Temu
ALINYAKUA Taji la U-miss Tanzania mnamo mwaka 1999. Tangu hapo amekuwa akijihusisha na mambo ya ujasiriamali ikiwemo uandishi wa vitabu ambapo alitoa kitabu chake cha kwanza alichokipa jina la Nakumbuka Yote ambacho kilimwingizia kipato kikubwa kutokana na historia yake kwa jamii.
Mbali na hapo, amekuwa akiwasaidia watu wenye matatizo katika jamii kwa kuendesha Kipindi cha Mimi na Tanzania kinachorushwa na Runinga ya Channel Ten ambacho kimekuwa kikiendesha harambee kwa lengo la kupata misaada kutoka kwa wasamaria wema wanaoguswa.
Millen Magese
HUYU anashughulika na mambo ya mitindo chini ya ‘lebo’ yake ya Magesse Foundation. Ni mshindi wa taji hilo mwaka 2001. Mrembo huyu amekuwa msaada mkubwa kwa jamii kwani anawasaidia wasichana na akina mama wenye matatizo ya uzazi. Pia amekuwa akitoa michango katika elimu ikiwemo madawati na vifaa mbalimbali huku akitarajia kujenga shule mkoani Mtwara.
Faraja Kotta
LICHA ya kushikilia taji la shindano hilo mwaka 2004, huyu kwa sasa ni mke wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Lazaro Nyalandu. Mrembo huyu anatajwa kuwa ni msimamizi wa Kipindi cha Njia Panda (Programme Officer) kinachorushwa kupitia Kituo cha Redio cha Clouds FM.
Mbali na hapo, Kotta amekuwa akijihusisha na uandishi wa vitabu na tayari ameshaandika kitabu cha Unaweza kinachotumiwa na wanafunzi wa shule mbalimbali.
Nargis Mohamed.
Nargis Mohamed
KUTOKANA na taaluma yake, ameajiriwa na benki ya Cooperative Rural Development Bank (CRDB). Alishiriki shindano hilo mwaka 2003 na kushika nafasi ya tatu. Mbali na kuajiriwa katika benki hiyo, Nargis amekuwa akijishughulisha na ujasiriamali kwa kumiliki maduka ya urembo na mavazi ya kike na kupamba maharusi ya Fashionista na Habibity.
Nasreen Karim
‘HILI ni zao’ la Mwanza. Alinyakua ushindi wa taji mwaka 2008. Amejikita katika ujasiriamali wa kuuza urembo wa wanawake wa kabila la Kimasai linalojihusisha na hereni na cheni zinazotengenezwa na wanawake wa kabila hilo. Lengo la kuanzisha duka hilo liitwalo Enjipai  ni kuitangaza jamii ya K-imasai kimataifa.
Nancy Abraham Sumari
ALILITANGAZA Taifa letu kimataifa zaidi mwaka 2005 katika kiwango cha Dunia.  Amekuwa akijihusisha na uandishi wa vitabu ambapo ameandika kitabu kwa ajili ya watoto kinachoitwa Nyota Yako na kukisambaza bure katika shule mbalimbali.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate