EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, May 7, 2015

MREMBO ABABULIWA ‘RECEPTION’

Shani ramadhani INASIKITISHA sana! Muuza baa mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Halima, anajiuguza vidonda vikubwa mwilini vilivyotokana na kumwagiwa maji ya moto na mwanamke ambaye ni mtalaka wa bosi wake ambaye ndiye mmiliki wa baa anayofanyia kazi, Amani linakupa zaidi.
Halima anayedaiwa kumwagiwa maji ya moto.
Kwa mujibu wa chanzo ambacho ni ndugu wa majeruhi huyo, tukio hilo lilijiri mwezi uliopita ndani ya baa moja maarufu iliyopo maeneo ya Ubungo, Dar es Salaam ambapo majeruhi huyo anafanyia kazi baada ya mwanamke huyo kuamini Halima anatembea na mtalaka wake.
Inadaiwa kuwa, mwanamke huyo ambaye ni mtuhumiwa na mwanaume mmiliki wa baa aliyejulikana kwa jina moja la Mushi waliachana miaka mingi iliyopita.“Lakini mwanamke akawa anamfuatilia mumewe kila siku na kwa kila kitu. Ilifika mahali akaambiwa kuwa, mwanaume huyo aliyetengana naye ana uhusiano wa kamapenzi na baamedi wake mmoja.”
“Ndipo siku ya tukio, mwanamke huyo alifika kwenye baa hiyo akitoka kusikojulikana. Wakati huo, Halima alikaa kwenye kiti akiangalia kaunta. Mwanamke huyo alipitiliza jikoni, akachukua sufuria yenye maji ya moto akammwagia Halima bila kujua kuwa, siye aliyemlenga mpaka Halima aliposema ‘siyo mimi’.”

“Kusema kweli baamedi aliungua sana hadi ngozi kuchunika na kuwa nyekundu kama mnyama aliyechunwa. Aliungua sehemu mbalimbali za mwili. Mfano, usoni ndiyo sana! Mgongoni pia, kifuani na mikononi,” kilisema chanzo hicho.
Ilidaiwa kuwa, maumivu ya maji yalimfanya baamedi huyo kulia kwa maumivu makali. Maana wakati anaungua, palepale ngozi ilianza kuchunika na kutoa majimaji ya malengelenge.”

Jeraha alilolipata sehemu ya bega.
“Ni ukatili mkubwa sana kutendeka maana hakuna ukweli wowote kwamba, yule baamedi alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na bosi wake na hakulengwa yeye. Halafu hata kama ni kweli alikuwa na uhusiano naye, yeye walishaachana kwa miaka saba nyuma, sasa wivu wa nini?” kilisema na kuhoji chanzo hicho.
“Ishu ilikwenda kisheria kabisa, walikubaliana kuachana. Wakagawana mali na hata watoto waligawana. Wapo watoto wanne, mwanamke akachukua wawili, wengine wakabaki kwa baba yao.Kikaendelea: “Mbaya zaidi, baada ya ukatili huo, yule mtuhumiwa hakuchukuliwa hatua zozote zile! Hii inaonesha ni jinsi gani wanyonge wanaishi kwa hatari ndani ya nchi yao wenyewe. Pale hakuna cha bahati mbaya bwana.
“Halima hakuwa na pesa za kujitibu zaidi ya kutegemea misaada kutoka kwa wasamaria wema ambao walifahamu kisa kizima. Inauma sana kwa kweli.”Baadhi ya vyanzo vilidai kwamba, baada ya tukio hilo, mtuhu
miwa alitumia pesa kumlaghai majeruhi kwa lengo la kutochukua hatua yoyote na kwenda kumficha mahali akiuguza vidonda.

Baada ya madai hayo, Amani lilimsaka mwanamke anayedaiwa kutenda unyama huo ambapo ilidaiwa anaishi maeneo ya River Side, Ubungo jijini Dar.Hata hivyo, nyumbani kwa mwanamke huyo hakuwepo ambapo baadhi ya majirani walisema alitoka kwenda kwenye biashara zake na muda wake wa kurudi hauna ratiba inayosomeka sawasawa.
...Jeraha alilolipata mgongoni.
Walipoulizwa kama wanajua lolote kuhusu mwanamke huyo kumuunguza kwa maji ya moto Halima, walisema wanatambua lakini walishaombana radhi.“Tunajua, lakini si waliombana msamaha wenyewe kwa wenyewe? Nadhani walipatana,” alisema mmoja wa majirani.
Nacho chanzo hicho kilipoulizwa kuhusu madai ya wawili hao kupatana na kusameheana, kilisema:
“Hakuna kitu kama hicho. Kwanza unajua kwamba, Halima amelazwa Hospitali ya Mwananyamala? Amelazwa kule kwa sababu hali yake bado si nzuri.”

Jitihada zote za kumpata Halima hospitalini hapo hazikufua dafu baada ya mganga mkuu ambaye ndiye aliyetakiwa kutoa kibali cha Amani kuzungumza na majeruhi huyo kuwa bize kwa muda mrefu.
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate