EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, May 29, 2015

Ngassa azuiwa kucheza Sauz


 
Mshambuliaji wa Free State Stars ya Afrika Kusini, Mrisho Ngassa.
Sweetbert Lukonge, Dar es Salaam
UNAWEZA kusema kitumbua kimeingia mchanga! Uamuzi wa kumzuia mshambuliaji Mrisho Ngassa kuitumikia klabu yake mpya ya Free State Stars ya Afrika Kusini, utapitishwa ndani ya siku chache.


Taarifa za uhakika zinaeleza, Ngassa hataruhusiwa kucheza nchini Afrika Kusini alikojiunga na klabu hiyo kwa miaka minne kwa kuwa klabu yake ya zamani ya Yanga imeandika barua kutaka uhamisho wake wa kimataifa (ITC) uzuiwe hadi atakapolipa deni linalokadiriwa kufikia Sh milioni 40.


Taarifa za uhakika kutoka ndani ya Benki ya CRDB zimeeleza Ngassa aliyekopa Sh milioni 45, aliacha kulipa fedha hizo kwa muda mrefu hadi alipoanza kufanya hivyo miezi michache iliyopita.“Kweli hakuwa akipeleka fedha kwenye akaunti yake, hata mshahara haukuwa ukienda na tulipofuatilia tulielezwa kwamba alikuwa akichukulia dirishani, tuliwasiliana na uongozi wa Yanga, mshahara wake ukaanza kuwekwa kwenye akaunti.

“Sasa tumesikia anakwenda Sauz kucheza huko, tumeuliza kuhusu deni letu, ikaonekana Yanga wanataka tuwasiliane naye. Imeonekana ni vigumu kumpata Ngassa, hivyo tumeandika barua ITC izuiwe.“Tumewasisitiza hilo Yanga kwa kuwa ndiyo walimuwekea dhamana. Tunaamini itazuiwa kwa kuwa hata TFF wanajua maana ya utaratibu wa madeni, hivyo tunawaachia kwa muda,” kilieleza chanzo muhimu.

Kwa upande wa Yanga, Mkuu wa Kitendo cha Mawasiliano, Jerry Muro, alisema: “Sijapata hizo taarifa kutoka kwa uongozi, zikifikia basi nitawataarifu.”Gazeti hili liliamua kuwatafuta TFF na msemaji wake, Baraka Kizuguto alisema pia hakuwa na taarifa hizo.

“Hizi kwangu ni mpya, lakini hadi sasa hakuna maombi ya ITC ya Ngassa. Labda barua haijafika, tusubiri ikifika itawasilishwa kwa uongozi na wenyewe utajua cha kufanya ni kipi.”Ingawa juhudi za kumpata Ngassa zilikuwa tatizo kubwa kutokana na simu zake zote kuwa zimezimwa, hata Championi Ijumaa lilipopiga hodi nyumbani kwake bado ikaelezwa hakuwepo, lakini taarifa za ndani za Yanga zinasema wanatambua alilipwa Sh milioni 90.

“Tulisikia ikielezwa Ngassa amelipwa dola laki moja na hamsini (zaidi ya Sh milioni 300), sisi tunajua amepokea Sh milioni 90. Lingekuwa jambo zuri sana kama angemalizana na CRDB, ili aende kwa amani.

“Kweli kuna mpango huo, lakini uongozi ndiyo utashughulikia. Hauwezi kumuacha Ngassa aende na deni halafu klabu isumbuke, nafikiri wasilianeni tena na uongozi unaweza kuwapa ufafanuzi,” kilieleza chanzo cha karibu kabisa na uongozi wa Yanga.
Fedha hizo ni mkopo aliochukua Ngassa ili kuilipa Simba baada ya TFF kumuamuru afanye hivyo kufuatia kubainika alikuwa akidaiwa na Simba baada ya kuchukua Sh milioni 30, huku Sh milioni 15 zikiwa ni kama adhabu.
Kutokana na hali hiyo, TFF ilimfungia Ngassa kucheza mechi sita za Ligi Kuu Bara, pia kulipa faini hiyo ambayo alilazimika kukopa CRDB huku Yanga ikimuwekea dhamana.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate