EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 20, 2015

MMAREKANI NE-YO AMVULIA KOFIA DIAMOND

Diamond Platinumz akifanya yake katika red carpet ya tuzo za MTV.
Musa Mateja
KIWANGO! Ndivyo unavyoweza kusema kufuatia staa mkubwa duniani, Shaffer Chimere Smith ‘Ne-yo’ kuukubali uwezo wa kimuziki alionao kijana kutoka Tandale, Dar es Salaam, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Ijumaa Wikienda linakupa mchapo kamili.
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na ‘Ne-yo’.
Kabla ya Mmarekani huyo aliyewahi kutamba na Wimbo wa Miss Independent kuukubali uwezo wa Diamond, mastaa mbalimbali wa Afrika wakiwamo David Adedeji Adeleke ‘Davido’ na P-Square (Peter na Paul Okoye) wa Nigeria, kwa nyakati tofauti waliwahi kuripotiwa kwenye vyombo vya habari wakiguswa na uwezo wake na kuamua kufanya naye kolabo.

11356934_1658943620994975_821029928_n
Mtangazaji wa Clouds FM, Hamis Mandi aka B-12 aka B-Dozen akiwa katika pozi na Diamond.
TUJIUNGE SAUZ
Kwa mujibu wa chanzo makini kilichoripoti ‘live’ kutoka Durban, Afrika Kusini (Sauz), wikiendi iliyopita kulikofanyika Tuzo za MTV Africa Music (Mama), Ne-yo ndiye aliyekuwa wa kwanza kuonesha shauku ya kutaka kumjua Diamond.
“Jamaa (Ne-yo) yeye mwenyewe ndiye aliyeonesha kuwa na shauku kubwa ya kutaka kumuona Diamond kwa sababu tayari alikuwa anafahamu habari zake na muziki wake.
AMSAKA HOTELINI
“Alilazimika kuanza kumsaka kwenye hoteli aliyofikia Diamond na kubahatika kukutana na meneja wa staa huyo aitwaye Salam. Akaomba amuitie Diamond kwani amekuwa akimfuatilia kwa muda mrefu katika mitandao mbalimbali ya kijamii,” kilisema chanzo hicho.
Wakipongezana.
MENEJA ATEKELEZA FASTA
Kikizidi kumwaga ‘ubuyu’, chanzo hicho kilisema, baada ya Salam kuombwa amuite Diamond, alimuongoza Ne-yo moja kwa moja hadi kwenye moja ya studio iliyopo jirani na hoteli waliyofikia jijini humo na kumkutanisha naye.
WAPEANA ‘HI!’
Kilisema kuwa, baada ya kufika, walisalimiana ambapo Ne-yo alionekana kwa asilimia kubwa kumkubali Diamond kwani baada ya kumuona alimwambia wazi kuwa amekuwa akimsikia mara kadhaa na kufuatilia kazi zake, hivyo siku hiyo alitamani kumuona kabla ya kutumbuiza kwenye hafla ya tuzo hizo.
“Waliongea mambo kibao huku wakipiga picha kisha Ne-yo akapiga picha na kruu nzima ya Wasafi Classic Baby (WCB) na kuondoka na Diamond hivyo kilichoendelea huko sikujua ni nini lakini kama unavyomjua mtoto wa Tandale kwa kutumia fursa, lolote linaweza kutokea,” kilisema chanzo hicho.
Ne-yo katika pozi.
DIAMOND AFUNGUKA
Paparazi wetu, baada ya kumwagiwa ubuyu huo, alimtafuta moja kwa moja Diamond kupitia ‘kiLongaLonga’ chake ili aweke wazi kama kuna ‘project’ yoyote itakayofanyika baada ya kukutana na Ne-yo.
“Nilikuwa zangu sehemu naongea na D-Banj (staa wa Nigeria), meneja wangu (Salam) akaja akaniambia Ne-yo amenifuata hivyo tukakutane naye, akaniambia kuwa amekuwa akisikia Diamond, Diamond, Diamond lakini hatimaye ameniona na amefurahi.
“Jamaa ananikubali mno. Kama hiyo haitoshi jana (Alhamisi iliyopita) alikuwa akihojiwa na Vanessa Mdee, alipoulizwa ni mwanamuziki gani anamkubali sana Afrika akasema ni mimi.
WATAFANYA KOLABO?
“Kuna mambo mengi sana ya msingi tumeongea naye hivyo kwa sasa siwezi kuyaweka wazi lakini kama unavyonijua mwanao huwa sina muda wa kupoteza, nikikutana na watu kama hawa lazima nitumie nafasi yangu bila kuzubaa,” alisema Diamond huku akishiria kuwa kuna kitu tayari wameshapanga kufanya na Ne-yo.
Akiwa na Peter wa P – Square.
DIAMOND APIGA SHOO YA NGUVU 
Mbali na kuwania tuzo hizo za MTV Africa Music (Mama), usiku wa Jumamosi iliyopita Diamond alipiga bonge la shoo katika hafla ya tuzo hizo sambamba na Ne-yo na Davido. Diamond Platnumz ametwaa tuzo ya MTV ya Best Live Act na kuwamwaga wasanii Mi Casa -South Africa, Flavour- Nigeria, Big Nuz -South Africa naToofan- Togo.
11330512_1651455635072048_1703453775_n
…Akiwa amelala baada ya kushinda tuzo hiyo.
NE-YO NI NANI?
Ne-yo mwenye umri wa miaka 35 ni staa mkubwa wa muziki wa RnB duniani aliyewahi kufanya kazi na lebo yenye umaarufu mkubwa Marekani ya Def Jam Recordings inayomilikiwa na rapa Jay-Z
Mbali na kuwa mwanamuziki mkali, Ne-yo ambaye pia ni prodyuza na muigizaji, ameshawaandikia mashairi wasanii wengi maarufu duniani akiwemo Mario (Let Me Love You) wimbo ambao ulikamata namba moja katika chati za Billboard Hot 100.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate