EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, August 21, 2015

JK: Serikali haitasita kufungia chombo cha habari

Wakati pazia la kampeni za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba likisubiri kufunguliwa kesho, Rais Jakaya Kikwete amesema Serikali haitasita kufungia chombo cha habari kitakachotumia uhuru wake kuleta uchochezi na vurugu nchini.
Rais Jakaya Kikwete akikabidhiwa tuzo na
Hiyo ni mara ya pili kwa Rais Kikwete kutoa kauli kama hiyo mwaka huu. Machi wakati wa mahojiano maalumu na Naibu Mkurugenzi wa Azam TV, Tido Mhando kwenye hafla ya uzinduzi wa studio za Kituo cha Televisheni cha Azam, alionya kuwa Serikali haitavumilia vyombo vya habari endapo vitumia uhuru wao kuchochea chuki, vurugu na mifarakano nchini.
Jana, wakati akitoa hotuba yake alipotembelea Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora jijini hapa, alirudia kauli hiyo na kusema; “kama watu watatumia uhuru wa vyombo vya habari kuchochea vurugu tutawafungia… huwezi kupewa uhuru na kuamua kufanya lolote.”
“Ndiyo maana nasema kila kitu kina ukomo wake, uhuru huo (wa vyombo vya habari) hauwezi tu kuwa wa kufanya lolote. Serikali inao wajibu kwa sababu tunaheshimu sana uhuru wa habari. Lakini mkichochea mgogoro kati ya Wakristo na Waislamu, Wagogo na Warangi hili hatukubali kwa sababu mtakuwa mmekwenda nje ya uhuru tunaoutaka,” alisema.
Rais Kikwete alisema aliwahi kuhojiwa na mwandishi wa habari wa Kenya kuhusu kufungia baadhi ya magazeti nchini kuwa ni kukiuka uhuru wa vyombo vya habari, naye akamjibu kwa swali kuhusu uchochezi wa machafuko ya nchi hiyo mwaka 2007.
“Nilimwambia mbona wasiiambie hivyo Mahakama ya ICC… kuna mwandishi wa Kenya ambaye chombo chake kilihusika na uchochezi kwenye uchaguzi na sasa ana kesi... kumjibu vile, yule mwandishi hakuuliza tena,” alisema.
Alitoa mfano wa machafuko yaliyowahi kutokea Rwanda kwamba yalichochewa na vyombo vya habari hadi kufikia hatua ya wananchi wengine kuitwa mende.
Alisema upo uhuru wa kuikosoa Serikali na kwamba ikisemwa inajiweka sawasawa, huku akisisitiza kuwa nchi haijamshinda kama baadhi ya watu wanavyosema.
“Katika kipindi hiki nimejitahidi kuwaachia, watu wako huru, wengine wanamwaga mpaka radhi kama wapo kwenye mdundiko,” alisema.
Kuhusu migogoro ya ardhi, alisema baadhi inasababishwa na watumishi wasiofuata sheria hasa mijini na wananchi kutokufahamu haki zao kuhusu matumizi ya ardhi.
Aliitaka tume hiyo iendelee kutoa elimu ili wananchi wafahamu haki zao.
Mwenyekiti wa Tume hiyo, Tom Nyanduga alimwomba Rais Kikwete kushughulikia suala la bajeti ndogo kwa tume hiyo akisema linakwamisha utendaji wao wa kazi.
“Naamini katika siku 65 zilizobaki unaweza kuisaidia tume kwa kuendelea kuwa wakili namba moja kupigia debe suala hili,” alisema Nyanduga.
Mbali na ombi hilo, Nyanduga alimpongeza Rais Kikwete ambaye anakaribia kumaliza kipindi chake cha uongozi kwa kuiacha nchi ikiwa salama.
“Tume inakupongeza kwa kudumisha utulivu na amani, umesimamia pia haki na misingi ya utawala bora kwa kipindi ulichokuwa madarakani,” alisema.
Alisema katika kipindi chake, Rais Kikwete amesimamia mabadiliko na kuwezesha mhimili wa Mahakama ambayo ni nguzo kuu ya kulinda haki za binadamu, kutekeleza majukumu yake kwa kikamilifu.
Kuhusu mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), alimpongeza kwa juhudi alizofanya katika kukemea mauaji hasa kwa kuhamasisha tume hiyo na wadau kuandaa mpango kazi wa kuyapinga.
“Mauaji hayo yalianza kutia doa nchi yetu hasa kwa mataifa ya nje, lakini kauli yako ya kukemea mauaji na ukatili huo, imeonyesha dhahiri kuwa hukupendezwa nayo,” alisema.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate