EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, October 14, 2015

Jokate, Kiba picha sasa zinaiva

Mwanamitindo Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na mwandani wake Ally Salehe Kiba wakikumbatiana.
MAYASA MARIWATA NA BONIPHACE NGUMIJE
MWANAMITINDO Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na mwandani wake Ally Salehe Kiba, wamethibitisha kuwa wana maelewano mazuri (picha zinaiva) baada ya mwishoni mwa wiki kuonekana pamoja katika bonanza maalum la wanafunzi, lililofanyika katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Jangwani, jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo lililojulikana kama Kidoti Bonanza liliandaliwa maalum kwa ajili ya kuthamini vipaji vya wanafunzi na ambalo lilihudhuriwa na madenti wa shule mbalimbali ambao pia walipata burudani kutoka kwa wasanii na makundi tofauti.
Jokate alikuwa jukwaani pamoja na msanii anayetamba na kibao cha Ni Yule, Hellen George ‘Ruby’ ambaye alishika kipaza sauti na kuwauliza madenti hao kama wanafahamu mtu aliyeimbwa na Kidoti katika kibao chake cha Leoleo ambao wote kwa pamoja walijibu kuwa mtu huyo ni Ali Kiba.

….Wakiwa stejini.
“Hivi nataka niwaulize, mnajua ile nyimbo Jokate aliposema anamvizia anapokatisha akienda mpirani alikuwa kamlenga nani,” aliuliza Ruby ambaye alikuwa ‘akimkata’ jicho Jokate aliyekuwa akiangua kicheko muda wote.
Muda mchache baadaye, Ally Kiba aliwasili eneo hilo akiwa ameongozana na dada yake Zabibu na alipokaribia jukwaani, Jokate alimkimbilia na kumkaribisha kwa busu na baadaye kukumbatiana bila kujali macho kodo ya madenti.
Kama hiyo haitoshi, mkali huyo wa Bongo Fleva alipopanda jukwaani kutumbuiza kwa sapraizi, watu walimgomea na kutaka ampandishe Jokate acheze naye na kujikuta akifanya hivyo, japo mwanadada huyo alionekana kuona aibu kucheza na mwandani wake huyo, wakabaki kuangaliana jambo lililozua shangwe na kuwalazimu kucheza Wimbo wa Chekecha-Cheketua baada ya Kiba kumlazimisha mlimbwende huyo acheze.
Jokate alipoulizwa na paparazi wetu aliishia kucheka na kuomba aachwe kwa muda huo kwa kuwa alikuwa `bize’, lakini ‘King Kiba’ alisema uwepo wake eneo hilo ni jambo linalojionyesha wazi kwani hakuna siri tena.
“Sipendi kuyaongelea hayo mambo, lakini hiyo imeshakuwa gumzo la jiji na nyinyi kama wanahabari kila kitu kinajionesha, kama kusoma huwezi basi hata picha huoni? Kilichonileta hapa ni kumsapoti Jokate sababu kitu anachokifanya ni kizuri na nitamuunga mkono mwanzo mwisho katika kila jambo.”
CHANZO: GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate