MCHEZA sinema maarufu kutoka nchini Marekani, Deidre Lorenz,
anatarajiwa kukimbia mbio za Mount Kilimanjaro Marathon zinazotarajiwa
kutimua vumbi mjini Moshi mkoani Kilimanjaro Juni 24 mwaka huu.
Ofisa Uhusiano wa Kilimanjaro Marathon, Grace Soka, alisema jana mbio
hizo zinatarajiwa kuwa za kilomita 42 na zitaanzia Moshi Club hadi Rau
madukani na kurudi mara tatu na pia kutakuwa na mbio za kilometa 21, 10
na 5 kwa watoto.
Alisema ujio wa mcheza sinema huyo aliyecheza picha mbalimbali kama
‘Santorini Blue’, ‘Perfect Strangers’, ‘The Great Fight’,
unaiweka Tanzania katika macho ya dunia na kuwavutia watalii wengi
kutoka taifa hilo tajiri duniani.
Soka alisema, Lorenz alizaliwa katika Jiji la Oregon nchini Marekani,
lakini akahamia New York City akiwa na kampuni yake ya kutengeneza
sinema inayoitwa Thira Films LLS.
Alisema Lorenz ameshawahi kuteuliwa zaidi ya mara tatu kugombea tuzo
za wacheza sinema maarufu duniani, zinazojulikana kama ‘Grammy’.
“Mcheza sinema huyu, ataambatana na Wamarekani wengine kuja nchini
Juni 24 kukimbia mbio hizo, ambazo zimetokea kuutangaza sana mji wa
Moshi tangu mwaka 1991,” alisema Soka.
Naye mwanzilishi wa mbio hiyo, Marie Frances ana historia ya kuanzisha
mbio na matamasha mbalimbali duniani, ambapo alikuwa pia mwanzilishi wa
mbio za Pyramid Marathon nchini Misri pamoja na Miss Universe Misri,
yaliyojizolea sifa kemkemu.
No comments:
Post a Comment