EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, June 29, 2012

Yanga yawatupia virago nyota 11

MABINGWA wa Soka Afrika Mashariki na Kati, Yanga ya jijini Dar es Salaam, wametangaza kuwatema wachezaji wake 11 kwa ajili ya Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kwa mujibu wa kalenda ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), mchakato wa klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara kuwasilisha majina ya wachezaji wanaoachwa ama kumaliza mikataba unafikia tamati kesho.
Ofisa Habari wa Yanga, Louis Sendeu, alisema jijini Dar es Salaam jana kwamba klabu yake imewaacha wachezaji hao, ambapo kati yao kuna waliomaliza mikataba yao na wengine kupelekwa kwa mkopo klabu nyingine za Ligi Kuu bara.

Aliwataja wachezaji walioachwa kuwa ni pamoja washambuliaji wa kimataifa, Mghana Keneth Asamoah na Mzambia Davies Mwape, huku wengine wakiwa Iddi Mbaga, Julius Mrope, Kiggi Makassi, Atif Amour, Abuu Ubwa, Zuberi Ubwa, Bakari Mbegu, Godfrey Bonny na Shaban Kado ambaye amepelekwa kwa mkopo Mtibwa Sugar.
Aidha Sendeu alisema kikosi cha Yanga kinaendelea na maandalizi yake, ambapo kesho kitashuka katika dimba la taifa jijini Dar es Salaam kucheza mechi ya kimataifa ya kirafiki na mabingwa wa soka nchini Uganda, Express.

Alisema, Express ilitarajiwa kuwasili jijini Dar es Salaam jana, ambapo kiingilio kitakuwa ni sh 20,000 kwa VIP A, sh 15,000 VIP B na C, sh 5,000 kwa watakaokaa viti vya kijani na wale watakaokaa viti vya rangi ya bluu na chungwa watalipa sh 3,000.
Katika hatua nyingine, klabu hiyo leo inatarajiwa kuendesha kisomo maalum ‘hitma’ kwa ajili ya kuwarehemu wanachama, mashabiki, wapenzi na wachezaji wa timu hiyo waliotangulia mbele ya haki, ambapo zoezi hilo litafanyika makao makuu ya klabu hiyo yaliyoko mitaa ya Jangwani na Twiga na kuongozwa na Katibu wa Baraza la Wazee, Ibrahim Akilimali.

“Kama mnavyojua, kila msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara unapokaribia kuanza, huwa tunasoma dua ya kuwarehemu wadau mbalimbali wa Yanga waliotangulia mbele ya haki, hivyo kesho (leo), majira ya saa sita mchana, hapa klabu tutaendesha kisomo hicho ambacho kitaongozwa na Sheikh Akilimali (Ibrahim), hivyo tunaomba Wanayanga kujitokeza kwa wingi,” alisema Sendeu.
Sendeu aliongeza kuwa baada ya dua hiyo, jioni ya leo kutakuwa na mkutano maalumu utakaohusisha wenyeviti na makatibu wa matawi yote ya Yanga ya jiji la Dar es Salaam.
                                 Chanzo cha habari na Dina Ismail wa Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate