EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, July 17, 2012

Wanafunzi hawatozwi viingilio katika mbuga za wanyama Tanzania - TANAPA

Shirika la Hifadhi za Taifa nchini, (TANAPA), limezitaka shule mbalimbali nchini kuacha kuwatoza wazazi fedha nyingi kwa ajili ya safari za watoto wao kutembelea  hifadhi zao kwani wanafunzi hao huingia bila kulipa viingilio kwenye hifadhi hizo.

Hayo yalisemwa na Meneja Utalii wa shirika hilo, Johnson Manase alipokuwa akiongea na Waandishi wa

Habari wa Kanda ya Kaskazini kwenye warsha ya siku moja kwa ajili ya kuhamasisha utalii wa ndani iliyofanyika  kwenye hoteli ya Salsalnero mjini Moshi.

Alisema kuwa TANAPA imekuwa ikishangazwa na kusikitishwa na hatua ya shule hizo kuwabebesha wazazi wa viwango vikubwa gharama wakati lengo la Shirika kutowatoza wanafunzi viingilio ni kuwawezesha wengi zaidi kutembelea hifadhi hizo kwa lengo la kujifunza.


“TANAPA hatutozi wanafunzi viingilio kwenye malango yetu lakini kuna baadhi ya shule zinawatoza wazazi mpaka shilingi 70,000 kwa ajili ya kugharamia safari za mtoto kutembelea hifadhi zetu. Haiwezekani gharama za usafiri, malazi na chakula zikawa kubwa kiasi hicho. Tunawaomba waache kwani viwango kama hivyo vinawashinda wazazi wengine hivyo kuwanyima fursa watoto kuja kujifunza,” alisema Manase.


Aidha,  alikemea tabia mbaya ya “wadaka watalii” maarufu kama “flyc atcher” waliozagaa kwenye maeneo mbalimbali ya jiji la Arusha na mkaoni Kilimanjaro ya kuwasumbua watalii pindi wanapopita kwenye maeneo mbalimbali wakijaribu kuwashawishi kuwaunganisha na makampuni mbalimbali ya uwakala wa utalii.

Manase aliziomba kamati za ulinzi na usalama za mikoa hiyo kulishughulikia suala hilo ili kuwaondolea adha watalii hao ambao kutokana na kubabaishwa na watu hao hupata hofu kubwa juu ya usalama wao jambo alilodai kuwa halitoi picha nzuri ya Taifa.


Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Mawakala wa Utalii nchini, (TATO), Cyril Ako alisema kuwa ni vema mfumo wa ufundishaji wanafunzi mashuleni juu ya maliasili zilizopo nchini ukabadilishwa ili kuwajenga watoto ari na nia ya kujifunza zaidi juu ya maliasili zilizopo nchini.

Alisema kuwa ni vema waalimu wakaanza  kuwafundisha wanafunzi namna wanavyoweza kunufaika na vivutio vivivyopo kwenye hifadhi za Taifa jambo litakalowahamasisha kutaka kuvijua zaidi tofauti na sasa ambapo huwafundisha wanafunzi kwa kuwaorodheshea idadi  ya hifadhi na vivutio vilivyomo ndani yake.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate