Shirika la Hifadhi za Taifa nchini, (TANAPA), limezitaka shule
mbalimbali nchini kuacha kuwatoza wazazi fedha nyingi kwa ajili ya
safari za watoto wao kutembelea hifadhi zao kwani wanafunzi hao huingia
bila kulipa viingilio kwenye hifadhi hizo.
Hayo yalisemwa na Meneja Utalii wa shirika hilo, Johnson Manase alipokuwa akiongea na Waandishi wa
Habari wa Kanda ya Kaskazini kwenye warsha ya siku moja kwa ajili ya kuhamasisha utalii wa ndani iliyofanyika kwenye hoteli ya Salsalnero mjini Moshi.
Alisema kuwa TANAPA imekuwa ikishangazwa na kusikitishwa na hatua ya shule hizo kuwabebesha wazazi wa viwango vikubwa gharama wakati lengo la Shirika kutowatoza wanafunzi viingilio ni kuwawezesha wengi zaidi kutembelea hifadhi hizo kwa lengo la kujifunza.
“TANAPA hatutozi wanafunzi viingilio kwenye malango yetu lakini kuna baadhi ya shule zinawatoza wazazi mpaka shilingi 70,000 kwa ajili ya kugharamia safari za mtoto kutembelea hifadhi zetu. Haiwezekani gharama za usafiri, malazi na chakula zikawa kubwa kiasi hicho. Tunawaomba waache kwani viwango kama hivyo vinawashinda wazazi wengine hivyo kuwanyima fursa watoto kuja kujifunza,” alisema Manase.
Aidha, alikemea tabia mbaya ya “wadaka watalii” maarufu kama “flyc atcher” waliozagaa kwenye maeneo mbalimbali ya jiji la Arusha na mkaoni Kilimanjaro ya kuwasumbua watalii pindi wanapopita kwenye maeneo mbalimbali wakijaribu kuwashawishi kuwaunganisha na makampuni mbalimbali ya uwakala wa utalii.
Manase aliziomba kamati za ulinzi na usalama za mikoa hiyo kulishughulikia suala hilo ili kuwaondolea adha watalii hao ambao kutokana na kubabaishwa na watu hao hupata hofu kubwa juu ya usalama wao jambo alilodai kuwa halitoi picha nzuri ya Taifa.
Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Mawakala wa Utalii nchini, (TATO), Cyril Ako alisema kuwa ni vema mfumo wa ufundishaji wanafunzi mashuleni juu ya maliasili zilizopo nchini ukabadilishwa ili kuwajenga watoto ari na nia ya kujifunza zaidi juu ya maliasili zilizopo nchini.
Alisema kuwa ni vema waalimu wakaanza kuwafundisha wanafunzi namna wanavyoweza kunufaika na vivutio vivivyopo kwenye hifadhi za Taifa jambo litakalowahamasisha kutaka kuvijua zaidi tofauti na sasa ambapo huwafundisha wanafunzi kwa kuwaorodheshea idadi ya hifadhi na vivutio vilivyomo ndani yake.
Hayo yalisemwa na Meneja Utalii wa shirika hilo, Johnson Manase alipokuwa akiongea na Waandishi wa
Habari wa Kanda ya Kaskazini kwenye warsha ya siku moja kwa ajili ya kuhamasisha utalii wa ndani iliyofanyika kwenye hoteli ya Salsalnero mjini Moshi.
Alisema kuwa TANAPA imekuwa ikishangazwa na kusikitishwa na hatua ya shule hizo kuwabebesha wazazi wa viwango vikubwa gharama wakati lengo la Shirika kutowatoza wanafunzi viingilio ni kuwawezesha wengi zaidi kutembelea hifadhi hizo kwa lengo la kujifunza.
“TANAPA hatutozi wanafunzi viingilio kwenye malango yetu lakini kuna baadhi ya shule zinawatoza wazazi mpaka shilingi 70,000 kwa ajili ya kugharamia safari za mtoto kutembelea hifadhi zetu. Haiwezekani gharama za usafiri, malazi na chakula zikawa kubwa kiasi hicho. Tunawaomba waache kwani viwango kama hivyo vinawashinda wazazi wengine hivyo kuwanyima fursa watoto kuja kujifunza,” alisema Manase.
Aidha, alikemea tabia mbaya ya “wadaka watalii” maarufu kama “flyc atcher” waliozagaa kwenye maeneo mbalimbali ya jiji la Arusha na mkaoni Kilimanjaro ya kuwasumbua watalii pindi wanapopita kwenye maeneo mbalimbali wakijaribu kuwashawishi kuwaunganisha na makampuni mbalimbali ya uwakala wa utalii.
Manase aliziomba kamati za ulinzi na usalama za mikoa hiyo kulishughulikia suala hilo ili kuwaondolea adha watalii hao ambao kutokana na kubabaishwa na watu hao hupata hofu kubwa juu ya usalama wao jambo alilodai kuwa halitoi picha nzuri ya Taifa.
Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Mawakala wa Utalii nchini, (TATO), Cyril Ako alisema kuwa ni vema mfumo wa ufundishaji wanafunzi mashuleni juu ya maliasili zilizopo nchini ukabadilishwa ili kuwajenga watoto ari na nia ya kujifunza zaidi juu ya maliasili zilizopo nchini.
Alisema kuwa ni vema waalimu wakaanza kuwafundisha wanafunzi namna wanavyoweza kunufaika na vivutio vivivyopo kwenye hifadhi za Taifa jambo litakalowahamasisha kutaka kuvijua zaidi tofauti na sasa ambapo huwafundisha wanafunzi kwa kuwaorodheshea idadi ya hifadhi na vivutio vilivyomo ndani yake.
No comments:
Post a Comment