EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, August 5, 2012

Makamba: Maisha bora hayawezi kuletwa na JK

BAADA  ya kimya cha muda mrefu, Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM, Yusuf Makamba  ameibuka na kusema kuwa maisha bora kwa kila Mtanzania hayawezi kuletwa na Rais Jakaya Kikwete.

Amesema kuwa mbunge mzuri anaweza kutoka chama chochote iwapo Watanzania watashirikiana naye katika kuleta maendeleo ya eneo husika.

Makamba ametoa kauli hiyo ikiwa imepita muda mrefu tangu aibuke katika kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho (Nec) na kumtuhumu Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye kwamba amekigeuza chama kuwa mali yake binafsi.

Katika kikao hicho Makamba alisema hatua ya Nape kugeuza chama hicho kama taasisi yake binafsi ndiyo ambayo imesababisha kikose mwelekeo.


Lakini jana wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam muda mfupi baada ya mwanaye, January ambaye ni Mbunge wa Bumbuli na Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia kufungua mkutano wa wakazi wa jimbo hilo, Makamba alisema maendeleo ya Watanzania yataletwa na wao wenyewe, kwa kufanya kazi.

Huku akizungumza baadhi ya maneno kwa lugha ya kisambaa na kunukuu baadhi ya vifungu vya biblia takatifu, Makamba alisema Watanzania wamekuwa wavivu wa kufanya kazi na kwamba kila kitu wanategemea kitafanywa na Rais Kikwete.

Makamba alisema kuwa kwa sasa kumezuka tabia ya baadhi ya Watanzania kuwatupia lawama viongozi kwa kushindwa kuwapa maisha bora.
Makamba, alisema kuwa maendeleo hayawezi kuletwa na mbunge peke yake bali kinachohitajika ni ushirikiano wa pamoja ili kuweza kutimiza lengo na ahadi mbalimbali alizotoa.
Alisema kuwa anashangazwa na baadhi ya Watanzania kuamua kumtupia lawama Rais Kikwete kuwa kashindwa kuleta maisha bora wakati hawana umoja wa kuunganisha nguvu katika kutatua changamoto zinazoikabili nchi.
“Hata kama CCM itaondoka madarakani na kuingia Chadema  bado Watanzania wataendelea kulia umaskini kwa kuwa hatuna tabia ya kushirikiana na kufanya kazi,” alisema Makamba.
Makamba alimwagia sifa mwanaye, January ambaye alikuwa akizindua Shirika la Maendeleo Bumbuli (SMB)ambalo alilianzisha baada ya kuwa mbunge mwaka 2010, kusema kuwa kijana huyo ni mfano wa kuigwa na Watanzania kwa kuwa katika kipindi kifupi cha uongozi wake jimboni humo ameweza kutekeleza ahadi mbalimbali.

Alisema kuwa wananchi wa Bumbuli hawakufanya makosa kumchagua mbunge huyo na kuongeza kwamba wanatakiwa kumpa ushirikiano ili kulifanya jimbo hilo kupiga hatua kimaendeleo.

Kwa upande wake, January wakati akiwakaribisha wakazi wa Bumbuli pamoja na waliotoka mikoa jirani, alisema kuwa wamekutana ili kuangalia namna ya kukabiliana na changamoto zilizopo jimboni humo.
Alisema kuwa siku zote maendeleo huletwa na wakazi waliopo mbali na nyumbani hivyo aliwaomba kuhakikisha kuwa na umoja ili kuondoa matatizo yaliyopo jimboni humo ikiwa ni pamoja elimu, afya, miundombinu na maji.
Alisema kwa upande wake atahakikisha BDC, linawasaidia wakazi hao katika masuala ya ajira na elimu.

Alisisitiza kuwa ili kuinua kiwango cha ufaulu katika jimbo hilo wamebuni njia ya kupandisha ufaulu wa wanafunzi kwani kuanzia sasa wameanzisha kambi ya wanafunzi zaidi ya 150 waliofanya vizuri katika mitihani yao ya mokono ili kuwanoa zaidi, lengo likiwa ni kuhakikisha wanafanya vizru katika mtihani wao wa mwisho.

Januari ambaye ni Naibu Waziri wa Sayansi na Mawasiliano, alisema kuwa wamegundua kuwa baadhi ya wazazi jimboni humo wamekuwa kikwazo cha wanafunzi kushindwa kufanya vema mitihani yao.
aliongeza kuwa  BDC imepata fedha kiasi cha Sh 730 milioni kwa ajili ya kukusanya na kununua mazao ya mboga mboga yaliyopo jimboni humo,  hatua ambayo itasaidia kununuliwa kipato cha wakulima.

Alisema hatua hiyo itakwenda sambamba na kukifufua kiwanda cha matunda cha Maweni ambapo mkulima ataweza kuuza mazao yao huko na kuepukana na madalali na kwamba vijana zaidi ya 120 watapata ajira.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate