EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, August 7, 2012

MKAPA NA SIRI ZA FREEMASON




Na Elvan Stambuli
RAIS Mstaafu wa Tanzania, Benjamin Mkapa anaongozwa kwa kualikwa katika hafla mbalimbali zinazofanywa na jamii ya siri (secret society) ya Freemasons, hali inayoonesha kuwa huenda ana siri nyingi za taasisi hiyo, Uwazi limegundua.
Kwa mujibu wa mtandao wa kiongozi wa muda mrefu wa jamii hiyo, Jayantilal Kashavji Chande almaarufu Sir Andy Chande, picha nyingi za Mkapa zimewekwa katika mtandao huo na kuelezwa kile alichokuwa akifanya akiwa na kinara huyo wa Freemasons Afrika Mashariki.

MIAKA 100 YA FREEMASONS
Katika sherehe ya jamii hiyo ya kutimiza miaka 100 tangu waingie Afrika Mashariki iliyofanyika jijini Dar es Salaam Oktoba 9, 2004, Mkapa alialikwa na kuwa mgeni rasmi na sherehe hiyo ilifanywa kwa siri kubwa.
Gazeti hili limegundua kuwa Sir Andy Chande katika mahojiano yake na mwandishi mkongwe nchini, Ernest C. Ambali aliyekuwa akiandikia Gazeti la The Guardian, lililokuwa mitaani Oktoba 8, 2004 hakueleza mahali patakapofanyika sherehe hizo jijini Dar es Salaam lakini alitaja waziwazi kuwa mgeni rasmi angekuwa Rais (wakati huo) Benjamin Mkapa ambaye angefuatana na mkewe mama Anna Mkapa.
Hata hivyo, wakati anasimikwa Chaim Henry Gehl kuwa kiongozi wa Freemasons Israel, ilitajwa kuwa sherehe hizo zingefanyika katika Hoteli ya Royal Palm jijini Dar es Salaam ambapo wageni 350 walihudhuria.

MKAPA, SIR CHANDE UGANDA
Mkapa ameonekana katika picha akiwa na Sir Chande nchini Uganda walipotembelea Kiwanda cha Sukari cha Kakira wakati huo akiwa madarakani mwaka 2005. Haikuelezwa kwa nini walitembelea kiwanda hicho.
Sir Andy Chande katika kudhihirisha kuwa ni marafiki na Mkapa, alimpa nafasi katika kitabu chake kuandika utangulizi ambapo rais huyo mstaafu amesema kazi anazofanya mfuasi huyo wa Freemason kwa jamii ni nzuri.
Aidha, Mkapa amebainisha kuwa mara baada ya kufahamiana na mzee Chande, alimteua kuwa mjumbe wa bodi ya Shule ya Shaaban Robert jijini Dar es Salaam na kufanya naye kazi kwa karibu na ndipo alipoelewa zaidi shughuli za Freemasons ambazo ni za kusaidia jamii.
 
“Mkapa amekuwa akihudhuria hafla nyingi za Freemasons tangu akiwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Tanzania wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere,” alisema Mnajimu Maalim Hassan Yahya Hussein aliyehojiwa na gazeti hili.
Aliongeza kuwa shughuli za Freemasons nyingi huwa ni za kijamii na zinafahamika na karibu viongozi wote wa kitaifa waliopo madarakani na hata wale ambao waliongoza nchi.
 
“Kama kuna siri, basi Mkapa atakuwa anajua maana amekuwa karibu na Sir Andy Chande kwa muda mrefu, tangu enzi za Mwalimu Nyerere” alisema.
Katika mtandao huo, kiongozi wa pili ambaye anaonekana kuhudhuria hafla za jamii hiyo ni rais wa awamu ya pili, Mzee Ally Hassani Mwinyi akifuatiwa na Rais Jakaya Kikwete na hata aliyekuwa Waziri Mkuu, Frederick Sumaye.

MWALIMU NYERERE
Mwalimu Julius Nyerere naye ana picha mbalimbali mtandaoni humo akiwa na Sir Andy Chande na alikuwa akifuatana na Mkapa katika shughuli za kiserikali kwani imeelezwa kuwa kigogo huyo wa Freemasons alikuwa akiaminiwa sana na baba wa taifa kiasi cha kumfanya kuwa mwenyekiti wa bodi mbalimbali za mashirika ya umma aliyoyaongoza vyema.
 
Miongoni mwa bodi alizozisimamia kwa umakini mkubwa ni Shirika la Reli Tanzania (TRC) na Shirika la Usagaji la Taifa (NMC), mashirika ambayo baada ya uongozi wake yalizorota na hatimaye kufa. Sir Andy Chande pia amewahi kuwa Mwenyekiti wa Bodi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania.
Gazeti hili hivi karibuni lilimtafuta Sir Andy Chande kwa njia ya simu ili kuhojiana naye lakini mmoja wa wasaidizi wake, Ramji Suryakanti alisema kiongozi huyo amekwenda nchini India kwa ajili ya kupata matibabu.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate