EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, August 2, 2012

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu ameonya walimu wa shule za msingi sekondari na vyuo

MKUU wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu ameonya walimu wa shule za msingi sekondari na vyuo mkoani hapa kusitisha mara moja mgomo na badala yake warudi kuendelea kufundisha  hasa ikizingatiwa kuwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wanajiandaa kuanza kufanya mithiani yao hivi karibuni.
Wito huo ameutoa jana wakati aakizungumza na walimu wakuu wa shule zote za halmashauri ya Manispaa ya songea  kwenye ukumbi wa chuo kikuu huria mjini Songea,amesema kila mwalimu anapaswa kutambua umuhimu alionao katika jamii hivyo ni vema kuachana na vishawishi vya kuendeleza migomo ambao unatolewa na chama cha walimu.
Mwambungu ameongeza kuwa,kwanzia sasa mwalimu yoyote ambaye hataonekana kuhamasisha mgomo kwa walimu wenzake atachukuliwa hatua kali za kisheria  kwani mgomo huo  siyo halali na tayari serikali imeshapeleka swala hilo mahakamani kwa ajili ya usuluhishi.
Amefafanua zaidi kuwa kila mwalimu kwanzia sasa hahakikishe kuwa anakuwepo katika eneo lake la kazi na anaingia darasani kufundisha na sio kwenda kusaini na kutoka kwani watakuwa wanapita na kuandika majina ya walimu ambao wamehudhuria kazini na kufundisha.
“Naomba muwaambie walimu wote warudi shuleni kufundisha kwani kila kila mtu aliomba kazi peke yake ,na ambao watakahidi agizo hili watachukuliwa hatua za kisheria,na hatuta mvumilia kiongozi yoyote ambaye ataonekana amehamasisha mgomo huo,”alisema Mwambungu.
Aidha,amewashauri walimu hao kuwa wavumilivu wakati serikali inashugulikia madai yao , nao wawape haki ya msingi wanafunzi  hao.
Kwa upande wake  katibu wa chama cha walimu mkoa wa Ruvuma Luya Ngonyani amesema mgomo huo ni halali na upo palepale kwani umezingatia sheria ya ajira na mahusiano kazini hivyo  hali halisi ya mgomo mkoani Ruvuma umeitikiwa kwa shule nyingi za msingi, sekondari na chuo cha ualimu cha Songea.
Ngonyani ameongeza zaidi kuwa ni walimu wachache ambao wameonyesha kutokukubaliana na mgomo huo  lakini bado wanaendelea ili kuwashawishi waungane na walimu wenzao ili kuhakikisha kuwa mgomo huo unakwenda kama CWT ilivyotaka.
Wakati huohuo baadhi ya shule za msingi zikiwemo Matalawe, mfaranyaki, maji maji na misufini zimewarudisha wanafunzi majumbani na kuwataka kurejea shuleni hapo siku ya ijumaa ambayo shule zote zitafungwa rasmi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate