EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, August 6, 2012

Shambulio la mpakani laipa Israel kiwewe


                                   Mpaka kati ya Misri na Israel katika eneo la Sinai
Rais wa Misri , Mohammed Mursi, ameahidi kuwa vikosi vya usalama vya Misri, vitachukua uthibiti kamili wa rasi ya Sinai baada ya shambulio lililotokea kwenye mpaka baina ya nchi hiyo na Israel.

Watu waliojihami kwa silaha waliwauwa walinzi sita wa mpaka wa Misri.
Israel ilisema washambuliaji waliokuwa wamejihami kwa silaha nzito walichukua magari ya kijeshi na kujaribu kulazimisha kuvuika mpaka huo .
Shambulio hilo lilitokea jioni katika kizuizi cha mpakani wakati wanajeshi walikuwa wakifunga kazi tayari kwa futari wakati huu wa mfungo wa mwezi wa Ramadhan.

Televisheni inayomilikiwa na serikali nchini Misri imesema kuwa kundi la watu waliojihami kwa mbuduki na maguruneti ya kurushwa kwa roketi liliwashambulia wanajeshi hao kabla ya kutoweka na gari moja la kivita.
Msemaji wa jeshi la Israel, hata hivyo alisema magari mawili yalitekwa na kwamba moja lililipuka karibu na eneo la kivuko cha mpakani la Kerem.

Gari la pili lililengwa na jeshi la wanahewa la Israel.
Tukio hilo litachukuliwa kama ushahidi wa kutia wasiwasi kwamba wanamgambo wa Kiislamu wanathibiti eneo la kaskazini mwa Jangwa la Sinai.
Wanamgambo hao wamelaumiwa kurusha maroketi kadhaa nchini Israel na kuwauwa Waisraeli tisa mwaka uliopita.

Wakati hali ya wasiwasi ikizidi kutanda Misri imetuma vifaru zaidi na wanajeshi katika eneo la Sinai-Mpango huo ulitekelezwa kwa makubaliano na Israel katika mkataba wa amani wa mwaka 1979.
Israel imeitaka Misri kuchukuwa uamuzi wa mara moja.
Tukio hilo limejiri wakati Israel ikitangaza kuwa inaboresha makombora yake ya masafa marefu aina ya Ballistic kukabiliana na kile inachokiona kuwa tishio la usalama wake linalozidi kujitokeza katika eneo la 

Mashariki ya Kati.
Mradi huo wa kujenga makombora ya masafa marefu unatekelezwa na serikali ya Israel kwa ushirikiano na Marekani.
Hii ni baada ya Iran kutangaza kuwa imefanikiwa katika kufanyia majaribio makombora yake ya masafa mafupi aina ya Ballistic, yaliyoboreshwa zaidi.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate