EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, September 24, 2012

Saintfiet kuifilisi Yanga Sh 201,500,000 milioni

KOCHA Tom Saintfiet amejifananisha na Alex Ferguson wa Manchester United, lakini Yanga italazimika kumlipa zaidi ya Sh 200 milioni sawa na dola 130,000. 
                  Kocha aliyetimuliwa na Yanga, Tom Saintfiet 
Katika mkataba wa miaka miwili kocha huyo aliosaini Julai 6 mwaka huu na Yanga analipwa dola 6,500 (zaidi ya Sh 10 milioni) kwa mwezi na tayari alilipwa taslimu mshahara wa kuanzia Julai mpaka Oktoba jambo ambalo linamfanya adai mishahara ya miezi 20. Yanga ndiyo iliyositisha mkataba huo ambapo kwa mujibu wa sheria za kazi watalazimika kumlipa miezi 20 iliyobaki ambayo ni Sh 201,500,000 milioni. 

Kocha huyo aliiambia Mwanaspoti jana Jumamosi kwa kifupi kwamba hatambui kusimamishwa kwake kwa vile hadi mchana alikuwa hajapewa barua rasmi zaidi ya kusikia kwa watu. "Kulikuwa na kikao kifupi jana (juzi Ijumaa) usiku na uongozi pamoja na wachezaji walikuja hapa hotelini kwangu (Protea-Masaki) kukaibuka majibizano ya hapa na pale na kutoleana lugha chafu na hakikuisha kwa amani. 

"Siwezi kuzungumza sana yaliyojiri waambie viongozi watasema. Lakini sikupendezwa na mambo yaliyotokea, nasikia nimesimamishwa lakini sijapewa barua rasmi wala sina taarifa ninachojua ni kwamba kulitokea kutokuelewana kati yangu na kiongozi mkubwa na tukajibizana sana. "Mwulize yeye atakuambieni alifanya nini, mwulizeni yule dikteta atasema. Wanafanya mambo ambayo siyaelewi kabisa ndiyo maana siwezi kuzungumza kiundani sana hili suala, lakini kama wametangaza kwamba wamenifukuza mimi nasubiri nione nini kitatokea. 

"Niliridhia kuja Yanga kwavile niliona ni sehemu salama ambayo naweza kufanya kazi na kuipa mafanikio makubwa zaidi lakini mambo yamekuwa magumu na nasikitikia mashabiki ambao niliwapenda na walinipa sapoti kubwa mimi na timu ndiyo maana Kombe la Kagame hatukulikosa. "Nilitaka kuwapa makombe zaidi kama zawadi na fadhila kwao na heshima ya klabu, tumekuwa kwenye kipindi kigumu hivi karibu lakini hiyo hali ndiyo ilikuwa inaelekea ukingoni. Yanga itaanza kushinda kuanzia sasa tumefanya maandalizi mazuri ambayo hata kama nisipokuwapo mimi, Minziro anaweza kuipa timu ubingwa. 

"Yanga itakuwa bingwa msimu huu, haya mambo yanayotokea ni ya kawaida kwenye maisha ya soka," alisisitiza kocha huyo mwenye miaka 39 ambaye uongozi umedai kuwa ana kiburi na ni mkaidi kutii maagizo ya mabosi wake. 

AJIBU MAPIGO 
Uongozi wa Yanga umedai kuwa kocha huyo haambiliki na hataki kambi ya muda mrefu, lakini yeye amejibu. "Mimi ndiye kocha wa Yanga na ndiye ninayewajibika kutoa uamuzi wa kiufundi kwa vile ninawajibika kwa kila kitu kinachotokana na matokeo yake. Uongozi hauwezi kunilazimisha niweke kambi wapi na ya aina gani, mimi ndiye kocha. Hata Manchester United huwa hawampangii kocha Ferguson jinsi ya kuweka kambi na kuishi na wachezaji wake kambini. 

Ana mipangilio yake ya kazi kuhusu kambi na huwa uongozi wa juu haumungilii na ndio utaratibu unaofanywa na makocha wote dunia, uongozi haupangi kambi hiyo, ni kazi ya Kocha Mkuu na benchi lake la ufundi. "Mimi ni kocha msomi na mwenye taaluma yangu najua nini cha kufanya na miiko ya kazi yangu naijua, mimi ni profesheno huwezi kunipangia mpaka jinsi ya kuweka kambi. Ni jukumu langu na naweka kambi kutokana na aina ya mechi niliyonayo na ni kitu cha kukumbushana tu na kuwaweka wachezaji kwenye utulivu wa muda mfupi kabla ya mechi. 

"Huwezi kumweka mchezaji kambini muda mrefu ukijiandaa na mechi moja ya ligi, mazoezi ninayowafanyisha ni ya hali ya juu sana na ninamwamini kila mmoja nikijua kwamba anajitambua," alisema kocha huyo huku akikana ukaidi wake. Mwanaspoti ilizungumza na kocha huyo saa tano asubuhi jana Jumamosi akikuwa kwenye taxi na mchumba wake wakielekea ufukweni kujipumzisha na kula wikiendi huku akionekana mwenye mawazo. 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate