EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, September 4, 2012

Watoto wanne ndugu wafa moto

 *Mapacha watumbukia chooni, wafa
Watoto wanane wamefariki dunia katika matukio tofauti wakiwamo wanne wa familia moja waliokufa katika ajali ya moto, huku mapacha wawili wakitumbukia katika choo na wengine wawili kutumbukia katika dimbwi kwenye mikoa ya Ruvuma na Simiyu.

Katika tukio la kwanza, watoto wanne wa familia moja, wakazi wa Mtaa wa Muungano Kata ya Mlingotini Wilaya ya Tunduru mkoani  Ruvuma, walikufa papo hapo baada ya nyumba waliyokuwamo wakiwa wamelala kuteketea kwa moto.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Ruvuma, Deusdedit Msimeki, alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi saa 1:45 usiku katika mtaa wa Muungano mjini Tunduru.

Kamanda Msimeki aliwataja watoto waliokufa kuwa ni Kharidi Nassoro (7) ambaye anasoma darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Muungano; Hamidi Nassoro (6) mwanafunzi wa darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Muungano, Ally Nassoro (4) na Hikani Nassoro (3).

Alisema watoto hao walipata ajali hiyo kwenye nyumba ya Nassoro Hamidi Said iliyopo katika mtaa wa Muungano, ambayo iliteketea kwa moto uliosababishwa na mshumaa.

Kamanda alisema kuwa ajali hiyo ilitokana na kaka wa marehemu hao, Abdulrahi Nassoro,  kufunga mlango kwa nje wa chumba walichokuwa wamelala wadogo zake.

Msimeki alisema kuwa inadaiwa Abdulrahi, mfanyabiashara ndogondogo mjini Tunduru kabla ya kutokea kwa tukio hilo alikuwa amewaandalia chakula wadogo zake na baadaye aliamua kuondoka kwenda kwenye biashara zake huku akiwa amefunga mlango wa chumba walichokuwa wamelala kwa nje.

Kwa mujibu wa Kamanda Msimeki, wazazi wa familia hiyo ambao pia ni wafanyabiashara wanadaiwa kuwa nao wakati ajali hiyo inatokea walikuwa kwenye eneo la biashara yao.

Alifafanua kuwa wazazi hao baada ya kupelekewa taarifa za vifo vya watoto hao, walipata mshituko mkubwa na baadaye walizimia na baadaye kukimbizwa katika Hospitali ya Tunduru ambako wamelazwa na  wanaendelea kupatiwa matibabu.

Msimeki alisema kuwa mshumaa huo uliokuwa umewashwa na Abdulrahi ulidondokea kwenye chandarua ambacho kilishika moto na kuanza kuteketeza godoro walilokuwa wamelalia marehemu hao.

Alisema kuwa majirani baada ya kugundua kuwa chumba hicho kilikuwa kinawaka moto, walijaribu kutafuta njia ya kuwaokoa watoto walikuwa wamelala ndani ya nyumba hiyo.

Majirani hao walipitisha mpira wa maji uliokuwa umefungwa kwenye kisima kirefu cha maji  kwa lengo la kuwaokoa watoto hao, lakini ilishindikana.

Hata hivyo, baadaye walibomoa mlango, lakini walikuta wakiwa wameungua vibaya na kufariki dunia.

Kamanda huyo alisema kuwa nyumba ilikuwa na umeme, lakini  siku hiyo Luku ilikuwa imekwisha na kulazimika kuwasha mshumaa.

Kamanda Msimeki alisema kuwa Jeshi la Polisi mkoani Ruvuma linamsaka Abdulrahi ambaye inadaiwa kuwa baada ya kutokea ajali hiyo alikimbia na kutokomea kusikojulikana.

MAPACHA WAWILI WAFA

Katika tukio la pili, watu wanne wamefariki dunia katika matukio tofauti mkoani Simiyu, wakiwemo watoto mapacha kutumbukia katika shimo la choo.

Mapacha hao walipatwa na mkasa huo wakati wakicheza nje ya nyumba ya babu yao katika kijiji cha Rumwa wilayani Bariadi.

Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Simiyu, Salumu Msangi, aliwataja mapacha hao kuwa ni Kurwa Kija (3) na Doto Kija (3), ambao walitumbukia katika shimo la choo lenye urefu wa mita mbili.

Msangi alisema kuwa tukio hilo lilitokea juzi  saa 11:00 jioni kijijini hapo wakati mapacha hao walipokuwa wakicheza nyumbani kwa babu yao, Kiyumbi Mangu (85).

Alisema watoto hao walikuwa mbali na wazazi wao, akiwamo babu yao na walitumbukia ndani ya shimo hilo na kufariki baada ya kushindwa kupata msaada wa kuwaokoa.

WENGINE WAWILI WAFIA KWENYE DIMBWI


Katika tukio la tatu, wanafunzi wawili wa Shule ya Msingi ya Igongwa katika kata ya Mwigwa wilayani Maswa, mkoa wa Simiyu,  Sado Luhende (12) mwanafunzi wa darasa la tano na Gigwa Luhende (9) mwanafunzi wa darasa la tatu, wamefariki dunia baada ya kutumbukia katika dimbwi la maji wakati wakiteka maji kwa matumizi ya nyumbani.

Kamanda Msangi alisema tukio hilo lilitokea juzi saa 12:00 jioni baada ya mabinti hao kutumbukia katika dimbwi la maji lililo karibu na nyumba yao.

Alisema hakuna mtu yeyote anayeshikiliwa na polisi kuhusiana na matukio yote mawili na uchunguzi kuhusiana na vifo hivyo unaendelea.

CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate