EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, October 26, 2012

MAKOSA MENGINE YA WAZIRI MULUGO KATIKA HOTUBA YAKE HAYA HAPA.


Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Augustino Mulugo wakati akitoa hotuba yake katika mkutano wa wataalam wa elimu huko Afrika Kusini. (Picha na Youtube)

Na Walusanga Ndaki
JANA mtandao huu uliandika makala iliyokuwa na kichwa cha habari ‘MAKOSA’ YA WAZIRI MULUGO NI YA BAHATI MBAYA AU UFAHAMU MDOGO?
Katika makaka hiyo tulionyesha makosa yaliyokuwa ndani ya hotuba ya naibu waziri huyo wa elimu aliyoitoa katika mkutano wa wataalam wa elimu huko Afrika Kusini mwanzoni mwa mwezi huu.

Baada ya wimbi kubwa la malalamiko ya umma kuhusu hotuba yake hiyo iliyokuwa imejaa dosari nyingi, waziri huyo leo alizungumza na kituo cha Clouds FM akikiri dosari hizo japokuwa kwa kujitetea kijanja.
Katika kuonyesha kwamba umakini kwa watumishi wa umma nchini ni mdogo sana,  ni jinsi waziri huyo alivyokuwa akiisoma hotuba hiyo bila hata kushitukia chochote.
Kwanza kabisa, kwa ufahamisho, ni kwamba mfumo wa sasa wa hotuba duniani ni kwamba msemaji anaposoma hotuba yake wakati huohuo huonyeshwa na kompyuta katika kiwambo ambapo washiriki wengine wanaweza kuifuatilia pia kwa kuisoma.
Mtandao huu umeandika yote yafuatayo kwa kufuatilia matamko ya hotuba ya Mulugo ambayo yalikwenda sambamba na hotuba yake ambayo ilionekana kwa ajili ya kusomwa.
Mfano wa kosa la kizembe la Mulugo ni pale aliposema kwamba Tanzania inapakana na nchi nane.  Miongoni mwa nchi hizo nane alizozitaja ajabu ni kwamba nchi ya Burundi haikuandikwa katika hotuba yake japokuwa aliitaja toka kichwani!
Jambo jingine, ni kwamba miongoni mwa nchi hizo zinazopakana na Tanzania aliitaja nchi moja kwa jina la “Congo DRC”, hii ni kwa mujibu wa alivyotamka katika hotuba yake na jinsi ilivyokuwa imeandikwa katika hotuba hiyohiyo. 
Kiuhalisia, hakuna nchi kama hiyo inayopakana na Tanzania. 
Nchi inayopakana na Tanzania miongoni mwa nchi nane alizozitaja ni Congo DR au Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.  Si “Congo DRC” aliyoitaja waziri Mulugo.
Kama Mulugo hakuliona kosa lake na alikuwa bado hajaliona hadi leo wakati anaongea na Clouds FM ni kwamba kirefu cha “Congo DRC” (kama kweli nchi hiyo ipo) ni “Congo Democratic Republic of Congo”!
Waziri Mulugo alisema kwamba neno Zanzibar alilitaja kimakosa kama Zimbabwe wakati wa hotuba yake akielezea nchi zilizounda muungano wa Tanzania, kwa vile msemaji aliyekuwa amemaliza kusema kabla yake alikuwa ametoka Zimbabwe.
Hata hivyo, katika kuisoma hotuba yake iliyokuwa imeandikwa “…islands of Pemba and Zanzibar…” aliisoma kama “…islands of Zimbabwe and Pemba…”.
Angalau kama kweli ni kwa kukosea angeisoma kama “…islands of Pemba and Zimbabwe…”, lakini  kwa vile hakuwa makini, jicho na akili zake vilikimbilia neno ‘Zimbabwe’ kwanza kabla ya kuitaja Pemba ambayo ndiyo ilikuwa ianze, kama hotuba yake ilivyokuwa imeandikwa!
Hebu ona hili lifuatalo!
Katika hotuba ileile, kuna aya iliyokuwa imeandikwa ifuatavyo: “The United Republic of Tanzania is located on the east cost of Africa.”
Hapa kuna makosa mawili yaliyokuwemo katika hotuba hiyo aliyoisoma.   Kosa kubwa la kwanza hapa ni neno “cost” ambalo ni la Kiingereza, maana yake ni “gharama” (likiwa ni nomino) au “kugharimu” (kitenzi).
Hivyo, hilo ni kosa la waziwazi na la kuchekesha na kuchefua lililokuwa katika hotuba ya Mheshimiwa Mulugo!
Neno sahihi lilibidi liwe “coast” yaani “pwani”.  Kwa mujibu wa hotuba hiyo ya Mulugo ambayo huenda aliiandika yeye mwenyewe au kuandikiwa, sentensi hiyo ya “The United Republic of Tanzania is located on the east cost of Africa” ingemaanisha nini?
Ingemaanisha kwamba “Jamhuri ya Muungano ya Tanzania iko mashariki mwa “gharama” (au “gharimu”) mwa Afrika!
Unaona kichekesho hicho?!  Hiyo ni hotuba ya waziri wa Tanzania aliyoiweka kwenye mkoba, akapanda ndege, akafikia hoteli ya kisasa, akala na kulala ambapo kesho yake akaenda mbele ya wasomi wenzake na kupeleka hotuba hiyo ya kusikitisha!
Siyo hivyo tu, Mulugo aliingiza maneno mengine kutoka kichwani ambayo hayakuwemo kwenye hotuba yake hiyo.  Mfano, aliingiza neno “geographically” katika sentensi hiyo kabla ya neno “located”, kitu ambacho kilionyesha wazi hakuwa anaiamini au aliipuuza hotuba yake hiyo iliyokuwa imeandikwa!
Makosa ni mengi ajabu.  La pili ni  kwamba sentensi hiyohiyo aliisoma hivi: “The United Republic of Tanzania is geographically located in east Africa.”
Kwa aliyeisoma vizuri sentensi hii atangundua kwamba ilikuwa na kasoro mbili.  Ya kwanza ni kwamba Mulugo aliongeza neno “geographically” ambalo halikuwa limeandikwa katika hotuba hiyo.  Pili, ukiisoma vizuri sentensi hiyo kuna maneno ambayo aliyaacha katika hotuba hiyo ambayo yalikuwa yameandikwa.
Makosa ni mengi, na yote ni mfano mzuri wa uzembe na kazi za kulipua zinazofanywa na watumishi wa umma karibu katika kila kona.
Cha kusikitisha zaidi ni kwamba uzembe huu wa kisomi umefanywa na mtu ambaye akiwa anazungumza na Clouds FM alijisifu kuwa ni msomi na mtu ambaye aliwahi kuwa mwalimu, lakini uhalisia umeonyesha mapungufu yake makubwa!
Waziri Mulugo ni mmoja tu ya mifano ya kusikitisha na kuudhi inayokwenda kwa jina la viongozi, watu ambao wengi wao wamekuwa ni kichocheo cha kuwakatisha tamaa wananchi wenzao kwa kuwaongezea majonzi ya kiuchumi, kijamii na kisiasa kutokana na kukosa umakini katika kazi zao.
Pia tukio hilo la Mulugo linachochea madai lukuki kwamba uongozi wa nchi hii ni jambo la “kupeana” kirafiki na si lenye kutokana na utaalam au utendaji bora!
Kwa Mulugo, njia ya kujitoa katika aibu hii na kupunguza hasira za Watanzania ni KUACHIA NGAZI MARA MOJA!

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate