EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, October 29, 2012

Taarifa ya Wanaharakati juu ya Gazeti la MwanaHalisi.



              TAARIFA KWA UMMA KUHUSU HATIMA YA MWANAHALISI 


28 Oktoba 2012
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Bidamu (THRD-Coalition), wadau wanaounda mtandao huu na mwanachama mwanzilishi wa Mtandao likiwa  ni shirika lenye  majukumu ya  ya kutetea uhuru wa habari kusini mwa Afrika (MISA-Tan) tunaendelea kwa pamoja kuonyesha kusikitishwa kwetu kwa kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi.

Kwa mara kadhaa sasa tunawakutanisha tena lengo likiwa ni kuendelea kuishawishi serikali ilifungulie gazeti la Mwanahalisi. Kwa vile hoja yetu ya kutaka kuliona gazeti la Mwanahalisi likiwa mitaani haijatimia basi na sisi kwa upande wetu kazi yetu bado haijatimia.

Tunatambua umuhimu wa kuheshimu sheria za nchi, lakini kwa upande mwingine tunaona kwamba ipo haja ya sisi watetezi wa haki za binadamu kupitia kwenye vyombo vya habari na pia kwenye mashirika mengine yanayounda mtandao huu kuishawishi serikali kuachana na sheria gandamizi ambazo ni za kidikteta kama sheria hii ya magazeti ya mwaka 1976 ambayo hukiuka misingi ya haki za binadamu na utawala bora. Pia kwamba maendeleo ya kiteknolojia na kisiasa hapa nchini yanaiweka rehani sheria hiyo gandamizi.

Tumebaini kuwa kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi siyo tu kwamba kunawaathiri kwa kiwango kikubwa wasomaji wake ndani na nje ya nchi bali pia kunaathiri uhuru wa kutafuta, kupata na kueneza habari, kunawaathiri waajiriwa wa gazeti hilo na familia zao na pia kunaiweka katika hati hati hata kampuni nzima ya Halihalisi ambayo ndiyo mchapishaji wa gazeti hilo.

Tunaendelea kusisitiza kuwa sababu walizotumia viongozi wa wizara ya habari kulifungia gazeti la mwanahalisi sio za kweli kwani kilichoandikwa na Mwanahalisi ni ukweli mtupu  ambao hivi karibuni umethibitishwa na  tamko la Dr Steven Ulimboka.

Pia, hivi karibuni Dkt Stephen Ulimboka, kupitia kwa wakili wake Mheshimiwa Nyaronyo Kicheere aliweka wazi kwamba Afisa wa Usalama wa Taifa Ramadhan Ighondu alihusika katika kutekwa kwake  kwa kuwa mazingira yote kabla na baada ya tukio yanaonyesha wazi kuwa Ramadhani Ighondu ni mdau katika tukio hili.

Kinachoshangaza zaidi ni kwamba baadala ya serikali kutoa tamko kwamba sasa imepata uhakika kwamba afisa wake alikiuka kanuni za ajira yake na ingeaza rasmi kuwasaka washirika wa afisa hiyu jambo hilo halijatokea mpaka sasa huku gazeti hili lililosidia kubainisha ushahidi likifungiwa. Zaidi, tulitegemea serikali ingemkana afisa huyo kwamba siyo mwajiriwa wake katika idara hiyo, kama hivyo ndivyo ilivyo, au vinginevyo tungeitarajia serikali itangaze kwamba inachukua hatua za kisheria dhidi ya afisa huyo ambaye ametajwa kuhusika katika makosa ya jinai kinyume cha utaratibu wa mwajiri wake. Pia tungetemea Jeshi la polisi lingetumia fursa hii kumkamata mshukiwa huyu wa Usalama wa Taifa na kulisadia Jeshi la Polisi kuwapata wale waliotekeleza  udhalimu huu dhidi ya Dr Steven Ulimboka. Kwa namna yoyote vitendo vya aina hiyo vinaiabisha serikali na haviwezi kuwa sehemu ya utawala bora ambao serikali yetu imekuwa ikitangaza kwamba inauzingatia.

Mpaka sasa kumekuwapo na matamko mbali mbali kutoka kwa wadau, viongozi wa kiroho, mabalozi na hata Baraza la Habari Tanzania (MCT) likiwa peke yake na hata kwa kushirikiana na wadau wengine wakilaani kufungiwa kwa gazeti hili lakini serikali imeendelea kuwa kaidi katika hili.

Tunachosisitiza

1.      Kwa Serikali

Tunaendelea kuwasihi viongozi wa nchi waone sasa umuhimu wa kukutana na viongozi wa Hali Halisi na kujadili namna ya kulifungulia gazeti hili kwani tayari Dr Steven Ulimboka ameshaweka wazi kilichoandikwa na Mwanahalisi ni cha kweli kabisa. Serikali itambue kuwa suala hili sio dogo katika anga za kidemokrasia na haki za binadamu kwani ubabe wa baadhi ya viongozi serikalini leo unaweza iweka nchi pabaya siku za usoni.

2.      Vyombo vya Habari

Vyombo vya habari pamoja na taasisi mbalimbali katika tasnia ya habari tuweke tofauti zetu pembeni  na kuungana kwa pamoja katika hili na kuhakisha kuwa ukandamizaji wa uhuru wa habari kama huu wa wazi wazi haupati nafasi katika enzi hizi za uwazi na ukweli. Vyombo na taasisi mbalimbali za habari bado mna nafasi na uwezo mkubwa katika kuhakisha gazeti la Mwanahalisi halipotei katika tasnia ya habari hapa nchini.

3.      Jumuiya ya Kimataifa

Kwa kuwa mmekuwa wadau wakubwa wa maendeleo na utekelezaji wa haki za binadamu hapa nchini, tukiwa tunaendelea kuuthamini mchango wenu, tunawasihi muendelee kuishawishi serikali kwa njia za kidiplomasia kuhusu suala la kuheshimu kazi za watetezi haki za binadamu na uhuru wa habari. Nafasi zenu za   kidiplomasia  na uhusiano mkubwa mlionao na nchi ya Tanzania inaweza pia kutumika kushawishi viongozi wa Tanzania walifungulie gazeti la Mwanahalisi.

Kutokana na hali ilivyo ya uvunjifu wa haki za watetezi wa haki za  binadamu ikiwamo haki ya kutoa habari, MISA-Tan, mwanachama wa THRD-Coalition anaehusika na uhuru wa habari  inaandaa  mkutano wa siku moja  utakaowakutanisha  wadau mbalimbali katika tasnia ya habari ili kujadili hatma ya gazeti la Mwanahalisi na uhuru wa habari nchini.

Mwisho Tunawasihi wanaharakati, watanzania  wote wasichoke  wala wasirudi nyuma katika azma hii ya kutetea haki, uhuru na ulinzi kwa haki na watetezi wake. 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate