EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, November 22, 2012

Mahakimu 370 wanalipwa mamilioni bila kufanya kazi.

Na Edson Kamukara
UKOSEFU wa umakini serikalini, umeendelea kuliingiza taifa kwenye gharama zisizo za msingi ambapo sasa mahakimu wakazi 370 wanalazimika kulipwa mishahara bila kufanya kazi, Tanzania Daima limebaini.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili, umebaini kuwa mahakimu wakazi 300 waliajiriwa Juni mwaka huu katika ajira mpya kwa masharti kwamba wangefanya kazi kwenye mahakama za mwanzo.
Baadaye Septemba mwaka huu, mahakimu wengine 70 waliapishwa na kupandishwa kutoka mahakama ya mwanzo kuwa mahakimu wakazi na hivyo kufanya idadi yao kufika 370 ambao hulipwa takribani sh 700,000 kila mmoja kwa mwezi.
Hata hivyo, katika kile kinachoonekana kama kukosekana kwa umakini katika utendaji serikalini, sheria iliyopo sasa kuhusu utendaji wa mahakimu hao ilipaswa kufanyiwa marekebisho kwanza kabla ya wao kuajiriwa.

Kwa mujibu wa sheria ya sasa ya mahakimu na mahakama sura namba 11 kifungu cha sita, ni kwamba hakimu mkazi hana mamlaka ya kukaa katika mahakama ya mwanzo bali mahakama ya wilaya na ya hakimu mkazi (mkoa).
Wakizungumza na gazeti hili, baadhi ya mahakimu hao waliilalamikia serikali kwa kukurupuka kuwapa ajira bila kufanyia marekebisho sheria, na hivyo kuhoji ni kwanini wasipangiwe kazi kwenye mahakama zenye hadhi yao hadi sheria itakapokuwa imebadilishwa.
“Kwa kweli kitendo hiki cha kulipwa mshahara pasipo kufanya kazi ni kama kuhujumu uchumi wa nchi, lakini pia serikali imeamua kuharibu taaluma zetu,” kilisema chanzo chetu.
Kwa sasa mahakimu hao wanaripoti tu kwenye vituo vyao vya kazi na kusaini kitabu cha mahudhurio kisha kuondoka kwa vile hawana kazi maalumu ya kufanya katika mahakama hizo.

“Mikoa kadhaa kama Mwanza na Pwani, majaji wenye uelewa wanawapangia kazi mahakimu hawa kwenye mahakama stahiki. Lakini bado si maeneo yote wanafanya hivyo.
“Serikali ni kweli ilikuwa na nia njema ya kuboresha mfumo wa mahakama ili hawa wasomi wahudumie huko, lakini kwanini wasirekebishe sheria kwanza?” kiliongeza chanzo hicho.
Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe pamoja na Naibu wake, Angela Kairuki hawakuwa tayari kupokea simu na hata walipoandikiwa ujumbe mfupi wa maneno vile vile hawakujibu, hivyo juhudi za kuwatafuta ili wafafanue zinaendelea.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate