EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, November 30, 2012

Poleni tasnia ya sanaa kwa kupoteza wasanii.

Awali ya yote naanza kwa kutoa mkono wa pole kwa wapenda burudani kote nchini kutokana na misiba ya wasanii iliyofuatana, jambo lililoipelekea kuwa na majonzi yasiyokoma.
Awali alianza Maria Khamis ‘Paka Mapepe’ aliyekuwa muimbaji wa muziki wa taarab wa kundi la Tanzania One Theatre (TOT) aliyefariki kutokana kifafa cha uzazi.
 
Wakati watu wakiwa hawajakaa sawa wala machozi kufutika vema usoni au kwa msemo mwingine naweza kusema ikiwa bado tanga halijaanuliwa sawasawa tasnia ya filamu ikaondokewa na Khalid Mohamed a.k.a Mlopelo (41) aliyeng’ara na kikundi cha Kaole kilichokuwa kikirushwa na kituo cha televisheni cha ITV ambako ndiko alikopata umaarufu wake na hatimaye kushirikishwa katika filamu kadhaa.

Wakati msiba wa Mlopelo haujaisha msanii mwingine wa Bongo Movie John Maganga akafariki Jumamosi iliyopita na kuzikwa Jumanne wiki hii.
Wakati kukiwa kuna msiba wa Maganga Jumatatu usiku msanii Ramadhan Mkiteti alipata ajali maeneo ya Maguzoni Muheza mkoani Tanga.
Hakika wasanii na tasnia wamekumbwa na misiba yote ya uchungu; nachukua fursa hii kuwapa pole.
Ni kweli hakuna msiba unaozoeleka hata siku moja kama babu au bibi yako amefariki miaka kadhaa iliyopita, inauma sana.


Kama hiyo haitoshi hata kwa sisi tuliopoteza wazazi wetu kama mimi ambaye sina mama kwa kweli ninaposikia habari ya msiba huumia sana na kunitonesha machungu ambayo ninayo wakati wote.
Vivyo hivyo napenda kuwapa pole wafiwa hasa mama Mlopelo, Mama Sharo Milionea na wazazi wa Maganga kuwa wamshukuru Mungu kwa yote.

Nikiwa nyumbani kwangu ambapo nilifuatilia kipindi cha ‘Take One’ kinachorushwa na televisheni ya Clouds nilimsikia baba mdogo wa marehemu Maganga aliyejitambulisha kwa jina la Deogratius Shija akibainisha kwamba kifo cha mtoto wao kilitokana na uzembe wa wasoma vipimo X-Ray ambapo wao walipofika katika Hospitali ya Mwananyamala walilazimika kupiga picha ili tatizo libainike.
 
Ndipo iliposomeka kwamba alikuwa na tatizo la kutoboka utumbo hivyo akatakiwa kufanyiwa upasuaji na akafanyiwa upasuaji lakini hali yake haikutengemaa.
Maskini pindi alipopewa uhamisho wa kwenda kutibiwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili (MNH), ambako ndiko kwenye mashine kubwa za kuweza kumsaidia kupumua akiwa huko ndipo akapatiwa vipimo vingine nao wakagundua kwamba bandama lilipasuka hivyo upasuaji aliofanyiwa katika Hospitali ya Mwananyamala ulifanyika kwa makosa.

Kama hiyo haikutosha tabibu bingwa wa magonjwa hayo alikuwa amemaliza muda wake wa kazi hivyo ndugu wakaambiwa wasubiri hadi ambapo angeliingia kazini kesho yake.
Ikumbukwe kwamba wakati huo marehemu Maganga alikuwa akipumua kwa msaada wa mashine hospitalini hapo.

Lakini hadi tabibu anafika alfajiri hali haikuwa nzuri kwani hata upumuaji wa mgonjwa ulikuwa wa taabu licha ya kusaidiwa na mashine.
Inasikitisha na inauma sana jinsi hali ilivyo na kifo cha Maganga kilivyotokea ni uzembe mtupu.
Jamani mbona hali inatisha kwenye hospitali zetu za serikali? Kwa nini iwe ni wao tu kila mara ni Mwananyamala tu? Hebu wahusika tupieni macho suala hili.

Waangaliwe wasoma vipimo na hata huyo tabibu na jopo lake waseme wazi kama kweli walipomfanyia upasuaji ni kweli walikuta utumbo umetoboka kwani hapa hakuna anayeweza kusema mkweli ni nani. Hivi wizara husika haisikii kadhia zote hizi zinazowakuta wananchi wake?
Nimeguswa na sana na vifo hivi huku kila mmoja akiwa na sababu yake iliyosababisha afe lakini sababu ya Maganga ni uzembe wa baadhi ya matabibu wetu hawakuwa makini kuanzia hatua ya awali.

Huenda wakati mwingine inawezekana ikawa ni uchakavu wa vifaa vya hospitalini kwetu lakini kwa nini iwe hivyo?
Jambo lingine lililonishtua ni kusikia kwamba walishindwa kumwekea mashine ya kupumua kwa sababu iliyopo katika Hospitali ya Mwananyamala haina nguvu hivi ni wagonjwa wangapi wanaopoteza maisha yao hospitalini pale?
Kumbe Mwananyamala kuna siri tena nzito ambayo imefichuliwa na kifo cha Maganga; siri hii ni kumsababishia maumivu makali yaliyosababisha kifo chake, walimkata utumbo pasi na sababu ya kufanya hivyo ilhali ana tatizo lingine na mashine zao hazina nguvu.

Huu ni ukatili kwa baadhi ya watendaji wa serikali kwa kutokuwa makini na kujali wananchi wake ambao wanakufa kwa kulazimishwa kwa matibabu yasiyokidhi na vifaa duni.
Na ni serikali hii hii itakayokaa kimya bila kulitolea ufafanuzi suala hili. Inasikitisha imekuwa ni mazoea sasa kwani historia ya matabibu wasiozingatia weledi inazidi kuandikwa, walipasuliwa wagonjwa kichwa badala ya mguu na mguu badala ya kichwa serikali hiihii ilikaa kimya.
Ndugu wa wagonjwa walishtaki hasa yule aliyepasuliwa kichwa kwani tayari amepewa ulemavu asiokuwa nao.

Vivyo hivyo kama mapenzi ya Mungu yasingetimia kwa kumchukua Maganga ina maana na yeye tayari alikuwa amepewa ulemavu wa utumbo wake na je angeishi vipi katika hali ile endapo yasingemkuta mauti?
Majibu ya hayo yote yanabaki kwa kila mmoja kujitafakari na kuchukua hatua.
Poleni wafiwa wote kwa yote yaliyowakuta; ni mapenzi yake, kila nafsi lazima itaonja mauti sawa lakini mauti nyingine husababishwa na baadhi ya matabibu wasiokuwa makini na kazi zao.
Huu ni mtazamo tu kwenu matabibu na wauguzi wala msiniwekee chuki.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate