EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, November 1, 2012

Umeme wawapa hofu ya ugonjwa Njiro-Arusha.


WANANCHI wa Njiro jijini hapa wamedai kuwa wako hatarini kupata maradhi ya saratani kufuatia hatua ya Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (Tanaesco) kubadili matumizi ya ardhi ya eneo walilokuwa wakilitumia kusambaza umeme na kulitoa kwa kampuni ya Symbion Power (T) Ltd kufua umeme.Aidha wamedai kuwa TANESCO hawajafanya tathmini ya athari za mazingira kama sheria inavyoagiza.

Wananchi hao kutoka vitalu B, C, na D wanadai kuwa mitambo mikubwa iliyofungwa kwenye kitalu C inayozalisha megawati 66 inasababisha kelele, mitikisiko inayosababisha nyufa kwenye nyumba zao, moshi wenye kemikali unaosababisha uchafuzi wa mazingira na kuhatarisha usalama wa afya zao.Tayari wananchi hao wamefikisha malalamiko yao kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magessa Mulongo, kwa barua iliyosainiwa kwa niaba yao na wananchi sita tokea Septemba 4 mwaka huu lakini wanadai kuwa licha ya mkuu huyo kuahidi kushughulikia suala hilo, hawaoni mabadiliko yoyote.

Mmoja wa wananchi hao, Gelase Rutachubira, aliieleza  jana kuwa walimuomba mkuu wa mkoa achukue hatua za haraka ikiwemo kusimamisha shughuli kwenye eneo hilo ili kunusuru afya na makazi yao.Kwa upande wake Mulongo alikiri kupata malalamiko hayo ambapo alisema kuwa kuyashughulikia ina maana awaagize TANESCO kusimamisha uzalishaji huo wa umeme jambo alilodai kuwa hana uwezo nalo kwani kwa sasa nchi inahitaji nishati hiyo ya umeme.
Alisema anachoweza kufanya ni kukutana na uongozi wa TANESCO kuona namna wanavyoweza kuboresha shughuli zao kwa kutumia teknolojia nyingine itakayowezesha kuzuia kelele, mitikisiko na uchafuzi wa hewa hata hivyo alidai kuwa shughuli kwenye eneo hilo hazifanyiki muda wote wa siku.

Aidha barua nyingine toka Baraza la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira Nchini (NEMC) yenye kumbukumbu namba NEMC/ 513/Vol 1/148 ikimjibu mwananchi wa eneo hilo, Method Mukurasi, aliyelalamikia kampuni hiyo ilidai kuwa tathmini ya mazingira kwenye eneo hilo ilikuwa bado haijafanyika hivyo wangefika kwenye eneo hilo kwa ajili ya kuifanya na wangempa taarifa.Hata hivyo juhudi za kumpata msemaji wa TANESCO kuzungumzia suala hilo ziligonga mwamba kutokana na simu yake ya kiganjani kuita bila kupokelewa.Habari na Grace Macha, Arusha.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate